sweetlady
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 16,947
- 8,409
Mzima kabisa Lizzy ila alisumbuliwa na sifa za kijinga, kuna siku moja police walimkuta amepaki gari vibaya wakamwuliza kulikoni?..badala ya kujibu akaanza kuchomoa noti moja, moja na kuzichana mbele yao, wakamkamata na kumsweka kwa masaa kadhaa ila walimwachia kwa nguvu ya pesa... Ila mungu alivyo wa ajabu alianza kuishiwa na kuuza kila kitu haikusaidia, mwisho wa siku akawa anatembeza viatu mjini tena anabeba mkononi na bado mungu akampiga fimbo, hivi yupo kibosho hana A wala Z, anakunywa mbege tu sasa. Mungu hajaribiwi ati.Loh, alikua mzima kweli?
Wakati nasoma nilijua anakusanya alafu anawapa aua hata anazirusha juu wagombanie.
Kweli wanadamu tunatofautiana.