mimi ni baba wa familia(nimeoa) kabla ya kuoa nilikuwa na rafiki yangu wa kike ambae nilidumu nae kwa miaka mitatu hivi. nilipokuwa tayari kuoa nilimtaarifu mwenzangu kuwa nataka kujitokeza kwao aliniambia kuwa kwa wakati huo hayupo tayari kuolewa kwa sababu bado hajajiandaa na wazazi wake hawawezi kukubali na pia alikuwa na plan ya kuendelea kusoma. kwa sababu nilikuwa nimeweka malengo yangu kuwa ikifika age fulani nioe nilichukua uamuzi wa kutafuta mtu mwingine aliyetayari kuolewa na mungu si athumani nikampata. baada ya kumpata nilitumia busara yangu kumjulisha kuwa nimeamua kutafuta mwingine aliye tayari kuolewa na nimeshampata so no need kuendelea kuwa na mahusiano nae, alikubali ingawaje kwa shingo upande na kwa kulia sana baada ya hapo tuliendelea kuwasiliana kama marafiki wa kawaida kwa sababu hatukugombana. sasa ni miaka mitatu imeshapita ametokea kuwa karibu tofauti na ilivyo kawaida na pia amekuwa akilalamika kila siku kuwa boyfriend wake hamkidhi mahitaji yake(sex) nimekuwa nikimshauri awe mvumilivu na ampeleke kwa washauri wa mahusiano lakini kali ni last week alipoanza kuniambia live kuwa hatokuwa na maana yoyote kama hatozaa nami maana ni mwanaume pekee ambaye nimebaki na nafasi katika moyo wake so anachoomba yeye si kurudiana bali niweze kuzaa naye ili iweze kuwa kumbu kumbu yake for rest of her life, kwangu imekuwa ni mtihani sana kwa sababu ya urafiki wetu hata baada ya mimi kuoa. ushauri wenu wanajf