Ex-GF kajitangaza anao, napata kero vibaya

Kuna demu alikuwa girlfriend wangu zamani, majuzi kaonekana kitaa anahamasisha masuala ya UKIMWI na amejitangaza laivu kuwa na yeye pia anayo ngoma. Washkaji kibao wanaelewa nilikuwa namega. Lakini mie siku zote nimetumia kondomu. Sasa tangu amejitangaza huyo demu napigiwa simu na sms kibao za kunipa pole kama vile nami pia nina ngoma! Kwa kadri ninavyojua ngoma inaenea kwa kufanya ngono zembe, na mimi sikufanya hivyo hata siku moja.

Najua hata nikitangaza redioni kuwa mi sina ngoma watu hawataniamini, na sasa naona hata mchumba nitakosa, maana hii habari ni mbaya kinoma!

Nishaurini wakubwa. Naomba msinishutumu mnaposhauri, sikupanga yatokee kama yalivyotokea. Nifanyeje niaminike? Tabia flani mbaya nilizokuwa nazo zamani zote nimeacha, lakini naona hii ya huyu demu kujitangaza itatibua kila kitu!
Nenda kapime ujue afya yako na uondokane na huo msongo wa mawazo!!
 
Wakubwa jana ndio ilikuwa siku ya appointment yangu ya confirmation test, na niliiwahi vizuri. Nashukuru tena nimepata jibu lilelile, kwamba sijaambukizwa. Nina furaha kupita kiasi. Na sasa sijali lolote atakalosema mtu yeyote, majibu yangu yameniridhisha kabisa na kuniondolea hofu. Na sitaki tena demu. Kama mke, sawa, lakini kipimo mbele kama tai!

Hongera sana mkuu hasa kwa kujitolea kwenda kupima, wewe ni balozi mzuri... na pia pole kwa wasiwasi!!!
 
Mkuu,bila kurefusha hadithi, nenda kapime, vinginevyo utaishi kwa wasiwasi na utajitia maradhi ya fikra bure(stress)

naungana na julius, wala usippate hofu ya bure na wala usijepe matumaini kuwa uko -safe wakati huna uhakika. la muhimu hapa ni kupata vipimo vya kitaalamu, UKIMWI haupimwi kwa macho kaka, nenda kapime upate uhakika, kama unao pole sana lakini kuna namna ya kuishi na ukimwi na ukaendelea na shuhguli zako kama kawaida, na kama huna utajua namna ya kujikinga na kuwa mwangalifu zaidi katika mahusiano, mbona simple tu kama kumsukuma mlevi vile!??
 
Mkuu MTM hiyo niliyobold ndiyo ambayo siiwezi kabisa, naiona ngumu kupita kiasi wala sitaki kuifikiria. Unajua kila mtu na roho yake bana, kuna anayeona kujitangaza ana ngoma ni poa, lakini mie kweli siwezi hata kidogo. Kwani lazima anayepima ajitangaze? Au kwani ni lazima anayeunga mkono mapambano dhidi ya UKIMWI kwani lazima naye aseme anao?

Ni maoni yako lazima yaheshimiwe, lakini je ukisikia dawa ipo tayari utakuwa radhi kujitangaza? ni swali tu na pole kwa masaibu yote vumilia si wanasema time will tell?

.....................................
Amani yetu inatumiwa vibaya
 
Mtu B wala usiwe na hofu, Ngoma sio big deal, watu kibao wanayo na wanaendeleza maisha kama kawaida. Wewe kapime ili ujue status yako then uangalie what next baada ya kujijua kama ni HIV negative au positive.

Mimi binafsi namjua mtu ana ngoma sasa yapata 20 + yrs na ukimuona mpaka uambiwe hvhv humjui na ni kiongozi fulani kule shidefa plus au shilika gani sijui yale ya mwanzomwanzo....... so dont ever loose hope maisha yapo upande wako acha huzuni zisizo na mpango.

............................................
Amani yetu inatumiwa vibaya
 
Hongera sana Mtu B, ukweli ni kwamba nilipoanza kushuka na thred sikusoma tarehe hivyo michango yangu iliyotangulia ilikuwa ya kukutia nguvu. na sasa baada ya kukaribia kufika stand yaani mwisho wa thred ndoo nikagundua tofauti (Mambo ya kutumikia Taifa usiku)...
kwa mara nyingine hongera na pole kwa msukosuko wa mawazo naamini chakula kilikuwa hakishuki kwenye kipindi cha mpito.

...................................
Amani yetu inatumiwa vibaya
 
Back
Top Bottom