Ndugu wana jf. Ni wiki chache zimepita toka waziri wa fedha atangaze bajeti ya nchi iliyo kuwa na mambo kadhaa moja wapo ni la kuongeza kodi katika mafuta ya taa na kupunguza kodi kwa petroli na diseli lengo likiwa ni kufuta kabisa tatizo la uchakachuaji. Nionavyo mimi na ndivyoilivyotakiwa kuwa kwamba kabla ya maamuzi haya lazima wizara ilikutana na wataalamu wa ewura na kujadiliana ndio wakafikia maamuzi haya. Chakushangaza mpaka sasa baada ya bei ya ewura kutangazwa vituo vyote vimetupilia mbali mapendekezo ya kushusha bei na kupandisha bei kama ewura na wizara ya fedha ilivyotaka. Kwa sasa bado mafuta ya taa yanauzwa kwa bei ya chini kuliko diseli na petroli, je huu si ushahidi tosha kwamba hawa ewura hawaijui sekta hii ya nishati wanayotakiwa kuiongoza? Je ni kweli kuondoa hii kodi iliyopendekezwa na wizara na ewura kutapunguza bei ya mafuta? Au kunamchezo humo ndani wa kuwanufaisha wafanyabiashara na kuikosesha serikali mapato hatimaye mlala hoi akose dawa hospitali?
Kwa maoni yangu
1. Ewura na wizara walitakiwa kukutana na wadau wa nishati na kujadili suala la uchakachuaji na kupata suluhisho
2. Kabla ya kuongeza kodi katika mafuta ya taa ilitakiwa watoe mbadala wa mafuta ya taa ambayo hutumiwa na 97% ya watanzania.
3. Kodi iliyoongezwa katika mafuta ya taa ingetolewa katika gesi.
4. Serikali ingetoa elimu ya matumizi ya biogesi bure vijijini kwa wale wenye mifugo.
Kwa maoni yangu
1. Ewura na wizara walitakiwa kukutana na wadau wa nishati na kujadili suala la uchakachuaji na kupata suluhisho
2. Kabla ya kuongeza kodi katika mafuta ya taa ilitakiwa watoe mbadala wa mafuta ya taa ambayo hutumiwa na 97% ya watanzania.
3. Kodi iliyoongezwa katika mafuta ya taa ingetolewa katika gesi.
4. Serikali ingetoa elimu ya matumizi ya biogesi bure vijijini kwa wale wenye mifugo.