- Thread starter
- #21
Jambo la kwanza inaonyesha kwa sasa wewe humpendi tena huyo binti. Mi nakushauri ukae upime upendo wako kwake, kama upendo umeisha ghafla mwambie ukweli na uachane nae.
2. Kama bado unampenda, kupenda pesa na kwenda disco siyo tatizo la kimsingi. Anapendaje pesa? Je, anaomba pesa kwa wanaume wengine? au anakuomba wewe? kama anakuomba wewe na inapilitiza basi kaa chini umulize pesa anazoomba anafanyia nini? hilo ni jambo dogo tu, hata hivyo kila mtu anapenda pesa coz ndiyo maisha yenyewe. Kuhusu kwenda disco ni hobby tuu hiyo na ina rika lake, kama haendi disco kwa mabaya (kutafuta wanaume) hapo hakuna tatizo. Wangapi wanaenda disco bana au unamtafutia sababu za kumpiga chini?
3. Wewe ulimpenda wakati ukiwa mdogo, ila baada ya kupotezana na kuonana baadae ulimtamani tu. Sasa umekuta mambo uliyokua unatarajia hayapo unataka kukimbia. Mwambie ukweli na muachane kwa amani kama mlivyokubaliana kupendana.
Mkuu umenena vyema sana, natakiwa nchukue uliyoyasema niyafanyie kazi. Shukrani