Eti mke bora hutoka kwa mungu?


Orait Seto, kama wengine walivotangulia kusema hili ni swala la kiimani zaidi, kutegemeana na jinsi wewe unavyoamini na unavyomwamini Mungu wako. Haijalishi watu fulani wanafundisha nini si kazi yetu kohoji hilo, haijalishi wanasema uombe kwa jinsi ipi hio ni imani yao

Swala hapa wewe unataka mke wa jinsi gani na unaamini nini katika hilo, Je unaamini Mungu anaweza kukupa hitaji la moyo wako??

Kutoka na mimi ninavyoamini, Mungu anakupa mume/mke mwema kwa wakati sahihi. Na sio lazima ukutane nae kanisani au msikitini. Unaweza ukakutana nae baa, anaweza kuwa changudoa, anaweza kuwa jambazi, anaweza kuwa ktk mazingira mabaya sana lakini wakati wa Mungu ukifika anamtoa huko, anamleta kwako.

Mke mwema/mume mwema ni yule ambaye utaishi nae kwa furaha na amani. Mnaweza kuchukuliana madhaifu yenu, kushirikiana nae na nafsi yako ina uhuru nae.
 
Just for Argument Sake.....
Hivi kuna kitu kama mke asiye bora?
Na kama yupo ni nani ambaye anafaa amuoe huyo?
Na kama Mungu anatupenda wote sawa, kwanini anichagulie mimi mke mbaya na wewe akupe mzuri?
Na je Mke akiwa bora na katikati ya ndoa akawa mapepe na hapo ni nani wa kulaumiwa?
Na wewe kama sio bora, je unahitaji mke bora?, kwanini huyo mwanamke bora abebe mzigo wa wewe ambae sio bora?

Haya ni baadhi tu ya maswali kwa yeyote awezae kunijibu....

Asanteni

mke asiye bora ni yule asiyekupendeza wewe, na kama hakupendezi wewe kuna mwingine atapendezwa naye hivyo bado ana nafasi yake ya kuolewa.
Mungu anatupenda wote na humpa mtu kile anachokiomba, kama umeomba upate mke mwenye tabia njema, utapewa huyo huyo, unataka mwenye sura nzuri mungu atakupa huyo huyo. Inabidi tumuombe mungu kile tunachostahili (what we deserve) na sio tunachohitaji(what we need) inawezekana tunastahili makubwa ila tunaomba madogo.

Tabia ya mtu hubadilika muda wowote, nafikiri tabia ulizokuwa nazo miaka 10 iliyopita inawezekana sio tabia yako uliyonayo sasa na inawezekana miaka 10 ijayo ikabadilika tena.
Kama mke atakuwa mapema, wa kulaumiwa anaweza kuwa yeye mwenyewe au mume au hata mazingira anayoishi yanaweza kuchochea.
 
huo ni ulimbukeni na kutojiamini,mke bora halafu uende kwa mchungaji au pasta akuombee,wengi wao ndiyo wanaonja kidogo then wanakupa wewe ni uongo mtupu,jiaamulie kusoma kitabu cha mungu cha imani yako muombe mungu na kisha funga na pia angalia yupi akufaaye the utaona tu kuwa fulani unampenda na kikubwa ni mazingira,kama upo moro huwezi kuoa bukoba au mtwara,definitely utaoa moro au dar,pwani,iringa au dom maeneo ambayo macho yako yanafika kwaharaka na kirahisi

haya ndugu, nimekusoma.
 
Cool Hus na LD..., Mmemaliza, na mnenijibu Vizuri Sana.... No Comment.. (Just Thanks)... Nimewakubali :)
 
Back
Top Bottom