MpigaFilimbi
JF-Expert Member
- Apr 30, 2008
- 1,169
- 182
Utafiti unasema kuwa lugha ya kisukuma ndio inazungumzwa na watu wengi kuliko kiswahili.
Na Abeid Poyo
MRADI wa Lugha za Tanzania (LoT) umezindua atlasi ya lugha na kuitaja lugha ya Kisukuma kuwa na wazungumzaji wengi nchini.
Katika uzinduzi huo uliofanyika jana katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, lugha ya Kisukuma ilitangazwa kuwa na wazungumzaji wapatao 5, 195, 504 ikifutiwa kwa mbali na lugha ya Kiswahili yenye wazungumzaji 2,379,294
Akizungumza katika hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa lugha kutoka ndani na nje ya nchi, Mratibu wa mradi huo, Prof Josephat Rugemalira alisema atlasi hiyo ya aina yake inatoa picha halisi ya idadi ya lugha zilizopo nchini, wazungumzaji, maandiko, usambaaji wake na maelewano ya karibu ya lugha.
Atlasi ya lugha za Tanzania ni kiungo muhimu katika mkakati wa wa kuzitambua na kuzitathmini rasilimali zetu za utamaduni, alisema Prof Rugemalira na kuongeza kuwa, uzinduzi wa atlasi hiyo unatoa picha halisi ya maendeleo ya sekta ya lugha nchini.
Kwa mujibu wa Rugemalira, atlasi hiyo ni matokeo ya utafiti wa miaka kadhaa wa mradi huo ulio chini ya Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Alibainisha kuwa utafiti huo pia ulibaini kuwepo kwa lugha 150 hapa nchini huku baadhi yake, kama vile lugha za Wanda, Kiga, Kikuyu na Bwali zikiwa hatarini kufa kwa kukosa matumizi.
Alifahamisha kuwa lugha hizo zimekumbwa na hali hiyo kutukana na mambo mbambali ikiwemo lugha hizo kumezwa na lugha kuu.
Katika hafla hiyo, machapisho 20 zikiwemo kamusi 18 za lugha za asili zilizinduliwa na Balozi wa Sweden nchini Staffan Herrstrom aliyekuwa mgeni. Hafla hiyo ilikwenda sambamba na maadhimisho ya Siku ya Lugha Mama duniani.
Source: Gazeti la Mwananchi
Wazo langu:
Utafiti huu bila shaka haukuangalia overlap ya hizi lugha, kama kuna watu wanaozungumza kiswahili na lugha zingine ikiwemo kisukuma chenyewe au ulilenga kwa wale wanaozungumza kiswahili tu bila lugha nyingine, na kisukuma tu bila kiswahili? Ina maana wasukuma wengi hawajui kiswahili?
Na Abeid Poyo
MRADI wa Lugha za Tanzania (LoT) umezindua atlasi ya lugha na kuitaja lugha ya Kisukuma kuwa na wazungumzaji wengi nchini.
Katika uzinduzi huo uliofanyika jana katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, lugha ya Kisukuma ilitangazwa kuwa na wazungumzaji wapatao 5, 195, 504 ikifutiwa kwa mbali na lugha ya Kiswahili yenye wazungumzaji 2,379,294
Akizungumza katika hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa lugha kutoka ndani na nje ya nchi, Mratibu wa mradi huo, Prof Josephat Rugemalira alisema atlasi hiyo ya aina yake inatoa picha halisi ya idadi ya lugha zilizopo nchini, wazungumzaji, maandiko, usambaaji wake na maelewano ya karibu ya lugha.
Atlasi ya lugha za Tanzania ni kiungo muhimu katika mkakati wa wa kuzitambua na kuzitathmini rasilimali zetu za utamaduni, alisema Prof Rugemalira na kuongeza kuwa, uzinduzi wa atlasi hiyo unatoa picha halisi ya maendeleo ya sekta ya lugha nchini.
Kwa mujibu wa Rugemalira, atlasi hiyo ni matokeo ya utafiti wa miaka kadhaa wa mradi huo ulio chini ya Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Jamii ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Alibainisha kuwa utafiti huo pia ulibaini kuwepo kwa lugha 150 hapa nchini huku baadhi yake, kama vile lugha za Wanda, Kiga, Kikuyu na Bwali zikiwa hatarini kufa kwa kukosa matumizi.
Alifahamisha kuwa lugha hizo zimekumbwa na hali hiyo kutukana na mambo mbambali ikiwemo lugha hizo kumezwa na lugha kuu.
Katika hafla hiyo, machapisho 20 zikiwemo kamusi 18 za lugha za asili zilizinduliwa na Balozi wa Sweden nchini Staffan Herrstrom aliyekuwa mgeni. Hafla hiyo ilikwenda sambamba na maadhimisho ya Siku ya Lugha Mama duniani.
Source: Gazeti la Mwananchi
Wazo langu:
Utafiti huu bila shaka haukuangalia overlap ya hizi lugha, kama kuna watu wanaozungumza kiswahili na lugha zingine ikiwemo kisukuma chenyewe au ulilenga kwa wale wanaozungumza kiswahili tu bila lugha nyingine, na kisukuma tu bila kiswahili? Ina maana wasukuma wengi hawajui kiswahili?