Nemesis
JF-Expert Member
- Feb 13, 2008
- 5,462
- 4,364
:A S-confused1:
Inasikitisha, inapotokea mamlaka zinashindwa kuthibiti wezi, wahuni na wahujumu uchumu na kuwaongezea gharama wananchi. EWURA inapendekeza Serikali iongeze kodi ya mafuta ya taa toka sh 53 kwa lita hadi 490 kwa lita ili bei yake ilingane na petrol na dizeli.
Petrol na dizeli zinatumika kuendeshea mitambo, magari na vitu vingine vinavyoingiza fedha nyingi tena vinavyotumiwa na watu wenye pesa (matajiri). Mafuta ya taa yanatumiwa zaidi majumbani tena na watu maskini au kipato cha chini. Watu wengi hawana umeme manyumbani iwe kwa kukosa uwezo au TANESCO hawajafikisha huduma.
Uzalishaji unaofanywa na mtu anapotumia mafuta ya taa nyumbani ni hakuna au mdogo haiwezekani ukalipa gharama ya kulingana na petrol au dizeli. Iweje EWURA wanatoa pendekezo hili? kama wameshindwa kazi si waondoke?
EWURA yaunga mkono bei ya mafuta ya taa kuwa kama dizeli, petrol
na Janet Josiah
MAMLAKA ya Udhibiti wa Matumizi ya Nishati na Maji (EWURA), imeunga mkono, mapendekezo ya baadhi ya wadau kutaka kupandishwa kodi mafuta ya taa kuwa sawa na ya diseli na petroli. Akizungumza na Tanzania Daima, Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo, Haruna Masebu, alisema endapo kodi hizo zitakuwa sawa na zingine hatua hiyo itakuwa suluhisho kuondoa tatizo la uchachushaji mafuta.
Mapendekezo ya EWURA na wadau wengine, yamekuja siku chache baada ya tukio la magari matano ya Rais Jakaya Kikwete kujazwa mafuta machafu na kugoma kuwaka wakati akiwa ziarani mkoani Kilimanjaro.
Masebu alisema ingawa bajeti ya mwaka wa fedha ya 2010/2011, haikuzungumzia suala la mafuta ya taa kupandishwa kodi kutokana na nishati hiyo kutumiwa na watu wa hali ya chini, alisema tatizo hilo halitaweza kuisha kwa kuwa ndilo linalowapa faida wafanyabishara wa mafuta.
Alisema wafanyabishara wamekuwa wakipata faida kubwa katika mafuta wanayoyauza baada ya kuyachakachua kutokana na mafuta ya taa kutozwa kodi ya shilingi 53 kwa lita na dizeli na petroli kutozwa shilingi 490 kwa lita pindi wanapoyaingiza.
Masebu alisema baada ya kufanya zoezi la kuyachakachua na kuanza kuyauza hupata faida ya shilingi 450, hali ambayo alisema endapo serikali haitachukua hatua za kuyapandishia kodi, hali hiyo itaendelea kama ilivyo. Alisema wao kama EWURA hawana uwezo wa kupandisha nishati hiyo kodi bali uwezo huo upo katika Wizara ya Fedha na Uchumi.
Masebu alisema kwa kuwa tatizo hilo ni kubwa na kwamba haliwezi kuisha mara moja kama nishati hiyo haitapandishiwa kodi, EWURA imejipanga kutumia njia za aina mbili ili kupunguza tatizo hilo mojawapo ikiwamo ya kuyawekea mafuta ya taa rangi ambayo itayatofautisha na mafuta ya dizeli na petroli hata kama yatachachuliwa yatagungulika mara moja.
Alisema njia nyingine ambayo EWURA itatumia kukabiliana na tatizo hilo, tayari imeagiza magari maalum yenye maabara Mobile Laboratory yatayoingia mwezi Agosti, ambayo yatazunguka nchi nzima kukagua na kuwachukulia hatua wafanyabiasha watakaokuwa wamefanya hivyo.
Alipoulizwa endapo nishati hiyo itapanda, haoni kama itawaumiza watu wa hali ya chini, alijibu kwamba kama serikali ikifikia muafaka wa kupadisha kodi, wananchi wa hali ya chini watatafutiwa nishati mbadala ya mafuta ya taa ili kukidhi mahitaji yao kama ilivyo katika nchi nyingine.
Wakati huo huo, Masebu alisema kuwa tayari mamlaka hiyo imeshakamilisha ripoti ya uchunguzi wa kituo cha mafuta cha mjini Moshi ambacho kiliyaweka mafuta machafu kwenye magari matano yaliyokuwa katika msafara wa Rais Kikwete.
Alisema kinachosubiwa sasa ni maelezo ya mmiliki wa kituo hicho ili ripoti hiyo itolewe mbele ya vyombo vya habari kesho kutwa (Ijumaa).
Source EWURA yaunga mkono bei ya mafuta ya taa kuwa kama dizeli, petrol
Inasikitisha, inapotokea mamlaka zinashindwa kuthibiti wezi, wahuni na wahujumu uchumu na kuwaongezea gharama wananchi. EWURA inapendekeza Serikali iongeze kodi ya mafuta ya taa toka sh 53 kwa lita hadi 490 kwa lita ili bei yake ilingane na petrol na dizeli.
Petrol na dizeli zinatumika kuendeshea mitambo, magari na vitu vingine vinavyoingiza fedha nyingi tena vinavyotumiwa na watu wenye pesa (matajiri). Mafuta ya taa yanatumiwa zaidi majumbani tena na watu maskini au kipato cha chini. Watu wengi hawana umeme manyumbani iwe kwa kukosa uwezo au TANESCO hawajafikisha huduma.
Uzalishaji unaofanywa na mtu anapotumia mafuta ya taa nyumbani ni hakuna au mdogo haiwezekani ukalipa gharama ya kulingana na petrol au dizeli. Iweje EWURA wanatoa pendekezo hili? kama wameshindwa kazi si waondoke?
EWURA yaunga mkono bei ya mafuta ya taa kuwa kama dizeli, petrol
na Janet Josiah
MAMLAKA ya Udhibiti wa Matumizi ya Nishati na Maji (EWURA), imeunga mkono, mapendekezo ya baadhi ya wadau kutaka kupandishwa kodi mafuta ya taa kuwa sawa na ya diseli na petroli. Akizungumza na Tanzania Daima, Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo, Haruna Masebu, alisema endapo kodi hizo zitakuwa sawa na zingine hatua hiyo itakuwa suluhisho kuondoa tatizo la uchachushaji mafuta.
Mapendekezo ya EWURA na wadau wengine, yamekuja siku chache baada ya tukio la magari matano ya Rais Jakaya Kikwete kujazwa mafuta machafu na kugoma kuwaka wakati akiwa ziarani mkoani Kilimanjaro.
Masebu alisema ingawa bajeti ya mwaka wa fedha ya 2010/2011, haikuzungumzia suala la mafuta ya taa kupandishwa kodi kutokana na nishati hiyo kutumiwa na watu wa hali ya chini, alisema tatizo hilo halitaweza kuisha kwa kuwa ndilo linalowapa faida wafanyabishara wa mafuta.
Alisema wafanyabishara wamekuwa wakipata faida kubwa katika mafuta wanayoyauza baada ya kuyachakachua kutokana na mafuta ya taa kutozwa kodi ya shilingi 53 kwa lita na dizeli na petroli kutozwa shilingi 490 kwa lita pindi wanapoyaingiza.
Masebu alisema baada ya kufanya zoezi la kuyachakachua na kuanza kuyauza hupata faida ya shilingi 450, hali ambayo alisema endapo serikali haitachukua hatua za kuyapandishia kodi, hali hiyo itaendelea kama ilivyo. Alisema wao kama EWURA hawana uwezo wa kupandisha nishati hiyo kodi bali uwezo huo upo katika Wizara ya Fedha na Uchumi.
Masebu alisema kwa kuwa tatizo hilo ni kubwa na kwamba haliwezi kuisha mara moja kama nishati hiyo haitapandishiwa kodi, EWURA imejipanga kutumia njia za aina mbili ili kupunguza tatizo hilo mojawapo ikiwamo ya kuyawekea mafuta ya taa rangi ambayo itayatofautisha na mafuta ya dizeli na petroli hata kama yatachachuliwa yatagungulika mara moja.
Alisema njia nyingine ambayo EWURA itatumia kukabiliana na tatizo hilo, tayari imeagiza magari maalum yenye maabara Mobile Laboratory yatayoingia mwezi Agosti, ambayo yatazunguka nchi nzima kukagua na kuwachukulia hatua wafanyabiasha watakaokuwa wamefanya hivyo.
Alipoulizwa endapo nishati hiyo itapanda, haoni kama itawaumiza watu wa hali ya chini, alijibu kwamba kama serikali ikifikia muafaka wa kupadisha kodi, wananchi wa hali ya chini watatafutiwa nishati mbadala ya mafuta ya taa ili kukidhi mahitaji yao kama ilivyo katika nchi nyingine.
Wakati huo huo, Masebu alisema kuwa tayari mamlaka hiyo imeshakamilisha ripoti ya uchunguzi wa kituo cha mafuta cha mjini Moshi ambacho kiliyaweka mafuta machafu kwenye magari matano yaliyokuwa katika msafara wa Rais Kikwete.
Alisema kinachosubiwa sasa ni maelezo ya mmiliki wa kituo hicho ili ripoti hiyo itolewe mbele ya vyombo vya habari kesho kutwa (Ijumaa).
Source EWURA yaunga mkono bei ya mafuta ya taa kuwa kama dizeli, petrol