Anselm
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 1,710
- 291
Wengi wamekuwa wakiamini uwekezaji ulio' na unaoendelea kufanywa na mmiliki wa Club ya mpira wa miguu ya Azam ni njia mojawapo itakayoligeuza soka la Tanzania kutoka kwenye u'kichwa cha mwendawazimu kwenda kwenye level nyingine, kitendo chao cha kumchapa Mnyama jana goli 3-1 kinaonekana kukoleza dhana hiyo na kuamini kuwa enzi za Tanzania kuchukulia mpira ni Simba na Yanga ndo zinaishilia taratibu kama siyo zimemalizika kabisa.
Ni kweli wamiliki wake wamewekeza sana katika team hiyo,wamesajili vizuri,wana walimu wazuri,madaktari wazuri,uwanja mzuri,Hostel nzuri vifaa vya team (mabasi na vifaa vingine vya mechi na mazoezi) vizuri tuseme almost wana kila kitu kizuri, lkn je uwepo wa team hii yenye kila kitu kizuri katika ardhi ya Tanzania kunaweza kuwa na mchango wowote chanya kwenye maendeleo ya hili soka la nchi yetu?
Hapa nitaongelea jambo 1 tu...
Issue ya Mrisho Khalfani Ngassa, habari nilizozipata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika kabisa ni kuwa Mchezaji huyu sasa hivi yuko kwenye mgomo usio rasmi unaotaka kufanana na ule wa madaktari wa hii Republic yetu, akishinikiza aruhusiwe kurejea kwenye Chama lake lililomuweka katika ramani ya juu katika usakataji wa kabumbu hapa nchini,lakini Viongozi wa Club hiyo wamemgomea na wamesema watamshikilia mpaka atakapomaliza mkataba wake.Licha ya team ya Yanga kujaribu mara kadhaa kuongea na viongozi wa Azam kuhusu kumnunua mchezaji huyo kwa njia tofautitofauti kama Cash kwa dau watakalolitaja Azam wenyewe au Cash plus mchezaji bado Viongozi wa team hii wamezikataa offer hizo pamoja na kujaza wachezaji wengi wa ndani na nje ya nchi wenye uwezo kama au pengine zaidi ya Ngassa....je kitendo hiki cha hawa Viongozi wa Azam ambacho dhahiri kinataka kufanana na cha wale viongozi wa team Swahiba wao (cha kukomoana) hakirudishi nyuma maendeleo ya soka la nchi hii kweli?,leo hii Ngassa mchezaji anayeweza kuwa na mchango mkubwa tu kwa team yake ya Taifa anashindwa kutumika vizuri kwasababu ndogondogo ambazo zingeweza kufanyiwa kazi na kumfanya aifanye kazi yake(ambayo ni kucheza mpira) kwa ufanisi wa hali ya juu kwa maendelo yake binafsi,Club yake na team yake ya Taifa.
Nilistaajabu sana kuona Ngassa akipewa dk 13 tu katika mechi kati ya team yake ya Azam na Tusker huku jana nikimshuhudia akisugua benchi kwa dakika zote 90+5...sikubaliani na hili kabisa,hawa Mabwanyenye waache kuua kipaji cha Mshikaji wamuache aje apige soka Jangwani, Taifa bado linamuhitaji akina Msuva,Atupele na Christopher Edward kule Ngorongoro Herois bado wanahitaji kujifunza vitu kutoka kwake.
Ni kweli wamiliki wake wamewekeza sana katika team hiyo,wamesajili vizuri,wana walimu wazuri,madaktari wazuri,uwanja mzuri,Hostel nzuri vifaa vya team (mabasi na vifaa vingine vya mechi na mazoezi) vizuri tuseme almost wana kila kitu kizuri, lkn je uwepo wa team hii yenye kila kitu kizuri katika ardhi ya Tanzania kunaweza kuwa na mchango wowote chanya kwenye maendeleo ya hili soka la nchi yetu?
Hapa nitaongelea jambo 1 tu...
Issue ya Mrisho Khalfani Ngassa, habari nilizozipata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika kabisa ni kuwa Mchezaji huyu sasa hivi yuko kwenye mgomo usio rasmi unaotaka kufanana na ule wa madaktari wa hii Republic yetu, akishinikiza aruhusiwe kurejea kwenye Chama lake lililomuweka katika ramani ya juu katika usakataji wa kabumbu hapa nchini,lakini Viongozi wa Club hiyo wamemgomea na wamesema watamshikilia mpaka atakapomaliza mkataba wake.Licha ya team ya Yanga kujaribu mara kadhaa kuongea na viongozi wa Azam kuhusu kumnunua mchezaji huyo kwa njia tofautitofauti kama Cash kwa dau watakalolitaja Azam wenyewe au Cash plus mchezaji bado Viongozi wa team hii wamezikataa offer hizo pamoja na kujaza wachezaji wengi wa ndani na nje ya nchi wenye uwezo kama au pengine zaidi ya Ngassa....je kitendo hiki cha hawa Viongozi wa Azam ambacho dhahiri kinataka kufanana na cha wale viongozi wa team Swahiba wao (cha kukomoana) hakirudishi nyuma maendeleo ya soka la nchi hii kweli?,leo hii Ngassa mchezaji anayeweza kuwa na mchango mkubwa tu kwa team yake ya Taifa anashindwa kutumika vizuri kwasababu ndogondogo ambazo zingeweza kufanyiwa kazi na kumfanya aifanye kazi yake(ambayo ni kucheza mpira) kwa ufanisi wa hali ya juu kwa maendelo yake binafsi,Club yake na team yake ya Taifa.
Nilistaajabu sana kuona Ngassa akipewa dk 13 tu katika mechi kati ya team yake ya Azam na Tusker huku jana nikimshuhudia akisugua benchi kwa dakika zote 90+5...sikubaliani na hili kabisa,hawa Mabwanyenye waache kuua kipaji cha Mshikaji wamuache aje apige soka Jangwani, Taifa bado linamuhitaji akina Msuva,Atupele na Christopher Edward kule Ngorongoro Herois bado wanahitaji kujifunza vitu kutoka kwake.