Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 67,976
- 95,295
Heshima zenu waungwana.....Ilikuwa wikiendi hatari kabisa (ongeeni na TBL wafunge kiwanda kwa afya yangu LOL)
Ni hivi:
Bibi yenu amesafiri. Kilichoniacha hoi, eti ameondoka na shati langu ambalo halijafuliwa. Namuuliza kulikoni ananiambia anapokuwa mbali nami anapenda anuse shati langu ili aipate harufu yangu nafsi yake itulie. Anaipenda eti.
Hivi wanungwana, hii inaweza kuwa kweli au bibi yenu anataka kuniloga?...Kuna wengine ishawatokea hii? Eti nyie wa jinsia ya kike, huwa mnafanyaga hivyo?....Kama vipi jamani niwahi kwa Kakobe na Mama Rwakatare waniwekee kinga.
Babu anarudi kitandani kutafakari kwa kina.
Na harufu yangu.
Ni hivi:
Bibi yenu amesafiri. Kilichoniacha hoi, eti ameondoka na shati langu ambalo halijafuliwa. Namuuliza kulikoni ananiambia anapokuwa mbali nami anapenda anuse shati langu ili aipate harufu yangu nafsi yake itulie. Anaipenda eti.
Hivi wanungwana, hii inaweza kuwa kweli au bibi yenu anataka kuniloga?...Kuna wengine ishawatokea hii? Eti nyie wa jinsia ya kike, huwa mnafanyaga hivyo?....Kama vipi jamani niwahi kwa Kakobe na Mama Rwakatare waniwekee kinga.
Babu anarudi kitandani kutafakari kwa kina.
Na harufu yangu.