Esther Bulaya VS Esther Wassira

Nani utampa kura yako ubunge Bunda kati ya Steven Wasira (CCM) na Esther Wasira (Chadema) ?


  • Total voters
    112
Status
Not open for further replies.
Naomba thread isomeke CDM Vs CCM nani zaidi, maana hapa ishabiki wa kochama hautaleta ukweli maana, huyo Wasira ameonekana jana tu tayari amemzidi mtu ambaye yupo ktk siasa kwa zaidi yake.
Mpishi bora ni yule anayepika chakula vizuri na wala sio uzoefu wa kukaa jikoni miaka mingi.
 
Kwa kuweka kumbukumbu sahihi, Coca cola kwa huku afrika mashariki waliendeshaga shindano linaloitwa "COCACOLA POP STAR"
na washindi wake kwa Tz walikuwa "WAKILISHA" ambalo ni kundi lilohusisha Langa, Sarah na Witness.
Ile Pop Idol ya mwaka 2003 ndiyo ilimng'arisha Esther Wasira (ambaye ndiye huyu anayejadiliwa hapa kwa upande mmoja), Terrence na Banana haikuhusika na Coca Cola.
Ni hayo tu Mkuu wangu.
Shukriyah........... Lol!


Shukrani sana mkuu wangu kwa masahihisho! Naomba kwenye Hansard za JF isomeke na marekebisho yake.
 
Wassira Ester kitu ingine kabisa mimi nilikuwa simfahamu jana nikawasha itv kusikiliza kongamano la kumkumbuka Kambarage, asalaaale binti nouma sijawahi kuona nilikuwa na kikao cha harusi nikaomba udhuru
Umeona eeeeh!!
Kuna taarifa zinadai huyu Esther Wassira ndiye aliyethibitisha kuwa ITV ni Television ya taifa, kwani wakati anaongea kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Nyerere, Rais JK naye alikuwa live TBC katika maadhimisho kama hayo, lakini watu wengi walikuwa wanaangalia ITV kumsikiliza Esther Wassira badala ya kumsikiliza mkuu wa nchi!!!
 
Huyu binti namkumbuka akiwa loyola 2003,alikuwa anashindana kwenye mashindano ya muziki ya pop idol,alikuwa mmoja wa waimbaji mahili na nakumbuka alitinga mpaka top 3.
 
Nina uhakika huyu binti jana atakuwa kawa-inspire vijana wengi sana, na sasa tutaanza kuwaona wengi tu wazalendo wakijitokeza kujiunga katika harakati hizi tuzionazo sasa za kudai mabadiliko ya kimifumo. Atakuwa amefanikiwa kuwatoa uoga na kutojali vijana wengi sana! Aliongea vizuri sana, infact bila yeye kuwepo kama mchokoza mada nadhani mdahalo wa jana ungedorora. Hata Kitila alionyesha kumkubali mara tu alipomaliza dakika zake 25 pale aliposema kuwa yale madai ya watu kuwa waongeaji wakuu hawatakuwa na uwezo wa kutoa hoja zenye mashiko, jibu lao lilitolewa na Esther. Hongera sana binti!
 
Umeona eeeeh!!
Kuna taarifa zinadai huyu Esther Wassira ndiye aliyethibitisha kuwa ITV ni Television ya taifa, kwani wakati anaongea kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Nyerere, Rais JK naye alikuwa live TBC katika maadhimisho kama hayo, lakini watu wengi walikuwa wanaangalia ITV kumsikiliza Esther Wassira badala ya kumsikiliza mkuu wa nchi!!!
Jk unasikia:-? Kama Ester tu anakufunika, je Dr wa ukweli..
 
'E wasira is all talent, while E.Bulaya is the product of much training
 
Unajaribu kushindanisha mlima na kichuguu!!!!wa CDM ni mlima wa CCM ni kichuguu...!!
Naomba kujuzwa kuna binti wassira mmoja aliwahi kuimba wimbo wa Sheilaa akiwa secondari, hivi ndo huyu Esther.?
 
Unajaribu kushindanisha mlima na kichuguu!!!!wa CDM ni mlima wa CCM ni kichuguu...!!
Naomba kujuzwa kuna binti wassira mmoja aliwahi kuimba wimbo wa Sheilaa akiwa secondari, hivi ndo huyu Esther.?
unasema kweli mkuu
 
Huyu binti namkumbuka akiwa loyola 2003,alikuwa anashindana kwenye mashindano ya muziki ya pop idol,alikuwa mmoja wa waimbaji mahili na nakumbuka alitinga mpaka top 3.

kumbuka rekodi yake iliyomtoa 'SHEILA'
 
*Esther Bulaya ni mbunge wa kike, kijana kwa tiketi ya CCM viti maalum, watu wengi wamepata kumzungumzia uwezo wake wa kisiasa humu JF mara kadhaa. Ameonekana Bungeni na mara kadhaa kwenye majukwaa ya kisiasa akijenga hoja.

*Esther Wassira alionekana kwa mara ya kwanza kwenye ulingo wa kisiasa siku akichukua kadi ya CHADEMA, watu wengi walitaka kumfahamu uwezo wake wa kisiasa(kujenga hoja na kuamsha ushawishi), na kupitia hotuba aliyoitoa kwenye kongamano la kumbukumbu ya mwalimu Nyerere pale Nkurumah kila mtu sasa anaweza kumzungumzia.

*Sababu za kutaka kuwalinganisha kisiasa.
1/Mfanano wao (Wote ni wanasiasa, vijana, wanawake, wanatoka Bunda, wameshawahi kuwa na mzozo wa kisiasa na Steven Wassira, wote wanaitwa Esther!!)

2/Wanatoka vyama viwili vinavyopinzana.

3/Watu wengi wanataka kuona mmoja wao akirithi kiti cha ubunge wa Steven Wassira kule Bunda 2015.

***Wadau wa JF mnaweza kuchangia kwa kujenga hoja za ulinganifu wao kisiasa.

Kwangu mimi naona ni mapema mno kuwalinganisha kwa sasa ukizingatia kuwa E. Wasira ndio kwanza ameanza kuchomoza. Tuvute muda kidogo.
 
baada ya Esther Wassira kuwatoa woga vijana wengi jana,
Tumtegeme hata Ridhiwani akija na mikakati yake sasa,
yaani nae huwenda amekuwa inspired sana.
Mia
 
E.wasira zaidi.huyo bulaya hamna kitu,yeye aendelee kuandaa mashindano ya vikombe vya mbuzi hulo bunda(strategy za kizamani za kuteka watu ili wakuchague)E.Wassira 2015 anaenda kuchukua jimbo kiulani tu.wenyewe jumapili mliona mauwezo yake pale Nkuruma Hall
 
Esther wassira ndiye haswaaa anastahili. Esther Bulaya gari lake bovu spanner mkononi hawezi kufikisha malengo.
 
Esther Wasira Akienda huko bungeni na akagoma kusign posho ya vikao vya bunge nitamuamini,vinginevyo ni yaleyale kugeuzana Mazombi!
 
Esther Wasira Akienda huko bungeni na akagoma kusign posho ya vikao vya bunge nitamuamini,vinginevyo ni yaleyale kugeuzana Mazombi!
Anaonekana ni mzalendo na mwanamapinduzi. Ametoka kwenye familia ambayo angeweza kupewa kazi nzuri tena ukizingatia ana ubongo lakini ameacha yote kwa ajili ya umma. nimependa aliposema, yanifaa nini kutumikia familia ya watu 5 wakati naweza kutumikia watanzania milioni hamsini?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom