Mbunge wa viti maalum CCM, amesema bungeni kuwa Polisi mkoa Mara wanahusika na kumuuwa kijana Chacha ambaye anatuhumiwa kwa wizi wa kuku.
Hujamaliza story, mwenyekiti/spika hajamtaka athibitishe?
shukrani zimwendee Mh.Naibu Spika kwa kumwokoa waziri Nchimbi, kwa kumtaka muuliza swali alete vielelezo.
My observation: majibu kama haya yanatokana na kesi ya mbuzi kumpa fisi ahukumu, sifahamu huo uchunguzi wa hayo mauwaji yalifanywa na nani?Polisi wenyewe au nani? ni matarajio yangu uchunguzi wa Sooo ya Dr.Ulimboka yatakuwa yaleyale na sawa sawa na Mh.Mwakyembe na ajali yake ya gari.
Naipenda sana Tanzania na watu wake
Nakubaliana na maneno ya Dr Mwakyembe aliyowahi kusema huko nyuma kwamba Tanzania inaweza kuwa nchi pekee duniani ambapo mtu anaporeport tatizo polisi mtu huyo anatakiwa atoe ushahidi badala ya police kuchunguza.
Waziri wa mambo ya Ndani kama hana taarifa sahihi kuhusu mauaji ya huyu kijana alitakiwa aombe radhi kwa familia ya marehemu na taifa kwa jumla. Kitendo cha kusimama ndani ya bunge na kutoa taarifa za jumla jumla tena zisizokuwa na ukweli ni kutokumtendea haki marehemu na familia yake. Hili ndicho watu wanaweza kuita 'double victimization'.
Mkuu FJM: ni vigumu sana kwa waziri kujifunga kengere, na hasa kwenye system ambayo imekaa ikiwa na majibu yake yakiwa tayari kwa kila tatizo - na ambayo yapo kwa ajili ya kujivua lawama na yasiyo leta suluhu...
Unajuwa kama tungekuwa na ungozi mzuri wa vikao vya bunge, kiti cha spika kingekuwa kinaingilia kati pale serikali inatoa majibu ya kubababisha. Hapa mwakilishi wa wananchi anatoa malalamiko waziri wa mambo ya ndani anajibu kwa ujanja ujanaj, lakini naibu speaker anarusha mpira kwa mwakilishi wa wananchi na sio serikali iliyokuja bungeni na majibu mepesi.
Naomba nikusahihishe kidogo mkuu,alikuwa ni Ester Matiko,na mwizi wa kuku ni kijana James Machota.Nimeshangashwa sana na majibu ya waziri,nadhani hawa mawaziri huwa wanakaa ofisini na kutunga taarifa.Huyo marehemu James Machota nilihudhuria msiba wake,mtu yeyote akifika Mugumu ataambiwa ni nini kilifanywa na polisi na inspector Temu aliyehusika na mauaji alihamishwa.Kwa kweli nimeamini hawa viongozi wetu ni dhaifu sana.Mh.Ester anaposema anao ushahidi ana uhakika.Nchimbi amechemsha sana.
Huyu Nchimbi angejiuzuru kazi inamshinda. usalama wa raia uko matatani
halafu akisha peleke, wata mfanyanini waziri alie lidanganya bunge na wananchi kwa ujumla au nikama issue ya Lema...kama kawaida ndani ya siku saba.
halafu akisha peleke, wata mfanyanini waziri alie lidanganya bunge na wananchi kwa ujumla au nikama issue ya Lema...
Yani mkuu majibu ya waziri yamenishangaza kweli.Hapo kwenye nyekundu uko sahihi kabisa,kwa sababu wenye dhamana ya kulinda usalama wetu, ndo wa kwanza kuhatarisha
Inatisha sana, na inahuzunisha mno. Hao ambao tunatakiwa tukawaarifu kuhusu uharifu ndio wanatuhumiwa kila kukicha juu ya waharifu 100%.
Raia watakimbilia wapi?
Agree with you mkuu, nilichangaya sana.Naomba nikusahihishe kidogo mkuu,alikuwa ni Ester Matiko,na mwizi wa kuku ni kijana James Machota.Nimeshangashwa sana na majibu ya waziri,nadhani hawa mawaziri huwa wanakaa ofisini na kutunga taarifa.Huyo marehemu James Machota nilihudhuria msiba wake,mtu yeyote akifika Mugumu ataambiwa ni nini kilifanywa na polisi na inspector Temu aliyehusika na mauaji alihamishwa.Kwa kweli nimeamini hawa viongozi wetu ni dhaifu sana.Mh.Ester anaposema anao ushahidi ana uhakika.Nchimbi amechemsha sana.