Pole YoYo....hiyo si dawa ya figo per se. Kwa kawaida mafigo hutoa kichocheo hicho cha erythropoietin ambacho kazi yake ni kustimulate bone marrow itengeneze chembe chembe nyekundu za damu (red blood cells). Mafigo yanapokuwa magonjwa yanashindwa kutoa erythropoitin na hivyo mgonjwa kupata upungufu mkubwa wa damu (severe anaemia). Sasa hiyo erythropoietin haitibu figo, ila inaenda kufanya kazi ya kustimulate bone marrow kuzalisha red blood cells figo zinaposhindwa kufanya hivyo.
Mara ya mwisho niliona mgonjwa akihitaji hiyo mwaka 2007, na tuliagiza toka Nairobi. Nilidhani mpaka sasa itakuwepo, ni aibu kama bado hatuna. Tafadhali check kwanza na maduka makubwa ya dawa mfano JD Pharmacy, Okinawa Pharmacy, Philips...kabla huaagiza Nairobi.
Hello... hiyo ni dawa ya kumsaidia mtu mwenye renal failure wakati anafanyiwa dialysis... erthropoietin katika mwili inahusika katika formation of red blood cells... Nenda OKINAWA PHARMACY .. Ipo Jirani Jirani na Askari Monument..au Salama Pharmacy Kariakoo... au Dawa Pharmacy Benjamini Mkapa Pension Tower.... JD Pharmacy Mlimani City au JD Pharmacy jirani na round about ya Askari Monument
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.