Erring on the Side of Caution: Kikwete usiwaapishe mawaziri wasioapishwa kuwa wabunge kwanza!

Hivi inakuwaje mwanasheria mkuu anashindwa kuona makosa ya waziwazi kama haya? Na kama haoni hili anawezaje kusimamia mikataba ya kibepari kama Barrick na Uranium guys toka Marekani? Kama hao mawaziri wataapishwa kesho ni wazi wakubwa watakuwa wamedharau katiba! Hilo halina ubishi. Na watu wataanza ku-question dhamira ya serikali kwa wananchi wake. Nchi haiwezi kuongozwa na watu ambao hawajala kiapo! Hilo halipo sehemu yoyote duniani. Hakuna! Pili, kuna kitu kingine office ya mwanasheria mkuu ajiridhishe. Nacho ni uraia wa wabunge wote wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania wakiwemo mawaziri na naibu mawaziri. Narudia, office ya mwanasheria mkuu ihakiki na kujiridhisha uraia wa wabunge wote wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja wakiwemo mawaziri na naibu mawaziri.

Makosa ya waziwazi yako wapi? Unaweza kuyataja tuyajadili?

Umesoma ibara ya 68 ya katiba? Unaelewa mtu anaanza kuwa mbunge wakati gani? unaelewa kuna wabunge wa aina ngapi?

Frankly mimi mtu akiniambia mtu kama Mizengo Pinda au January Makamba hastahili kuingia bungeni na hivyo kuwa katika cabinet nitaona ana argument nzuri zaidi ya hizi fringe fanaticism claims ambazo hazina msingi wa kikatiba.

Kama hizi ndizo opposition anazopata Kikwete mtawapa watu msemo kwamba mnamuandama Kikwete kwa kila afanyacho bila kujali ukweli.


Mie si mtu wa kumtetea Kikwete kwa kawaida lakini katika hili hayuko nje ya katiba wala sheria. labda mseme katiba / sheria inayofanya kuwepo na perception ya "oath of office" katika "oath of allegiance" si nzuri.

Watu wengi wanashindwa kutofautisha, wanafikiri kwamba kile kiapo cha Spika ni "oath of office" wakati ni "oath of allegiance"
 
Sawa,

Hakuna anayesema hawa wabunge walioteuliwa na rais wanataka kufanya zaidi (mambo ya ubunge) kabla ya kuapishwa na Spika.

Swala hapa, wao ni wabunge kabla ya kuapishwa ama la?

Ibara ya 68 inatuambia ni wabunge.

Hivyo Kikwete anapowaapisha kuwa mawaziri washakuwa wabunge tayari. Kikwete mwenyewe aliapishwa hivyo hivyo kwa mujibu wa mdau mmoja hapa. Kitu ambacho kinasadikika kwa sababu Kikwete first time alivyoingia bungeni alikuwa mbunge wa kuteuliwa na rais na akaingia unaibu waziri moja kwa moja.

Inawezekana hilo la JK ni kweli lakini labda kwa sababu hawakuwepo watu walioweza kuona hili tunaloliona sasa.. kwa sababu kama ni kweli kwanini Rais anasubiri wabunge waapishwe ndio ampate waziri mkuu na mawaziri wengine baada ya uchaguzi badala ya kuwatangaza kabla hawajaapishwa na wakati tayari ni wabunge wateule?

Kwamba ni wabunge ni wabunge kwa maana ya kwamba wamechaguliwa wawakilishi lakini si kwa maana ya kwamba wanafurahia haki na madaraka yao ya kibunge. Vinginevyo, kama tayari ni wabunge kamili kiapo cha nini basi? Kama kiapo hakiongezi lolote kwenye ubunge wao au kukamilisha process ya wao kuwa wabunge kwanini ni muhimu?
 
Sawa,

Hakuna anayesema hawa wabunge walioteuliwa na rais wanataka kufanya zaidi (mambo ya ubunge) kabla ya kuapishwa na Spika.

Swala hapa, wao ni wabunge kabla ya kuapishwa ama la?

Ibara ya 68 inatuambia ni wabunge.
.

NEC ikishamtangaza mshindi wa kiti cha urais, mtajawa anakuwa rais au la? Na kesho yake akiamka anaanza kufanya kazi za rais au la?
 
Kosa kubwa ambablo binafsi naamini ni mahakama inastahili kuamua ni phrase ya "shughuli za kibunge". Watu wengi wanatafsiri kama "shughuli bungeni".Shughuli za kibunge na 'shughuli bungeni' ni vitu viwili tofauti. Shughuli za kidaktari na shughuli hsopitali si kitu kimoja.

Kwa mfano, mtu aliyesomea uwakili akapasi hadi mtihani anaweza kuwa na sifa zote za kufanya kazi za uwakili. Lakini ili aweze kujitambulisha kuwa ni wakili ni lazimaale kiapo cha kazi hiyo. Hata daktari ni hivyo hivyo, anaweza akawa amehitimu masomo yote na kufanya vizuri lakini ili aweze kuingia katika udaktari ni lazima aape kwanza. Sasa udaktari siyo kutibu tu au kugawa dawa tu; ni mjumuisho wa mambo mengi yanayohusiana nahilo.

Watuwengi na hata Werema mmojawapo wanapozungumzia shughuli za "kibunge" wanaifunga hii kumaanisha ni yale ambayo mbunge anayafanya bungeni tu na yanayohusiana na mambo ya bunge tu. Naamini tafsiri hii si sahihi. Tafsiri sahihi ina maana ya mambo yote abmayo yanaweza kufanywa na mbunge ikiwemo kuwa waziri!

Kuwa waziri si shughuli, ni state.

Mbunge Ukishakuwa katika state ya uwaziri sasa, kuna shughuli za kiwaziri, shughuli za kibunge, shughuli za kimahakama.

Huyu waziri ambaye ni mbunge, kaapishwa uwaziri, lakini hajaapishwa uwaziri, anaweza kufanya shughuli za kiwaziri kwa sababu kashaapishwa uwaziri, hawezi kufanya shughuli za kibunge kwa sababu hajaapishwa "oath of allegiance" na Spika.

Usichanganye the state of being a minister - kitu ambacho si shughuli, na wala si shughuli ya kibunge- na shughuli za kibunge.
 
Sijaona utata uko wapi bado. Mbunge mteule ni nani na mbunge ni nani?

Hakuna kitu kama "mbunge mteule" kwa sababu, kwa wabunge wa kuchaguliwa, kabla ya kutangazwa kuwa mshindi na Tume ya uchaguzi, mtu anakuwa mgombea ubunge tu, akitangazwa kuwa mshindi hapo hapo anakuwa certified kuwa mbunge. Sasa hii concept ya "mbunge mteule" inatoka wapi? Au inajengeka kwa dhana ya kwamba mbunge akitangazwa na kuwa certified anakuwa si mbunge kamili, bali ni "mbunge mteule" mpaka aapishwe? Mbona katiba haisemai "wabunge wateule watamchagua Spika", inasema "wabunge" ?

Ditto kwa wabunge wanaoteuliwa na rais, rais akiwateua kashawa certify kuwa wabunge. Kiapo cha utiifu na uaminifu, kinahusika na utiifu na uaminifu na uwezo wa mbunge kufanya shughuli za kibunge zaidi ya kumchagua Spika.

Tumejadili hili sana katika post aliyoilink Mkuu Kimbunga hapo juu. Naona watu wanataka ku split atoms kama CERN tu sehemu ambayo hakuna argument. Ukiendekeza sana ku err on the side of caution utashindwa kwenda kazini.

Rais akiteua mtu kuwa mbunge, anam-certify huyo mtu kuwa mbunge. Kiapo cha ubunge hakihusiki kumfanya mtu kuwa mbunge, hili tumeshalijadili kirefu.Kiapo cha utiifu/uaminifu kwa Jamhuri kinahusika kwa mbunge kuweza kufanya shughuli za ubunge zaidi ya kumchagua Spika. Kiapo cha ubunge hakimfanyi mtu kuwa mbunge. Tushajadili sana hili na tumeona, kwa mfano wabunge wa kuchaguliwa wanakuwa certified kuwa wabunge wanapotangazwa washindi na Tume ya Uchaguzi, kwa hiyo wanakuwa wabunge kabla ya kiapo. Ndiyo maana ibara ya 68 imesema wabunge watamchagua Spika, haikusema "wabunge wateule". Na kama wabunge watamchagua Spika, halafu Spika atawaapisha wabunge, basi wabunge hawa wamekuwa wabunge kabla ya kuapishwa. Hapa ndipo ninaposema kiapo hakimfanyi mtu kuwa mbunge.

Kwa minajili hii basi, hata hao wabunge wa kuteuliwa na rais hawahitaji kiapo ili kuwa wabunge. Rais anapowateua anawa certify kuwa wabunge. Kwa hivyo basi, sasa hivi wanaweza kuapishwa kuwa mawaziri bila ya utata wowote. Wasichoweza kufanya ni shughuli za kibunge (kama wabunge) kwa sababu katiba inawataka wale kiapo kwanza.

Sioni utata.

Nyinyi ndio mnamwingiza chaka mkulu!!!!
tunakwambia it is unconstitutional for mp elect to assume mp's power before taking oath! "tutamuapisha, kama ni mkristo tutamuapisha kwa biblia, kama ni muislamu tutamuapisha kwa kuruani, kama hana dini tutatafuta namna ya kumuapisha, lakini laazima tutamuapisha" by Nyerere RIP

Kwa kukukumbusha umuhimu wa kiapo, rais Obama wa marekani alirudia kuapishwa baada ya kugundulika kuwepo makosa kwenye kiapo chake cha awali.

Nashauri katiba iheshimiwe, kwa kuwa jk aliapa si tu kuilinda katiba bali pia kuiheshimu, ASITUTIE MAJARIBUNI WATANZANIA, Asichelee kuruka majivu ya zitto akakanyaga moto wa TUNDU LISU ALIYEJERUHIWA NA KESI YA UBUNGE.
 
NEC ikishamtanga mshindi wa kiti cha urais, mtajawa anakuwa rais au la? Na kesho yake akiamka anaanza kufanya kazi za rais au la?

Hili nimeshali address kama mara nne hapo juu. Do not compare apples to oranges.

Mgombea ubunge akikosa mpinzani anapita bila kupigiwa kura kama alivyopita Mizengo Pinda au January Makamba, can you say the same for the presidency?

Unaona analogy yako inavyoanguka flat?
 
NEC ikishamtanga mshindi wa kiti cha urais, mtajawa anakuwa rais au la? Na kesho yake akiamka anaanza kufanya kazi za rais au la?

ili a assume power za urais lazima aape kwanza!!!
 
Nyinyi ndio mnamwingiza chaka mkulu!!!!
tunakwambia it is unconstitutional for mp elect to assume mp's power before taking oath! "tutamuapisha, kama ni mkristo tutamuapisha kwa biblia, kama ni muislamu tutamuapisha kwa kuruani, kama hana dini tutatafuta namna ya kumuapisha, lakini laazima tutamuapisha" by Nyerere RIP

Kwa kukukumbusha umuhimu wa kiapo, rais Obama wa marekani alirudia kuapishwa baada ya kugundulika kuwepo makosa kwenye kiapo chake cha awali.

Nashauri katiba iheshimiwe, kwa kuwa jk aliapa si tu kuilinda katiba bali pia kuiheshimu, ASITUTIE MAJARIBUNI WATANZANIA, Asichelee kuruka majivu ya zitto akakanyaga moto wa TUNDU LISU ALIYEJERUHIWA NA KESI YA UBUNGE.

1.Ukisema "unconstitutional" bora tupe na ibara tujadili, sio useme vitu kutoka kichwani mwako.
2. Ukichukua quote ya Nyerere kuhusu "oath of office" ya urais, ukaileta katika issue ya "oath of allegiance" ya ubunge unaonekana huelewi unachozungumzia na unaenda kijumlajumla bila uchambuzi makini. Labda ndiyo maana umeshindwa kuleta ibara hapo juu.
3. Unatuchamnganya zaidi kwa kuleta habari za Marekani, nchi tofauti, yenye katiba tofauti na historia tofauti katika mazungumzo ya Tanzania.

Get your story right first.
 
Hili nimeshali address kama mara nne hapo juu. Do not compare apples to oranges.

Mgombea ubunge akikosa mpinzani anapita bila kupigiwa kura kama alivyopita Mizengo Pinda au January Makamba, can you say the same for the presidency?

Unaona analogy yako inavyoanguka flat?

Unaongelea kinyang'anyiro cha kuugombea huo ubunge, kuthibitishwa ubunge kiapo ni lazima, kabla ya hapo ni kusherehekea ushindi au uteuzi!
 
Kama hakuna ushauri wangu ni kuwa Rais awaapishe wale ambao tayari ni wabunge lakini wale waliowapya wasubiri hadi Bunge liitishwe au (si lazima Dodoma hata Karimjee linaweza kukutana kama Spika ataamua hivyo) ili kuwaapisha hawa wabunge. WE HAVE TO RESPECT THE CONSTITUTION. Pamoja na ubovu wake wote; it is the only one we have.

sasa akiwaapisha tu wale ambao ni wabunge hawa wengine wasubiri lets say Rais ameteua Waziri na naibu wake na wote ni wapya ndio wameteuliwa kua wabunge...kwa hiyo wizara iendeshwe na katibu mkuu mpaka hapo bunge likae na kuwaapisha hao wabunge wapya...

Sijawahi sikia mbunge kateuliwa saa sita mchana alafu saa kumi jioni kawa waziri maana yake huyo waziri hata kazi za ubunge hazijui na hata bungeni hajawahi kufika na hawajui bunge likoje au limekaaje hao wengine hata dodoma hawajawahi kufika and yet sasa hivi ni mawaziri...IT CAN ONLY HAPPEN IN BONGO
 
Mimi sioni ulazima wa mawaziri kuwa wabunge. Wabunge waachwe kuwa wabunge na mawaziri waachwe wawe watendaji wa serikali.

Haya mambo ya mawaziri kuwa lazima wawe wabunge ni upumbavu tu. Hivi kuna hata anayejua sababu ya ulazima huo ni nini?

Kwani mawaziri wasipokuwa wabunge watashindwa kufanya kazi zao?

Dawa hapa ni ndogo sana - ondoa ulazima wa mawaziri kuwa wabunge.
 
Unaongelea kinyang'anyiro cha kuugombea huo ubunge, kuthibitishwa ubunge kiapo ni lazima, kabla ya hapo ni kusherehekea ushindi au uteuzi!

Wanaomchagua Spika ni kina nani wale? Hii habari ya "kuthibitishwa ubunge" iko katika ibara gani ya katiba?
 
Mimi sioni ulazima wa mawaziri kuwa wabunge. Wabunge waachwe kuwa wabunge na mawaziri waachwe wawe watendaji wa serikali.

Haya mambo ya mawaziri kuwa lazima wawe wabunge ni upumbavu tu. Hivi kuna hata anayejua sababu ya ulazima huo ni nini?

Kwani mawaziri wasipokuwa wabunge watashindwa kufanya kazi zao?

Dawa hapa ni ndogo sana - ondoa ulazima wa mawaziri kuwa wabunge.

That's a totally different debate.

Rationale - not that I support it- ni kwamba, mawaziri wakiwa wabunge watakuwa ni watu waliochaguliwa na wananchi. Sio rais kujiteulia ndugu zake tu.
 
Sijawahi sikia mbunge kateuliwa saa sita mchana alafu saa kumi jioni kawa waziri maana yake huyo waziri hata kazi za ubunge hazijui na hata bungeni hajawahi kufika na hawajui bunge likoje au limekaaje hao wengine hata dodoma hawajawahi kufika and yet sasa hivi ni mawaziri...IT CAN ONLY HAPPEN IN BONGO

Umeona eeh? Yaani ni ujinga ujinga mtupu!

Sasa sijui hata hiyo orientation ya bunge atapata lini.....
 
That's a totally different debate.

Rationale - not that I support it- ni kwamba, mawaziri wakiwa wabunge watakuwa ni watu waliochaguliwa na wananchi. Sio rais kujiteulia ndugu zake tu.

Mawaziri kutokuwa wabunge inaondoa utata wa mambo mengi sana.

Na hiyo rationale ni ya kipumbavu tu vile vile.

Na kama mawaziri wasingekuwa wabunge basi huu utata mnaobishania hapa wala usingekuwepo.

Yaani mambo mepesi mepesi tu kama haya yanatushinda. Huu ni uwendawazimu kabisa.
 
Mawaziri kutokuwa wabunge inaondoa utata wa mambo mengi sana.

Na hiyo rationale ni ya kipumbavu tu vile vile.

Rationale haiangalii ukweli kwamba waziri kuwa mbunge kunaleta conflict of interest na kuondoa integrity ya "checks and balances". Inaturudisha kwenye "rubber stamp parliament"

Ukihesabu wabunge walio mawaziri walivyo wengi, hata kama wabunge wa CCM wakiamua kuipinga serikali, sehemu yao kubwa watashindwa kwa sababu wao ndio serikali yenyewe.
 
Back
Top Bottom