Didia
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 719
- 258
Leo katika Kipindi cha Tuongee Asubuhi cha Star TV nimemuona Bw. Eric Shingongo akitangaza Tamasha la Wasanii Lenye Kuitwa "TAMASHA LA UZALENGO TANZANIA KWANZA" Katika maelezo yake lengo la tamasha ni kuwaunganisha wasanii kulinda amani ya nchi ambayo inaonekana kuanza kuvurugwa.
Hii ni njia nyingine ambayo wabinafsi wanaodhani wanajenga na huku wakibomoa amani ya Nchi Yetu Tanzania. Bw. Shingongo anapaswa kuelewa kuwa msingi wa Amani katika nchi na hata familia ni Haki. Ndio maana tulipo pata uhuru nguvu kubwa ya Hayati Baba wa Taifa ililenga kujenga Taifa lenye usawa na haki. Hivyo huwezi kuhubiri kujenga amani bila kuhubiri haki kutendeka katika jamii. Hata kama watanzania tungekuwa na chama/dini moja, pasipo haki, Amani haiwezi kudumu.
Natambua kuna wasanii wengi wabinafsi na au viraza ambao hawaoni au kuelewa matatizo yanayoikumba nchi hii na visababishi vyake hasa UFISADI, UBINAFSI WA VIONGOZI, UZEMBE WA SERIKALI KATIKA KUTATUA KERO ZA WANANCHI n.k. Wapo wasanii wengi ambao kwa vile kwa sasa wanapata vijisenti vya kuendea Club na au kuendesha Toyota Corolla wanadhani shida hakuna. Wasanii hawa huenda wasione hali ngumu ya maisha inayowakumba watanzania wenzao. Hawa watamuunga mkono Shingongo kama baadhi yao walivyo badili nyimbo zao na kuweka tungo za kusifia chanzo cha tatizo wakati wa kampeni za uchaguzi.
Hivi unaposema "Tanzania kwanza" ni yapi ambayo unataka yaje baadae? Wananchi, Siasa, Uchumi n.K? Hivi Mzalendo ni yupi? Yule anayesifia wizi na unyang'anyi, Anayekaa kimya bila kuchukua hatua dhidi ya uovu au anayekemea na kuweka maisha yake rehani kwa mstakabali wa Taifa?
WanaJF nisaidieni kwa kila namna kuwaelimisha wasanii wetu watoke gizani. Najua historia ya siasa ya Bw. Shingongo, bila shaka, malengo yake katika tamasha hili. Tusimuache azidi kutumia nafasi yake kupotosha wananchi.
Hii ni njia nyingine ambayo wabinafsi wanaodhani wanajenga na huku wakibomoa amani ya Nchi Yetu Tanzania. Bw. Shingongo anapaswa kuelewa kuwa msingi wa Amani katika nchi na hata familia ni Haki. Ndio maana tulipo pata uhuru nguvu kubwa ya Hayati Baba wa Taifa ililenga kujenga Taifa lenye usawa na haki. Hivyo huwezi kuhubiri kujenga amani bila kuhubiri haki kutendeka katika jamii. Hata kama watanzania tungekuwa na chama/dini moja, pasipo haki, Amani haiwezi kudumu.
Natambua kuna wasanii wengi wabinafsi na au viraza ambao hawaoni au kuelewa matatizo yanayoikumba nchi hii na visababishi vyake hasa UFISADI, UBINAFSI WA VIONGOZI, UZEMBE WA SERIKALI KATIKA KUTATUA KERO ZA WANANCHI n.k. Wapo wasanii wengi ambao kwa vile kwa sasa wanapata vijisenti vya kuendea Club na au kuendesha Toyota Corolla wanadhani shida hakuna. Wasanii hawa huenda wasione hali ngumu ya maisha inayowakumba watanzania wenzao. Hawa watamuunga mkono Shingongo kama baadhi yao walivyo badili nyimbo zao na kuweka tungo za kusifia chanzo cha tatizo wakati wa kampeni za uchaguzi.
Hivi unaposema "Tanzania kwanza" ni yapi ambayo unataka yaje baadae? Wananchi, Siasa, Uchumi n.K? Hivi Mzalendo ni yupi? Yule anayesifia wizi na unyang'anyi, Anayekaa kimya bila kuchukua hatua dhidi ya uovu au anayekemea na kuweka maisha yake rehani kwa mstakabali wa Taifa?
WanaJF nisaidieni kwa kila namna kuwaelimisha wasanii wetu watoke gizani. Najua historia ya siasa ya Bw. Shingongo, bila shaka, malengo yake katika tamasha hili. Tusimuache azidi kutumia nafasi yake kupotosha wananchi.