ERB acheni njaa

Snitch

Senior Member
Oct 22, 2011
165
42
Hii Engineers Registration Board nao wamezidi njaa, Wamekua wakiwakata Trainee Engineers ambao wanachelewa kusubmit Quarter Report on time na kuwapa fedha nusu na hata wanapowasilisha Report Ile Pesa hawawapatii ndio imeliwa...

Sasa Mimi najiuliza lengo ni la kufanya hivyo ni Zuri kwa maana ya kuhamasisha wasibweteke wafanye kazi kwa wakati na wasubmit Report kwa wakati,

Lakini , hawataki kupata ukweli kua delay nyingine haisababishwi na Trainee Engineer Bali ni SUPERVISORS,sasa je haki ya Trainee Engineer ni Ipi Kwani Hawa Ma Supervisors hawalipwi na wanafanya Kama vile basi tu na wengi wao ni wale Primitive kweli wanataka Kuabudiwa sana, sisemi wote ila wengi wao wako hivyo,

Je,hizi fedha baadae wanazipeleka wapi au ndio ufisadi?

Acheni ulafi kuna wengine mwezi wa tatu mfululizo hajapewa Pesa ya kujikimu????

Acheni ulafi na ufisadi wapeni Pesa zao na Kama Report haijasigniwa mnalalamika kwanini msiwasiliane na Supervisor na Wote mnawajua.

Kuchukua hatua ni kukata Pesa tu ila hamtaki kujua chanzo cha tatizo?
Tatizo ni Masupervisors sio Trainee wapeni Pesa zao...
 
Ungekuwa mwandishi mzuri ulikuwa na habari nzuri sana ya kuripoti.
Ila kuna point nime-miss ili niweze kuchangia kwa ufasaha.
Nina maswali haya:-

Kuna sheria/regulations zozote zinazo-guide submission of quarterly repors? Due date iko clear?
Kama uki-default muda wa kupeleka reports, adhabu ziko clear?

Nimegundua wakati mwingine interpretation ya hizi sheria inatuchanganya wote consumers na watumishi wa serikali, tunajikuta tunajikanganya.
Hakuna kitu kizuri kama kuwa clear na taratibu zinazokuongoza katika jambo, kuna wizara moja inatoa penalty kwenye malipo hiyo, mpaka basi.

Ila, kama tatizo ni supervisor, sioni kwa nini unalaumi ERB, hasa kama sheria iko clear. Ni kuongea na supervisor au stake holders wote kukaa pamoja na kuliongelea hili.

Ntarudi!
 
Ungekuwa mwandishi mzuri ulikuwa na habari nzuri sana ya kuripoti.
Ila kuna point nime-miss ili niweze kuchangia kwa ufasaha.
Nina maswali haya:-

Kuna sheria/regulations zozote zinazo-guide submission of quarterly repors? Due date iko clear?
Kama uki-default muda wa kupeleka reports, adhabu ziko clear?

Nimegundua wakati mwingine interpretation ya hizi sheria inatuchanganya wote consumers na watumishi wa serikali, tunajikuta tunajikanganya.
Hakuna kitu kizuri kama kuwa clear na taratibu zinazokuongoza katika jambo, kuna wizara moja inatoa penalty kwenye malipo hiyo, mpaka basi.

Ila, kama tatizo ni supervisor, sioni kwa nini unalaumi ERB, hasa kama sheria iko clear. Ni kuongea na supervisor au stake holders wote kukaa pamoja na kuliongelea hili.

Ntarudi!
Urudi kufanya nini wakati tumeshakuelewa....

Halafu hii biashara ya kujisajili kwenye mibodi inakeraga sana asee.

Yaani shule nikate mimi, kufaulu nifaulu mimi..... sitambuliki mpaka bodi inisajili......agrrrrrr
 
Urudi kufanya nini wakati tumeshakuelewa....

Halafu hii biashara ya kujisajili kwenye mibodi inakeraga sana asee.

Yaani shule nikate mimi, kufaulu nifaulu mimi..... sitambuliki mpaka bodi inisajili......agrrrrrr
Najua tatizo lako.Wewe na ripoti mbalimbali.Usijali tutandamana hicho kifungu cha ripoti na kusajiliwa kiondolewe..
 
Ha ha ha ha, basi sirudi tena.

Ukiona unasajiliwa ujue umequalify kuwa profesheno.
Mie sijawahi sajiliwa, umama ntilie huu!!

Urudi kufanya nini wakati tumeshakuelewa....

Halafu hii biashara ya kujisajili kwenye mibodi inakeraga sana asee.

Yaani shule nikate mimi, kufaulu nifaulu mimi..... sitambuliki mpaka bodi inisajili......agrrrrrr
 
Ha ha ha ha, basi sirudi tena.

Ukiona unasajiliwa ujue umequalify kuwa profesheno.
Mie sijawahi sajiliwa, umama ntilie huu!!
Sijawahi kusajiliwa kwenye unywaji wa bia, lakini nikiugua TBL na SBL wananitumia kadi ya Get Well Soon.
 
Kweli trainee hawajaliwi hata kidogo maana hata hiyo ya kujikimu yenyewe haitoshi...fikiria home bunju umepata pa kufanyia trainee mbagala? Hata usafiri tu haitoshi. Mungu awepe ujasiri wa kuirekebisha japo kidogo
 
Halafu mie baada ya pasaka tu ndio nafata trainee certificate,hata hizo riport sijajua utaratibu wake wa kusubmit...msaada plz niwe updated jamani!!!
 
moja una bahati kama unakatwa nusu wengine wanakatwa zote

mbili mara nyingi kabla hawajaacha kukupa wanakupigia simu wanakuambia unadaiwa report na wanakupa deadline halafu usipopeleka wanakata

tatu mwenye jukumu la kupeleka taarifa kuwa report itachelewa ni trainee sio mpaka utafutwe

nne nafikiri wakikata wanatafuta mtu mwingine wanampa maana wapo wengi wanaohitaji

hayo ndio maoni yangu.
 
Halafu mie baada ya pasaka tu ndio nafata trainee certificate,hata hizo riport sijajua utaratibu wake wa kusubmit...msaada plz niwe updated jamani!!!

natamani nikuelewe embu nijibu umeshajiunga na seap au bado?
 
Nimeshangaa kwenye post hii kufahamu kwamba kunakuwa na "Supervisors wa mainjinia ambao ni primitives". Nilitegemea kwamba supervisor wa engineer lazima awe professional engineer ili aweze kumpika huyo graduate aive na kuwa professional vile vile. Sasa kama mnakamata mtu yeyote mtaani kuwapika mainjinia wetu, tutakuwa tunakwenda kinyume na malengo ya hayo mafunzo kwa vitendo kwa mainjinia wetu.
 
Urudi kufanya nini wakati tumeshakuelewa....

Halafu hii biashara ya kujisajili kwenye mibodi inakeraga sana asee.

Yaani shule nikate mimi, kufaulu nifaulu mimi..... sitambuliki mpaka bodi inisajili......agrrrrrr

ni muhimu kusajili kwa sababu we need the right people and classroom performance does not guarantee that your competent in the field, thats why in every field and jobs experience counts. otherwise even those ladies who performed in class by sleeping with lecturers will be counted competent.
 
Nimeshangaa kwenye post hii kufahamu kwamba kunakuwa na "Supervisors wa mainjinia ambao ni primitives". Nilitegemea kwamba supervisor wa engineer lazima awe professional engineer ili aweze kumpika huyo graduate aive na kuwa professional vile vile. Sasa kama mnakamata mtu yeyote mtaani kuwapika mainjinia wetu, tutakuwa tunakwenda kinyume na malengo ya hayo mafunzo kwa vitendo kwa mainjinia wetu.

every trainee must must have a professional engineer and not otherwise that's why the logbooks and reports must have a professional engineer's stamp and signature, company stamps are not even allowed so its not anybody.
 
ahsante kwa maada ya erb mi ningependa tu kuwataadharisha kuwa rushwa itawapeleka pabaya, kuna ukiukaji mkubwa sana wa sheria na pia quality imeshuka mfano wametengeza engineers. architects and quantity surveyors directory kwa kweli ni jambo zuri lakini imewaletea aibu kwa sababu details nyingi either zimekosewa au zinamiss lakini kibaya ni pale ambapo wanamiss details za board member this shows high level of lack of seriousness its a shame na alikabidhiwa rais siku ya uzinduzi jamani watanzania tufanye kazi, document ikiandikwa united republic of Tanzania should be something serious.
 
moja una bahati kama unakatwa nusu wengine wanakatwa zote

mbili mara nyingi kabla hawajaacha kukupa wanakupigia simu wanakuambia unadaiwa report na wanakupa deadline halafu usipopeleka wanakata

tatu mwenye jukumu la kupeleka taarifa kuwa report itachelewa ni trainee sio mpaka utafutwe

nne nafikiri wakikata wanatafuta mtu mwingine wanampa maana wapo wengi wanaohitaji

hayo ndio maoni yangu.

Ndugu,

Hatukai kila kitu ila maisha yamepanda sana sasa unakuta hata lengo halitimii kwakua wanaosimamia ni Wababaishaji na wanaosimamiwa nao wanababaisha,

Kwanza si kweli Kama wakikukata wanatafuta Mtu mwingine Kwani Budget iko kwa kila member and they still encouraging new members to join as many as they can,

Kwahiyo,suala la kukata Pesa tunataka kujua Zinakwenda wapi na mbona siku za nyuma waliwakata na wakasubmit Report hawajawaongezea mpaka Leo na makosa sio ya Trainee ni ya Ma supervisors, na ujue Hawa supervisors wengine wako busy na wengine ni wale wanaopenda Kuabudiwa na hata ukisema ubadilishiwe supervisor labda utafute company au sehemu nyingine kitu ambacho bado ni Tatizo kupata sehemu ya kufanyia SEAP.

Kwahiyo hili,waohawalioni Bali wanajua kukata fedha tu na sio kuweka utaratibu mzuri wa kujua km Trainee anafanya vizuri na anagain kitu wao wanataka report tu,


Watajitokeza humu kudefend hili kwa kusema oh wengi hawasubmit report ?

Je mnajua Kama tatizo nisupervisors...

??????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom