BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Kada wa CCM alikiri kuchota mamilioni BoT
Shadrack Sagati na Neema Mgonja
Daily News; Thursday,November 20, 2008 @21:15
Upande wa mashitaka katika moja ya kesi za ufisadi umeiambia mahakama kuwa mmoja wa washtakiwa katika kesi ya ufisadi, Rajabu Shaban Maranda, alikiri kushirikiana na maofisa watatu wa Benki Kuu (BoT) kuchota mamilioni ya fedha.
Maranda ambaye ni Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kigoma anashtakiwa kwa kuiba Sh milioni 207 kutoka katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kwa kutumia kampuni ya Rashhas.
Akisoma maelezo ya awali, Wakili wa Serikali Boniface Stanislaus aliiambia mahakama hiyo kuwa mshtakiwa baada ya kukamatwa na kuhojiwa na vyombo vya dola alikiri kufanya wizi huo wa Sh milioni 207.3.
Akielezea mwanzo wa kampuni iliyotumika kuchotea mamilioni hayo ya fedha, wakili huyo alidai kuwa Maranda kwa mara ya kwanza alisajili kampuni ya Rashhaz Tanzania Ltd kwa msajili wa kampuni na Mkurugenzi mwenzake aliyetajwa kuwa ni Maranda Rajabu Maranda.
Alidai kuwa ukusanyaji wa madeni haikuwa kazi ya kampuni ya Rashhaz tangu isajiliwe na haikuwahi kubadili kazi zake ambazo zimeandikishwa Brela. Aliendelea kudai kuwa Desemba 10, 2004 Maranda aliwasilisha waraka Benki Kuu ukimtaja
Jaffer Hussein Jaffer kuwa ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Rashhas (T) Ltd na kwamba kampuni hiyo ilikuwa imeteuliwa na kampuni ya General Marketing ya India kukusanya deni la dola za Marekani 1,252,480.48.
Mbele ya Hakimu Mkazi wa Kisutu Hezron Mwankenja, wakili huyo alidai kampuni ya Rashhaz na Rashhas ni vitu viwili tofauti; lakini Maranda kwa kutumia udanganyifu alidai kuwapo kwa mabadiliko ya wakurugenzi na kumwingiza Jaffer kuwa ni mmoja wa wakurugenzi wa Rashhas wakati ni uongo.
Alidai miezi saba baadaye Maranda Julai 14, 2005 alitumia jina la Jaffer kama mmoja wa wakurugenzi wa Rashhas akaandika barua kwa Gavana wa BoT akimjulisha kuwa kampuni yake hiyo imepewa jukumu na kampuni ya General Marketing ya India kudai rupia 8,141,123.09.
Agosti 11 maofisa wawili wa BoT waliokuwa Kitengo cha Madeni Iman Mwakyosa na Esther Mary Komu waliidhinisha deni hilo kulipwa kwa kampuni feki ya mshtakiwa. Alidai maofisa hao waliidhinisha kwa makusudi malipo hayo licha ya kuwa barua iliyoandikwa na kampuni ya Rashhas iliomba ilipwe dola za Marekani wakati fedha iliyokuwa inadaiwa katika akaunti ya EPA ilikuwa ni rupia ya India.
Kwa upande wa mshtakiwa wa nne Bosco Kimela ambaye alikuwa Katibu wa BoT inadaiwa aliidhinisha malipo hayo kufanywa na akashauri barua ya maombi iandikwe na iombe kulipwa fedha za rupia na sio dola za Marekani kama ilivyokuwa katika barua ya awali.
Alidai Agosti 12, 2005 Mwakyusa na Komu walimtaarifu Maranda kuwa maombi yake yamekubaliwa na BoT, lakini wakamshauri akaandike barua inayoonyesha kutaka alipwe fedha za rupia 8,141,123.09 na aiwasilishe haraka na sio malipo ya dola.
Baada ya kuelezwa hivyo siku hiyo hiyo Maranda akitumia jina la Jaffer kama Mkurugenzi wa Rashhas aliwasilisha barua mpya BoT ya maombi ikionyesha kuwa ilisainiwa mjini Mumbai, India Julai 12, 2004 na kushuhudiwa na wakili aliyetajwa M.V Shinde wa Mahakama Kuu ya Mumbai, India.
Lakini barua hiyo haikuwa imesainiwa na ofisa yeyote wa Rashhas lakini Maranda akaithibitishia benki hiyo kuwa nyaraka hiyo ilikuwa halali kisheria. Baadaye Agosti 15, 2005 BoT iliidhinisha malipo kwa kampuni halali ya Rashhaz na kupitishia fedha hizo katika akaunti zake ambazo Maranda alizichukua katika mikupuo minne.
Hata hivyo washtakiwa wote wanne walikubali majina yao na nafasi zao lakini walikana maelezo yote yaliyosomwa na Wakili wa Serikali. Mshtakiwa wa pili alikana kuwa na cheo cha Kaimu Mkuu wa Idara ya Madeni BoT. Upande wa mashitaka umeiambia mahakama hiyo kuwa unatarajia kuwaita mashahidi 16 akiwamo Naibu Msajili wa Kampuni (Brela) Andrew Mkapa kutoa ushahidi katika kesi hiyo.
Miongoni mwa mashahidi hao yumo Twilumba Tawara wa Benki ya Kenya (KCB) na Ronald Manongi wa Commercial Bank of Afrika (CBA) ambako BoT ilipitishia fedha hizo kwa ajili ya kulipwa kwa Maranda. Wamo pia maofisa wa BoT ambao ni Emmanuel Boazi, Tamali Mwakilema, Elisa Kisangya, Peter Noni, Rashid Mwanga, Samwel Mark, Athumani Mtengeti na Stela Chaula.
Wengine ni maofisa wa Polisi SP Mkonyi na ASP Salumu Kisali. Pia wengine ni mmoja wa wakurugenzi wa Rashhaz, Jaffer Hussein Jaffer ambaye jina lake lilitumiwa kufanyia wizi huo na Joseph Sheffu Mkaguzi wa Hesabu wa Kampuni ya Ernst and Young. Upande wa mashitaka uliiambia mahakama kuwa aliyetoa taarifa za wizi huo ni Sheffu ambaye ni mkaguzi ambaye kampuni yake iligundua wizi huo. Kesi hiyo itaanza kusikilizwa Januari 20.
Shadrack Sagati na Neema Mgonja
Daily News; Thursday,November 20, 2008 @21:15
Upande wa mashitaka katika moja ya kesi za ufisadi umeiambia mahakama kuwa mmoja wa washtakiwa katika kesi ya ufisadi, Rajabu Shaban Maranda, alikiri kushirikiana na maofisa watatu wa Benki Kuu (BoT) kuchota mamilioni ya fedha.
Maranda ambaye ni Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kigoma anashtakiwa kwa kuiba Sh milioni 207 kutoka katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) kwa kutumia kampuni ya Rashhas.
Akisoma maelezo ya awali, Wakili wa Serikali Boniface Stanislaus aliiambia mahakama hiyo kuwa mshtakiwa baada ya kukamatwa na kuhojiwa na vyombo vya dola alikiri kufanya wizi huo wa Sh milioni 207.3.
Akielezea mwanzo wa kampuni iliyotumika kuchotea mamilioni hayo ya fedha, wakili huyo alidai kuwa Maranda kwa mara ya kwanza alisajili kampuni ya Rashhaz Tanzania Ltd kwa msajili wa kampuni na Mkurugenzi mwenzake aliyetajwa kuwa ni Maranda Rajabu Maranda.
Alidai kuwa ukusanyaji wa madeni haikuwa kazi ya kampuni ya Rashhaz tangu isajiliwe na haikuwahi kubadili kazi zake ambazo zimeandikishwa Brela. Aliendelea kudai kuwa Desemba 10, 2004 Maranda aliwasilisha waraka Benki Kuu ukimtaja
Jaffer Hussein Jaffer kuwa ni mmoja wa wakurugenzi wa kampuni ya Rashhas (T) Ltd na kwamba kampuni hiyo ilikuwa imeteuliwa na kampuni ya General Marketing ya India kukusanya deni la dola za Marekani 1,252,480.48.
Mbele ya Hakimu Mkazi wa Kisutu Hezron Mwankenja, wakili huyo alidai kampuni ya Rashhaz na Rashhas ni vitu viwili tofauti; lakini Maranda kwa kutumia udanganyifu alidai kuwapo kwa mabadiliko ya wakurugenzi na kumwingiza Jaffer kuwa ni mmoja wa wakurugenzi wa Rashhas wakati ni uongo.
Alidai miezi saba baadaye Maranda Julai 14, 2005 alitumia jina la Jaffer kama mmoja wa wakurugenzi wa Rashhas akaandika barua kwa Gavana wa BoT akimjulisha kuwa kampuni yake hiyo imepewa jukumu na kampuni ya General Marketing ya India kudai rupia 8,141,123.09.
Agosti 11 maofisa wawili wa BoT waliokuwa Kitengo cha Madeni Iman Mwakyosa na Esther Mary Komu waliidhinisha deni hilo kulipwa kwa kampuni feki ya mshtakiwa. Alidai maofisa hao waliidhinisha kwa makusudi malipo hayo licha ya kuwa barua iliyoandikwa na kampuni ya Rashhas iliomba ilipwe dola za Marekani wakati fedha iliyokuwa inadaiwa katika akaunti ya EPA ilikuwa ni rupia ya India.
Kwa upande wa mshtakiwa wa nne Bosco Kimela ambaye alikuwa Katibu wa BoT inadaiwa aliidhinisha malipo hayo kufanywa na akashauri barua ya maombi iandikwe na iombe kulipwa fedha za rupia na sio dola za Marekani kama ilivyokuwa katika barua ya awali.
Alidai Agosti 12, 2005 Mwakyusa na Komu walimtaarifu Maranda kuwa maombi yake yamekubaliwa na BoT, lakini wakamshauri akaandike barua inayoonyesha kutaka alipwe fedha za rupia 8,141,123.09 na aiwasilishe haraka na sio malipo ya dola.
Baada ya kuelezwa hivyo siku hiyo hiyo Maranda akitumia jina la Jaffer kama Mkurugenzi wa Rashhas aliwasilisha barua mpya BoT ya maombi ikionyesha kuwa ilisainiwa mjini Mumbai, India Julai 12, 2004 na kushuhudiwa na wakili aliyetajwa M.V Shinde wa Mahakama Kuu ya Mumbai, India.
Lakini barua hiyo haikuwa imesainiwa na ofisa yeyote wa Rashhas lakini Maranda akaithibitishia benki hiyo kuwa nyaraka hiyo ilikuwa halali kisheria. Baadaye Agosti 15, 2005 BoT iliidhinisha malipo kwa kampuni halali ya Rashhaz na kupitishia fedha hizo katika akaunti zake ambazo Maranda alizichukua katika mikupuo minne.
Hata hivyo washtakiwa wote wanne walikubali majina yao na nafasi zao lakini walikana maelezo yote yaliyosomwa na Wakili wa Serikali. Mshtakiwa wa pili alikana kuwa na cheo cha Kaimu Mkuu wa Idara ya Madeni BoT. Upande wa mashitaka umeiambia mahakama hiyo kuwa unatarajia kuwaita mashahidi 16 akiwamo Naibu Msajili wa Kampuni (Brela) Andrew Mkapa kutoa ushahidi katika kesi hiyo.
Miongoni mwa mashahidi hao yumo Twilumba Tawara wa Benki ya Kenya (KCB) na Ronald Manongi wa Commercial Bank of Afrika (CBA) ambako BoT ilipitishia fedha hizo kwa ajili ya kulipwa kwa Maranda. Wamo pia maofisa wa BoT ambao ni Emmanuel Boazi, Tamali Mwakilema, Elisa Kisangya, Peter Noni, Rashid Mwanga, Samwel Mark, Athumani Mtengeti na Stela Chaula.
Wengine ni maofisa wa Polisi SP Mkonyi na ASP Salumu Kisali. Pia wengine ni mmoja wa wakurugenzi wa Rashhaz, Jaffer Hussein Jaffer ambaye jina lake lilitumiwa kufanyia wizi huo na Joseph Sheffu Mkaguzi wa Hesabu wa Kampuni ya Ernst and Young. Upande wa mashitaka uliiambia mahakama kuwa aliyetoa taarifa za wizi huo ni Sheffu ambaye ni mkaguzi ambaye kampuni yake iligundua wizi huo. Kesi hiyo itaanza kusikilizwa Januari 20.