Enzi hizo JKT....

Kwa tuliobahatika kuhenya JKT enzi hizo,embu tujikumbushe top ten za disco la enzi hizo. Naanza:
Kule kwa chinova,
kule kule,
kule kwa chinoova,
tunasonga na kuzimbabwe,
masika na toye,toyela
toye,toya na kuzimbabwe,
mama na babaeee,tunasonga na kuzimbabwe.
Jamani ongezeni mistari hapa na pia angusheni na ma singo mengine yaliyovuma JKT enzi hizo !
Wewe mtani wangu Bishanga nasikia ulikuwa selule kule, kwa hiyo kazi yako ilikuwa ni kulinda hanga...kweli?.
 
Kuna mtu aliwahi kunipa hadithi kama hii ya kwako kuwa wanachoka mpaka inafika mahali hawatamaniani tena,...inaonekana ilikuwa raha sana lol.
jkt haijali wewe ni mtoto wa mkulima,tajiri,nyerere wala kawawa,wote mlikuwa mnachangnywa kapu moja,na ole wako ijulikane we babako Rais,waziri,katibu mkuu au MD wa shirika la serikali,utashughulikiwa mpaka unyooke.
Jkt was the best leveller of our society.
 
Wewe mtani wangu Bishanga nasikia ulikuwa selule kule, kwa hiyo kazi yako ilikuwa ni kulinda hanga...kweli?.
selule mwenyewe! Mi nilikuwa mtunza bustani bana ruvu fire coy,ila kwa wizi wa nyama (kijeshi inaitwa kusogeza) mi ndo nilikuwa mwenyewe,naziibua za moto kwenye gudulia.Siku moja MP akanibamba live,nikafungwa peki bega na mzigo wa nyama,siku nzima nikakimbizwa uwanjani naimba...'mimi mwizi wa nyama'...hahahahaaa jkt bana!
 
Du hi hi hi...umenikumbusha mambo ya kuwania top layer usawa wa gudulia!.
mtani,gudulia lenyewe si mpaka ulifikie?unaikumbuka kwata ya kuelekea kwenye gudulia? Halafu mkisha kula ni moja,moja mbili tatu,moja,yaani maafande wanawarusha eti wanapanga matofali ya jeshi matumboni mwenu!
 
jkt haijali wewe ni mtoto wa mkulima,tajiri,nyerere wala kawawa,wote mlikuwa mnachangnywa kapu moja,na ole wako ijulikane we babako Rais,waziri,katibu mkuu au MD wa shirika la serikali,utashughulikiwa mpaka unyooke.
Jkt was the best leveller of our society.
Kama ni hivyo inatakiwa irudishwe...
 
JKT.....lilikuwa na faida zake: mojawapo ukakamavu na kujua kuishi mahali popote! It was a good experience.
 
  • Thanks
Reactions: a45
Moja ya vitu nilitamani sana lakini nikavikosa!! But nilipeenda ili nikawe fit zaid na kukaa mkao wa ki-askari zaidi though sio askari. Kitu kilichonisikitisha ni kusema ilifundisha "uraia" na "uzalendo" lakini nikiangalia kwa asilimia kubwa kizazi kilichotuonyesha kukosa uzalenda kwa mali na rasilimali za nchi hii ni kizazi kilichopita JKT, japo pia kizazi kilichokosa JKT nacho kimekuwa ni kizazi cha kulalamika saaaaana bila actions!

Hebu wanikonvisi tena upya kwenda JKT labda nitafikiria
 
Nilipenda every moment ya JKT hasa baada ya kuzoea. Hii ilichukua miezi mitatu plus.
Homa ilikuwa inaanza kupanda baada ya kupata form iliyokuambia unaenda kambi gani. Basi hapo utacheki na wenzio ili uone uko na kina nani.
Mi nilipangiwa Msange/Masange Tabora, lakini nikavecha nikaenda Makutupora. Kwata huko kwa kwenda mbele.
Ila nilijiunga na Usanii ( Kikundi cha Sanaa cha Jeshi ) ambako nilikuwa mahiri hadi nikaombewa na AFande incharge wa Dept hiyo nisikatwe bogi.
Marafiki tuliokuwa nao JKT wamekuwa wa kudumu maana mnakuwa mmepitia mambo magumu but mazuri pamoja.

Sijuti kwenda JKT.... kwa kweli.

AKA ...... wa Makutupora... LOL ( n.b: AK = Askari wa Kike) maana tulikuwa na Force Number.
Mpo hapo?
 
Naongezea.....
ha ha ha ha

siku moja Makutu, ( short form ya Makutupora) mdada mmoja AK .. akawa ana rafiki yake wa kiume. Sasa kumbe walikuwaga wanakutana na may be ku vi do huko katika hanga la wanaume. Kumbuka JKT mahanga yote ( mabweni) ya maaskari wa kike ni Serengeti na yako mbali na wa kiume.
Nadhani wale vijana wenzie na yule mkaka aidha walichoshwa na kula ugali kwa picha ya samaki ( tehe) au walichoshwa kuringishiwa mwenzao anapata wakati wao wanacheza golf usiku; wakamchomea kwa MP Kimaro...

zile time ambazo yule mdada alikuwa anatoroka kwenda kule chini mahanga ya wanaume ( nikifikiria hivi leo with hindsight advantage, nadhani ilikuwa baada ya disko la usiku kombania, alikuwa harejei nasi Serengeti maana pana kaumbali ).
siku hiyo yuko ndani ya neti ya mkaka, MP KIMARO huyu hapa!
mida hiyo saa tisa usiku hivi. yaani usiku mnene.
Valangati na Timbwili lililozuka hapo, usipime. Ukapigwa ukunga kuamsha kikosi .. na wao wahanga wakaambiwa wazunguke kikosi kizima wakiimba kuwa 'sisi Waz....' imagine.
Na nadhani walifungwa pia ( ndio JKT kulikuwa na jela) maana tulipoondoka siku rasmi ya kufunga msimu wetu , 30 June 198... wao walibaki.

mmh !
 
Hehehe! Ila ilikuwa nzuri sana, vijana wanapata ukakamavu kabla ya kwenda chuoni..
jkt ilikuwa pia inaondoa dhana ya matabaka maana wote mlikuwa mnaipata fresh equally,hakuna cha mtoto wa bakresa wala reginald mengi.
 
JKT.....lilikuwa na faida zake: mojawapo ukakamavu na kujua kuishi mahali popote! It was a good experience.
wee said Kerren,nambie dada experience yako siku ya kwanza afande anakurushia bukta na T shirt kisha anakwambia hilo ndo gauni lako la harusi?
 
Moja ya vitu nilitamani sana lakini nikavikosa!! But nilipeenda ili nikawe fit zaid na kukaa mkao wa ki-askari zaidi though sio askari. Kitu kilichonisikitisha ni kusema ilifundisha "uraia" na "uzalendo" lakini nikiangalia kwa asilimia kubwa kizazi kilichotuonyesha kukosa uzalenda kwa mali na rasilimali za nchi hii ni kizazi kilichopita JKT, japo pia kizazi kilichokosa JKT nacho kimekuwa ni kizazi cha kulalamika saaaaana bila actions!

Hebu wanikonvisi tena upya kwenda JKT labda nitafikiria
ngoja tuwaite vingunge wa jukwaa la siasa waje wajibu hii hoja,sisi wengine ni magwiji wa mmu na chit chat.
 
Nilipenda every moment ya JKT hasa baada ya kuzoea. Hii ilichukua miezi mitatu plus.
Homa ilikuwa inaanza kupanda baada ya kupata form iliyokuambia unaenda kambi gani. Basi hapo utacheki na wenzio ili uone uko na kina nani.
Mi nilipangiwa Msange/Masange Tabora, lakini nikavecha nikaenda Makutupora. Kwata huko kwa kwenda mbele.
Ila nilijiunga na Usanii ( Kikundi cha Sanaa cha Jeshi ) ambako nilikuwa mahiri hadi nikaombewa na AFande incharge wa Dept hiyo nisikatwe bogi.
Marafiki tuliokuwa nao JKT wamekuwa wa kudumu maana mnakuwa mmepitia mambo magumu but mazuri pamoja.

Sijuti kwenda JKT.... kwa kweli.

AKA ...... wa Makutupora... LOL ( n.b: AK = Askari wa Kike) maana tulikuwa na Force Number.
Mpo hapo?
kwa hiyo mkuu ulijifunza na utaalam wa kilimo cha zabibu,mimi jkt nilitika nikiwa bingwa wa gardening,kuchoma mkaa na kufyatua tofali,of course na kufyatua SMG (sikuji kwa nini AK47 hazikuwepo).
 
Naongezea.....
ha ha ha ha

siku moja Makutu, ( short form ya Makutupora) mdada mmoja AK .. akawa ana rafiki yake wa kiume. Sasa kumbe walikuwaga wanakutana na may be ku vi do huko katika hanga la wanaume. Kumbuka JKT mahanga yote ( mabweni) ya maaskari wa kike ni Serengeti na yako mbali na wa kiume.
Nadhani wale vijana wenzie na yule mkaka aidha walichoshwa na kula ugali kwa picha ya samaki ( tehe) au walichoshwa kuringishiwa mwenzao anapata wakati wao wanacheza golf usiku; wakamchomea kwa MP Kimaro...

zile time ambazo yule mdada alikuwa anatoroka kwenda kule chini mahanga ya wanaume ( nikifikiria hivi leo with hindsight advantage, nadhani ilikuwa baada ya disko la usiku kombania, alikuwa harejei nasi Serengeti maana pana kaumbali ).
siku hiyo yuko ndani ya neti ya mkaka, MP KIMARO huyu hapa!
mida hiyo saa tisa usiku hivi. yaani usiku mnene.
Valangati na Timbwili lililozuka hapo, usipime. Ukapigwa ukunga kuamsha kikosi .. na wao wahanga wakaambiwa wazunguke kikosi kizima wakiimba kuwa 'sisi Waz....' imagine.
Na nadhani walifungwa pia ( ndio JKT kulikuwa na jela) maana tulipoondoka siku rasmi ya kufunga msimu wetu , 30 June 198... wao walibaki.

mmh !

du! Hawatamsahau afande kimaro.sisi tulikuwa na CO makame rashid,wakati huo kanali,ukiweza kucheza mpira tu kwake ulikuwa umeula ni shushi tu.
 
Back
Top Bottom