Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,227
- 113,579
Enzi za ma Ikarusi kumbakumba...
Enzi hizo za Bahari beach hotel, Kunduchi beach hotel, Rungwe oceanic, Silversands hotel, Africana....daah those were the days.
Nilikuwa napenda sana kwenda Africana kwa sababu walikuwaga wanafuga wanyama pori pale kwa mbele upande wa kushoto kwenye entrance. Basi siku moja mi na mdingi tukaenda pale. Mdingi alikuwa na mkutano. Basi mimi nikaenda zangu kuwacheki wanyama. Palikuwa na kila aina ya wanyama lakini mimi nilikuwa fascinated sana na simba. Ilikuwa mida ya saa kumi na mbili jioni.
Out of nowhere yule simba dume akaunguruma bana....heheheheee ebana eeh....usiambiwe na mtu. Muungurumo wa simba dume kiboko. Manake ardhi ilirindima utadhani kulikuwa na tetemeko. Mimi sikujua kilichokuwa kinaendelea maana kama vile nilipoteza fahamu kiaina. Kwa kweli sitaisahau hiyo siku maana mpaka leo hii ile sauti bado naisikia.
Oooh halafu mnakumbuka enzi zile wageni wakiwatembelea kutoka bushi mnawapeleka uwanja wa ndege kwenda kutembea...lol.....man oh man...we have come a long way....pia mnawapeleka bandarini kwenda kuangalia meli. Mimi nilikuwa lazima nivalie suruali yangu ya mchele mchele tulipokuwa tukienda uwanja wa ndege. Nilikuwa natooooka mwenyewe...lazima nipendeze.
Enzi hizo tunaenda kuazima movie pale empire....mtaani ni watu wachache tu wenye vcr....basi jumapili lazima watoto wa jirani waje kuangalia movie....movie za kihindi...Disco Dancer...akina Mithun Chakraboty, Amitah Bachan, Govinda...Amjad Khan....
Duh enzi hizo bana.
Enzi hizo za Bahari beach hotel, Kunduchi beach hotel, Rungwe oceanic, Silversands hotel, Africana....daah those were the days.
Nilikuwa napenda sana kwenda Africana kwa sababu walikuwaga wanafuga wanyama pori pale kwa mbele upande wa kushoto kwenye entrance. Basi siku moja mi na mdingi tukaenda pale. Mdingi alikuwa na mkutano. Basi mimi nikaenda zangu kuwacheki wanyama. Palikuwa na kila aina ya wanyama lakini mimi nilikuwa fascinated sana na simba. Ilikuwa mida ya saa kumi na mbili jioni.
Out of nowhere yule simba dume akaunguruma bana....heheheheee ebana eeh....usiambiwe na mtu. Muungurumo wa simba dume kiboko. Manake ardhi ilirindima utadhani kulikuwa na tetemeko. Mimi sikujua kilichokuwa kinaendelea maana kama vile nilipoteza fahamu kiaina. Kwa kweli sitaisahau hiyo siku maana mpaka leo hii ile sauti bado naisikia.
Oooh halafu mnakumbuka enzi zile wageni wakiwatembelea kutoka bushi mnawapeleka uwanja wa ndege kwenda kutembea...lol.....man oh man...we have come a long way....pia mnawapeleka bandarini kwenda kuangalia meli. Mimi nilikuwa lazima nivalie suruali yangu ya mchele mchele tulipokuwa tukienda uwanja wa ndege. Nilikuwa natooooka mwenyewe...lazima nipendeze.
Enzi hizo tunaenda kuazima movie pale empire....mtaani ni watu wachache tu wenye vcr....basi jumapili lazima watoto wa jirani waje kuangalia movie....movie za kihindi...Disco Dancer...akina Mithun Chakraboty, Amitah Bachan, Govinda...Amjad Khan....
Duh enzi hizo bana.