Chatumkali
JF-Expert Member
- Sep 9, 2011
- 2,037
- 458
Ilikuwa piga nikupige kati ya mwanasiasa John Komba na walimu wa Mbinga.Mh aliwajia juu walimu kwa kushangilia watoto wetu kufeli mtihani wa drs la saba.Walimu nao wakajaribu kutunisha misuli wakanywea!Hivi serikali imejaribu kujiuliza kwanini watoto wanafeli halafu walimu wao wanaangusha shangwe kama ya harusi?Hapa tatizo ni nini?Ni kwanini tumefikia mahala sasa watanzania wanashangilia pindi wanapopata matokeo HASI?
Majuzi tulishuhudia mashabiki wa soka wanashangilia Kilimanjaro stars kufungwa!Sasa walimu wanashangilia vijana kufeli!Nachelea tusifike mahali madaktari nao wakashangilia wagonjwa wakifa,askari wa usalama barabarani nao wakashangilia ajali zikitokea,polisi wakashangilia wakitorokwa na mwizi,JWTZ wacheze sebene nchi ikivamiwa na ikitokea wakulima nao wakasherehekea kwa mvua kutokunyesha basi tujue kiama cha nchi kimefika.Watawala mtafakari na mchukue hatua maana ni dhahiri kuna kitu hakipo sawa.KAZI KWENU!
Majuzi tulishuhudia mashabiki wa soka wanashangilia Kilimanjaro stars kufungwa!Sasa walimu wanashangilia vijana kufeli!Nachelea tusifike mahali madaktari nao wakashangilia wagonjwa wakifa,askari wa usalama barabarani nao wakashangilia ajali zikitokea,polisi wakashangilia wakitorokwa na mwizi,JWTZ wacheze sebene nchi ikivamiwa na ikitokea wakulima nao wakasherehekea kwa mvua kutokunyesha basi tujue kiama cha nchi kimefika.Watawala mtafakari na mchukue hatua maana ni dhahiri kuna kitu hakipo sawa.KAZI KWENU!