Enyi serikali na DAWASCO, kero ya maji Dar hasa Kimara na Mbezi itaisha lini?

Kwa taarifa yako, maji kimara hayawezi kupatikana. Wauza maji wote wametengeneza mtandao wao na watu wa DAWASCO, ili wakate maji wao waje kutuuzia na magari. Jaribu kufanya utafiti utaelewa na kama kuna mtu anabisha alete

sababu za kukosekana maji sehemu hizo.
Nahisi itakuwa kweli. Nasikia waksti mwingine wanafumlngulia pressure ndogo km ushahidi tu! Iweje uwe karibu na barabara, eti usipate maji? Hawa jamaa wamekuwa sugu kabisa!
 
Mwanzo mlisema mwisho wa March, baadaye mkasema May, baadaye July. Yaani imekuwa ni mwendo wa kusogeza tarehe mbele!

Je, shida ni nini? Bomba bado halijamalizika au nini? Ajabu ni kwamba hata zile sehemu tulizokuwa tunapata maji walau mara moja kwa wiki sasa ni miezi inakwenda mitatu hatupati hata tone! Shida ni nini jamani.

Kimara na Mbezi yote, ukiacha baadhi ya watu walio usawa wa si zaidi mita mia tano kutoka Morogoro road maji hayafiki kabisa. Tatizo ni nini? Mbona mwaka jana shida haikuwa kubwa hivi?

Tafadhali sikieni kilio chetu, enyi wahusika, na mtoe taarifa nini kinaendelea!
Tatizo mnyika na kubenea hawafuatilii suala hilo. Wameshikilia kufuatilia mambo ya maandamano tu. Maendeleo kwenye majimbo hawana mpango nayo.
 
Huku kwetu walituambia tuchimbe mfereji wa kutandaza mpira wa maji,, siku,, wiki,, miezi inakatika hatuoni mpira wala nini,, hadi tunaambiwa tuhamie Dodoma hatujapata maji wenzenu,,
 
Tunashindwa kutoa Maji mto Ruvu mpaka Dar tuu hapo harafu tunazungumzia nchi itakua ya Viwanda bila maji wala umeme hakuna kitu kama hicho...
 
Kwa taarifa yako, maji kimara hayawezi kupatikana. Wauza maji wote wametengeneza mtandao wao na watu wa DAWASCO, ili wakate maji wao waje kutuuzia na magari. Jaribu kufanya utafiti utaelewa na kama kuna mtu anabisha alete sababu za kukosekana maji sehemu hizo.
Inawezekana mkuu. Kuna figisu figisu za kufa mtu.
 
Kule Ununio karibu na kwa wasomali bomba kubwa limepasuka WIKI sasa wakazi hawapati maji.Watu wa Dawasco Boko nendeni mkarekebishe, maji yanapotea bure
 
Oneni mabomba yanavyo tiririsha tu maji no repair!;Wengi hatuna maji,magari ya maji yanaongezeka kila kukicha tena yamesajiliwa na sticker za rangi ya blue na nyeupe.Du!,ndivyo tunavyosomeshwa namba kumbe!.
 

Attachments

  • IMG_20160726_064951[1].jpg
    IMG_20160726_064951[1].jpg
    195.2 KB · Views: 62
  • IMG_20160726_065004[1].jpg
    IMG_20160726_065004[1].jpg
    221.7 KB · Views: 62
  • IMG_20160726_065017[1].jpg
    IMG_20160726_065017[1].jpg
    236.3 KB · Views: 59
Back
Top Bottom