Engineer aliyejenga uwanja wa ndege Mwanza

kukumdogo

JF-Expert Member
Feb 1, 2011
2,866
2,746
Mabibi na mabwana mkandarasi aliyejenga uwanja wa mwanza ni Engineer Omary Chambo ambaye kwa sasa ndio katibu mkuu wizara ya uchukuzi. Wakaguzi kutoka TCAA walisema toka mwanzo kuwa uwanja upo chini ya kiwango na Engineer achukuliwe hatua ila hakuna chochote kilichochukuliwa. Kwahiyo mtu wa kuwajibika ni Eng Omari Chambo katibu mkuu uchukuzi.
 
Hili swali nilikuwa najiuliza sana tu, wakati wanajenga alikuwa ni consultant engineer au project engineer?
 
Alaumiwe kwa lipi je design yake i mean including calculation and his structural drawings are they wrong?or below standard?what exactly was his position?sometimes engineers work is professiònaly perfect but what are the qualifications of the executors meaning the contractor?unafikiri kwa mfano majengo yakianguka kosa ni engineer sa ingne sio?nipe vigezo toka kwa wahandisi wengine vya kumuwajibisha,je board ya engineers walikuwa wapi?
 
Kwenye ujenzi kuna mkandarasi-contractor,
mhandisi-engineer,embu tupe team kamili ya project,
 
Mabibi na mabwana mkandarasi aliyejenga uwanja wa mwanza ni Engineer Omary Chambo ambaye kwa sasa ndio katibu mkuu wizara ya uchukuzi. Wakaguzi kutoka TCAA walisema toka mwanzo kuwa uwanja upo chini ya kiwango na Engineer achukuliwe hatua ila hakuna chochote kilichochukuliwa. Kwahiyo mtu wa kuwajibika ni Eng Omari Chambo katibu mkuu uchukuzi.

MHANDISI ALIYEBORONGA UWANJA WA NDEGE MZ (marekebisho makubwa ya mara ya mwisho)=KATIBU MKUU WIZARA YA UJENZI!

Nani ataweza kufunga kengele katika shingo (hata walau mkia) wa PAKA BAUNSA? Hii ni muendelezo wa yale ambayo ishakuwa kama wimbo nambari 1 katika chati ya radio zote za FM:-(
 
Wakati Ndege ya ATCL iliposerereka Mwanza Airport, sababu kubwa ilikuwa ni kutuama kwa maji kwenye runway, ambapo wazi kabisa hilo ni kosa la Engineer aliyefanya ukarabati na si makosa ya design!...si rahisi makosa ya kwenye design yakapitiliza na kuwa approved hadi stage ya ujenzi, maana levels zitakataa na hivyo physical working itakataa.

Kuhusu consultant, mara nyingi watu hawa wanaweza kumezwa na nguvu ya pesa ya contractor, na hivyo hata client
(mwenye kazi) hatajua kilichofanyika, especially kama hayuko makini.

Chambo alipofika Mwanza baada ya kuambiwa sababu ya kuserereka ndege alikuwa mkali sana na akabisha mno, na akasema sababu hiyo iwe ruled out haraka sana, na alitishia kuwafukuza baadhi ya watu kazi kama wangeendelea kushupalia kuwa kutuama kwa maji ndiyo sababu ya ajali ile!

bAHATI MBAYA au nzuri mambo ya ndege ni ya taaluma, na taarifa za blackbox zilithibitisha kuwa ajali hiyo ni mserereko wa tyres kutokana na uwepo wa maji!
Chambo na kampuni yake wanahusika moja kwa moja na ubovu wa Kiwanja cha MWANZA, HILI halina kujificha!

Shida inakuja kwamba nani atamfunga paka kengele?
System nzima imeoza, wakimwaga mboga anamwaga ugali!
Uzuri ni kwamba PINDA mwenyewe jAna alikaa masaa zaidi ya 6 mwanza KWA KUKWAMA KUTOKANA NA UWANJA KUJAA MAJI!
Nilifurahi sana kuona naye anasota kama sisi!
 
Nilishangaa siku moja niliposhuhudia mfanyakazi moja wa airport akitangaza bila kipaza sauti,alikuwa anawafuata abiria kwenye viti vyao
 
Mahali ulipojengwa uwanja wa ndege wa Mwanza ni eneo la bonde na mkondo wa maji, ambapo mvua ikinyesha mwanza maji toka maeneo tofauti hutumia uwanja ule kama mkondo kuelekea ziwani.
 
Mahali ulipojengwa uwanja wa ndege wa Mwanza ni eneo la bonde na mkondo wa maji, ambapo mvua ikinyesha mwanza maji toka maeneo tofauti hutumia uwanja ule kama mkondo kuelekea ziwani.
Mkuu,
Design ilitakiwa kuona hilo tangu mwanzo, maana feature hiyo haijatokeza mwaka jana, ipo tangu dahari.
Kwanini ukarabati mkubwa uliofanywa haukusolve suala hilo?
Mkuu, kuna viwanja vilivyojengwa kwenye basin, baharini, kwenye swamps etc, lakini viko efficient mbaya kabisa, kama ni matatizo wanayo ya aina tofauti, na si yanayohusiana na maji!
 
Wakati sisi tunashindwa kudhibiti maji ya mvua tu, hebu ANGALIA KIWANJA HIKI kwa wen.zetu!
Shida ni hii ya wakubwa wanaojiona wako juu ya sheria......Senzi kabisa!
airports-10-500x375-0210-lg.jpg
 
There are reasons why people need to declare interest before participating in issues...HUYU Mgosi ilibidi afanye hivyo badala ya kujaribu kutoa maamuzi ambayo itaonekana ameyafanya kujilinda. Wandugu hivi huozo huu tutaendelea nao mpaka lini? Mkandarasi awa katibu mkuu wa wizara...hivi kweli verting ipo?
 
Engineering ina majibu ya uhakiki kila sehemu. Tatizo liliopo si Omari chambo au wahandisi bali ni mfumo. Hata ungekuwa na wahandisi wazuri kutoka Japani , kama atufanyi kazi zetu kwa moyo na uaminifu ni bure. Kama supervisor atafanya tofauti na kibarua wa mwisho nae atafanya tofauti. Hapa tatizo sio mhandisi ni sisi wote. Anzia kwako mwenye na baadae uende kwa Chambo. Wangapi wakiskia sement za za wizi wanakimbilia hata kama wanajua ni za kujengea shule au daraja la yeye kupita na gari lake! Ndio kwanza anauliza . Atuwezi kupata zaidi? Aibu kwetu wote. WOTE TUWAJIBIKE.
 
Nilishangaa siku moja niliposhuhudia mfanyakazi moja wa airport akitangaza bila kipaza sauti,alikuwa anawafuata abiria kwenye viti vyao

Endelea kushangaa maana hata Jana nilipita pale kabla ya hiyo mvua wanayosema ilimkwamisha pinda. Nilishangaa kuona mtu anataarifu abiria kuwa abiria wanapsafiri na ndege namba ...... kuelekea .... waende kupanda ndege. Bahati nzuri au mbaya watu walioenda walikuwa wachache compred na expectation zake hivyo ilimlazimu kuzunguka na kwenda toilet huku anatangaza ili walau kama kuna mtu asikie asiachwe. Ilinishangaza na kunisikitisha. Kumbe hiyo nayo ni ya siku nyingi!! Tanzania zaidi ya uijuavyo. Labda wanaogopa kuhatarisha amani kwa kununua na kufunga vipaza sauti.
 
Mahali ulipojengwa uwanja wa ndege wa Mwanza ni eneo la bonde na mkondo wa maji, ambapo mvua ikinyesha mwanza maji toka maeneo tofauti hutumia uwanja ule kama mkondo kuelekea ziwani.

Hapo siyo design lakini hapakufanyika tathmini ya athari ya mazingira. Ingefanyika EIA basi wangeligundua hilo.
 
That Mwanza airport is one of our biggest shame when it comes to airports. Eti airport ya jiji/City mtangazaji sometimes hana hata mic. Damn it, kuwa raia wa hii nchi kazi kwelikweli, na hizi scandals zote yani presha ni ya kugusa tu!
 
PakaJmmy hao unaowashangaa walifanya EIA kwanza, wakaplan ni aina gani ya mitigation measures zinahitajika na baadae ndio ukajengwa uwanja.

Huo wa Mwanza ulijengwa lini? Na kosa halipo kwenye uwanja tu hata mfano yale majumba ya serikali yaliyojengwa Dodoma hayakufanyiwa EIA na inasemekana eneo lile linakaa maji.
 
hapa ndio tunapokosea tunazungumzia tatizo lililopo,usitake kumuokoa.ametugharimu.tutatumia fedha nyingine za walipa kodi hasa wafanya kazi wa nchi hii wanaumia sana na hizi kodi zinazochezewa hovyo.mwaka 2008 niliongea na mfanyakazi mmoja wa TRA aliniambia,mfanya kazi mwenye mshahara wa 1.5 mil analipa kodi zaidi ya 275,000/= kwa mwezi ambayo ni zaidi ya 3mil per year, na mfanya biashara mwenye turn over ya 10mil per month analipa kodi 275,000/= kwamwaka.Hapo ndio utaona uchungu wa kodi kama wewe ni mfanya kazi kama mimi.Tusiwe tunatetea ujinga,dawa ni kufukuza wanaoharibu na ndipo wengine pia watajifunza.lakini ikibaki hivi wengine nao wanaiga.
 
Back
Top Bottom