Mpatanishi
JF-Expert Member
- Jul 1, 2011
- 1,810
- 623
Kwako Eng. Nsiande.
Pole na kazi.
Binafsi napenda uniweke sawa jambo hili linalonitatiza.
Ni muda mrefu sasa wananchi wa sehemu mbali mbali wanalalamika kwa mgao wa umeme.
Wakazi wa Mwanza na Arusha wamekua wakilalamika sana kuwa wanapewa mgao mkali zaidi kwa kuwa tu wanaongozwa na wabunge wa upinzani. Na wa Dar kama Kawe na Ubungo nao ni hivyo hivyo.
Wakati huohuo nikapata taarifa kuwa Tanga hawana kabisa mgao wa umeme. Mwanzoni sikuamini ila kwa likizo yangu ya mwaka huu nimeamua kuja Tanga na kweli nimedhibitisha kuwa hakuna mgao wa umeme, nipo huku kwa mwezi mmoja sasa, umeme haukatiki si mchana si usiku, nimetembea majimbo yote ya mkoa huu na wakazi wameniambia hawana mgao wa umeme tangu mwezi April.
Je ni kweli kuwa Mkoa mzima wa Tanga hakuna mgao kutokana na kuongozwa majimbo yote nane na wabunge wote wa CCM??
Je ni kweli kwamba mgao mkali umeme Mwanza, Arusha, Ubungo, Kawe n.k ni kutokana na wao kuongozwa na wabunge wa Chadema?!
Niweke sawa Mkuu.
Pole na kazi.
Binafsi napenda uniweke sawa jambo hili linalonitatiza.
Ni muda mrefu sasa wananchi wa sehemu mbali mbali wanalalamika kwa mgao wa umeme.
Wakazi wa Mwanza na Arusha wamekua wakilalamika sana kuwa wanapewa mgao mkali zaidi kwa kuwa tu wanaongozwa na wabunge wa upinzani. Na wa Dar kama Kawe na Ubungo nao ni hivyo hivyo.
Wakati huohuo nikapata taarifa kuwa Tanga hawana kabisa mgao wa umeme. Mwanzoni sikuamini ila kwa likizo yangu ya mwaka huu nimeamua kuja Tanga na kweli nimedhibitisha kuwa hakuna mgao wa umeme, nipo huku kwa mwezi mmoja sasa, umeme haukatiki si mchana si usiku, nimetembea majimbo yote ya mkoa huu na wakazi wameniambia hawana mgao wa umeme tangu mwezi April.
Je ni kweli kuwa Mkoa mzima wa Tanga hakuna mgao kutokana na kuongozwa majimbo yote nane na wabunge wote wa CCM??
Je ni kweli kwamba mgao mkali umeme Mwanza, Arusha, Ubungo, Kawe n.k ni kutokana na wao kuongozwa na wabunge wa Chadema?!
Niweke sawa Mkuu.