EMS Posta kuna nini wanaJF?

RedDevil

JF-Expert Member
Apr 30, 2009
2,367
1,519
WanaJF, Juzi kuna jamaa yangu katuma mzigo wake kwa mke wake kupitia EMS services na kulipia hela kibao kutoka huku ughaibuni. Mzigo umefika, mwenye kuupokea kapigiwa simu aende akachukue mzigo, alipofika pale ofisi za EMS kaambiwa alipe fedha za clearance ya hicho kifurushi, huyo bwana aliyeenda kuchukua mzigo basi akashtukia dili akakomaa hadi wakampa bila malipo yeyote.

Zamu imekuja kwangu, nimetuma mzigo kwa mchumba wangu kutoka huku ughaibuni, kama kawaida nikalipa pesa nyingi zaidi ya thamani ya mzigo, nikautuma. Cha ajabu mzigo ulifika mapema lakini hawakupiga simu hadi mimi mwenyewe nimetrack mzigo na kupata taarifa kuwa mzigo umemiss delivery. Cha ajabu kaenda kuulizia mzigo anaambiwa alipe Tsh 15900 kwa ajili ya kuhifadhia huomzigo. Ikabidi alipe baada ya kuanza kubishana kwa muda, lakini kabla ya hapo nilishawahi kutuma mizigo kibao na kupokelewa bila malipo ya ziada.

Ndugu zangu, najiuliza kuna nini siku hizi EMS - Posta au ndo ufisadi? naombeni mnisaidie kunielewesha maana hapa nawashangaa EMS badala ya kumbembeleza wateja,wao wanasema hata usipokuja.
 
Tatizo letu watanzania tunakata tawi tulilokalia. Shirika la Posta lina hali mbaya sana kiuchumi, ungetarajiwa wafanyakazi wawe na bidii na kujituma na kwa uaminifu, lakini wapi, kila mtu anataka kuchukua chake mapema. Shirika likifa watu waanza kupiga miayo majumbani.
 
RedDevil nafikiri hapa kuna haja ya kuwekana sawa, kwani kama mzigo uko subject to custom duty & vat hapo ni lazima mtumiwa alipe na mara nyingi ni vitu zaidi ya barua. Maana hata customs wanakitengo chao posta kwa ajili ya kuweza kujua ni mzigo gani utozwe kodi kabla ya kuchukuliwa.
 
Mkuu Bihashara huria......angalia makampuni mengine zaidi ya hiyo EMS,Few to name;-FedEX,UPS,DHL
Kati ya hayo niliokutajia mawili nilishayatumia yako serious sana na kazi...hakuna mizinguo kabisa.
 
Mkuu Bihashara huria......angalia makampuni mengine zaidi ya hiyo EMS,Few to name;-FedEX,UPS,DHL
Kati ya hayo niliokutajia mawili nilishayatumia yako serious sana na kazi...hakuna mizinguo kabisa.
Ushauri wako ndio dawa na jibu halisi kwa RedDevil. Asante maana hata mie ningempa jibu hili hili.
 
RedDevil nafikiri hapa kuna haja ya kuwekana sawa, kwani kama mzigo uko subject to custom duty & vat hapo ni lazima mtumiwa alipe na mara nyingi ni vitu zaidi ya barua. Maana hata customs wanakitengo chao posta kwa ajili ya kuweza kujua ni mzigo gani utozwe kodi kabla ya kuchukuliwa.

Mkuu nimekupata, nilituma handbag na nguo 2 basi!
 
Pole mdau, kila mbuzi anakula kwa urefu wa kamba yake

PayGod, Thanx! Hii style huwezi kuamini hata Uhamiaji kunanuka rushwa ile mbaya. Mdogo wangu kaenda kufuatilia passport kazenguliwa hadi katangaza dau fasta kaambiwa aende kuchukua ndani ya siku tatu!! Yaani hapo ndo nachoka wadau!
 
Ushauri wako ndio dawa na jibu halisi kwa RedDevil. Asante maana hata mie ningempa jibu hili hili.

Mkuu kuna jamaa alikuwa anataka kutuma simu kutoka UK je njia gani hasa rahisi katika hizo kampuni hapo??maana nimesikia hawa DHL wanaiba sana je kuna njia yoyote ambayo anaweza kutuma na mzigo ukafika bila tatizo kabisa??Msaada please kama itawezekana
 
Mkuu kuna jamaa alikuwa anataka kutuma simu kutoka UK je njia gani hasa rahisi katika hizo kampuni hapo??maana nimesikia hawa DHL wanaiba sana je kuna njia yoyote ambayo anaweza kutuma na mzigo ukafika bila tatizo kabisa??Msaada please kama itawezekana

Hapana DHL hawaibi mkuu, si kweli lakini wako strict kabisa kuhakikisha wanakupitisha TRA usurubiwe. EMS si wabaya kihivyo lakini uzuri wao wanaweza wasikupitishe kwenye suruba za TRA kama uki plea
 
Hapana DHL hawaibi mkuu, si kweli lakini wako strict kabisa kuhakikisha wanakupitisha TRA usurubiwe. EMS si wabaya kihivyo lakini uzuri wao wanaweza wasikupitishe kwenye suruba za TRA kama uki plea

Asante sana kwa majibu yako nashukuru sana mkuu wangu, sasa hapo bora kutumia njia gani hasa??Na kitu kama simu charge zake zinaweza kuwa ndefu sana??maana kuna thread humu nimeona jamaa wanasema DHL wanachukua mizigo halafu wanasingizia sijui wamemtafuta mpokeaji hajapokea mzigo umepelekwa sijui Customs wenyewe wanaita. Sasa hapa njia rahisi ni ipi??
 
Asante sana kwa majibu yako nashukuru sana mkuu wangu, sasa hapo bora kutumia njia gani hasa??Na kitu kama simu charge zake zinaweza kuwa ndefu sana??maana kuna thread humu nimeona jamaa wanasema DHL wanachukua mizigo halafu wanasingizia sijui wamemtafuta mpokeaji hajapokea mzigo umepelekwa sijui Customs wenyewe wanaita. Sasa hapa njia rahisi ni ipi??

Tumia posta tu upande wa parcel hakuna tatizo lolote mwaka wa nane sasa natumia njia hii na kila baada ya wiki chache natuma kitu Tz..cost ni ndogo sana toka hapa dubai kilo ni kama tsh 40,000 na inachukua wiki mbili...huko lazima ulipe pesa kidogo ya ushuru
 
Tumia posta tu upande wa parcel hakuna tatizo lolote mwaka wa nane sasa natumia njia hii na kila baada ya wiki chache natuma kitu Tz..cost ni ndogo sana toka hapa dubai kilo ni kama tsh 40,000 na inachukua wiki mbili...huko lazima ulipe pesa kidogo ya ushuru

Asante sana mkuu, ila hawa watu wa posta wana limit fulani hivi, maana nawasema parcel ikizidi limit yao huwa hawapendi kusafirisha hasa kwa Africa maana wanapata sana malalamiko watu wanaibiwa...Sasa kwa hapo ushauri gani hasa utakuwamzuri??
 
Asante sana mkuu, ila hawa watu wa posta wana limit fulani hivi, maana nawasema parcel ikizidi limit yao huwa hawapendi kusafirisha hasa kwa Africa maana wanapata sana malalamiko watu wanaibiwa...Sasa kwa hapo ushauri gani hasa utakuwamzuri??
Limit iliyopo ni uzito tu,max ni 30kg..wizi sijui unatokea wapi maana unapotuma mzigo wako unaandika vyote vilivyomo,wengine wanamashaka mizigo yao inapofunguliwa,ni lazima ifunguliwe ili watu wa mapato wathaminishe kodi,binafsi sijawaipoteza mzigo
 
Limit iliyopo ni uzito tu,max ni 30kg..wizi sijui unatokea wapi maana unapotuma mzigo wako unaandika vyote vilivyomo,wengine wanamashaka mizigo yao inapofunguliwa,ni lazima ifunguliwe ili watu wa mapato wathaminishe kodi,binafsi sijawaipoteza mzigo

Sawa sawa mkuu wangu na nashukuru sana kwa msaada wako, nitajaribu kupitia then nione itakuwaje.hamna tatizo kama ni hivyo.
 
maximum weight ni kg 30 kwa ndege, kama una zaidi ya kg 30 inabidi utenganishe vifurushi viwili. Parcel post wanajitahidi sana na siku hizi wana trace na track.
 
Limit iliyopo ni uzito tu,max ni 30kg..wizi sijui unatokea wapi maana unapotuma mzigo wako unaandika vyote vilivyomo,wengine wanamashaka mizigo yao inapofunguliwa,ni lazima ifunguliwe ili watu wa mapato wathaminishe kodi,binafsi sijawaipoteza mzigo
kufunguliwa ni wajibu wa Customs dept kujua kama vinavyoingia ni nlegal na kama havistahili kutozwa ushuru. ukitumiwa laptops au computers hutozwi ushuru. ukitumiwa nguo mtumba utatozwa ushuru. ukitumiwa perfumes utatozwa ushuru. wana discourage uingizaji wa vitu "luxurious"
 
kufunguliwa ni wajibu wa Customs dept kujua kama vinavyoingia ni nlegal na kama havistahili kutozwa ushuru. ukitumiwa laptops au computers hutozwi ushuru. ukitumiwa nguo mtumba utatozwa ushuru. ukitumiwa perfumes utatozwa ushuru. wana discourage uingizaji wa vitu "luxurious"
EMS juzi hapa walinivuruga khaaa nilitumiwa pump ya kukamulia maziwa ya kunyonyesha ilivyoletwa mezani wakaniuliza unajua imenunuliwa kiasi gani nikawaambia nafikiri dolla 100 ..akanijibu mbona hapa imeandikwa usd400 nikamwambia sawa tunafanyaje..ooh unatakiwa ulipe ushuru nikamjibu sawa akaanza kunipigia mahesabu khaa ananiambia kalipe pale laki350000 nilichoka yani ushuru 50%!!hamu ya pump yote iliniisha mmh
 
ndugu SIERA WALIOKUTUMIA MZG ndio wamekuangusha. why wameandika 400usd wakati wangeweza kuandika hata 50usd.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom