........... [B said:Angepatikana mtu kama Mh.Dr.Slaa atie miguu Arumeru mashariki.[/B]:lol:
natabiri ushindani ni kati ya e.kaaya na j.nassari.nassari ana kazi ya kuwashawishi wazee wa kimeru.Huyu bwana ni kweli anautamani huo ubunge ila wameru walikuwa na mahanjam nae 2005 mamvi akamtaka a2lie ila kwa sasa amefutika huko Milima na aliyesababisha akasahaulika ni Samwel Nassary,TUTAFURAHI AKIPITISHWA magamba wakione.
Namfahamu Elishilia Kaaya tangu akiwa KKKT makao makuu kama Naibu Katibu Mkuu (Utawala na Fedha).Ni mchapa kazi hodari,mwanahabari mzuri aliyebobea katika mashairi ya kidhungu ukibahatika kulisoma gazeti la Arusha Times utakutana na mashairi yake.Ni mtunzi wa kitabu cha mashairi "The Bleeding Heart and Other poems" ambacho kimeidhinishwa na wizara ya elimu kutumiwa na wanafunzi wa kidato cha tano & sita mchepuo wa literature.
Bwana Kaaya alijiunga na AICC kama meneja wa fedha na baadae akapanda cheo hadi mkurugenzi wa fedha na hatimaye mkurugenzi mkuu.Mchango wake ni mdogo sana ukimlinganissha na wakurugenzi waliomtangulia kama Sammy Mdee ambaye alikifanya kituo cha mikutano cha AICC kujulikana sehemu kubwa ya dunia mikutano mikubwa enzi za Mdee imeyeyuka kabisa siku hizi mikutano ya ndani kama NSSF,CCM,EUWRA,NBAA ndiyo inayotgemewa.
Bwana Kaaya ni mjumbe wa Halmashauri kuu taifa CCM nafasi hii ameipata kupitia mlango wa nyuma.Ikumbukwe mkoa wa Arusha nafasi ya ujumbe ilikuwa ikigombewa na Elisa Mollel na Mwenyekiti wa mkoa Mzee Lekule Laiser wapinzani wa maslahi ya Laigwani Lowassa.Lowassa alitumia nafasi yake ya uwaziri mkuu wakati huo kuwazushia kashfa ya rushwaa na hatimaye alifanikiwa kuwaondoa kwenye mpambano wa kuwania nafasi hizo.Elishilia Kaaya chaguo la Lowassa akazawadiwa nafasi ya ujumbe kwaajili ya kulinda maslahi ya Laigwanani Lowassa.
Kama unayosema ni ya kweli wameperform sana kwanini anataka kuacha fani yake kukimbilia siasa?
kama unayosema ni ya kweli wameperform sana kwanini anataka kuacha fani yake kukimbilia siasa?
siasa ni kila kitu ndugu asikudanganye mtu
hiyo cha mtoto alipiga fedha ya uhakika katika ukarabati wa ukumbi mkubwa wa aicc wa simba kwa ajili ya maandalizi ya mkutano wa sullvan yaani hakuna ukumbi mbovu duniani kama huo ukikaa kiti cha katikati ili kutoka ili ukajisaidie lazima watu wote msimame ni kama ukumbi wa sinema jamaa hapo alipiga fedha iliyosimama
Wewe uliyajuaje haya????
Unatafuta umbeya ? Kuna mpya ya mradi wa nyumba za fire jamaa kabiga nyingine