Wasomi wanatakiwa wawe wavumbuzi na wajenzi wa uchumi, kwa mfano ukisoma jinsi ndege ilivyovumbuliwa utashangaa, ilianza mwaka 1799-1913. Kila mvumbuzi alikuwa anajitahidi kufanya kitu, anakata tamaa lakini anaacha kijitabu cha theory zake. Kufikia mwaka 1913 wright brothers walipitia vitabu vyote na matokeo yake ni mafanikio ya binadamu kutumia usafiri wa anga. Elimu ya vitendo ndio matokea ya wenzetu kupiga hatua katika nyanja mbalimbali, silaha za kisasa za kivita, vyanzo vya umeme, haya magari ya kifahari tunayotamba nayo, yote ni matokeo ya wasomi waliotumia elimu yao katika vitendo.
Sisi watanzania hatuna cha kujivunia kwa hawa wasomi wetu wanaoringa kwa kuvaa majoho, hatuoni impact yoyote kwenye jamii kutokana na usomi wao. Kwa mfano mtu amesota hapo UDSM amepata hadi PhD, huyu mtu atatafuta wahisani(donors) atafanya research ambayo haina faida kwa nchi yake bali kwa hao wahisani(kuganga njaa), ni hawa hawa wasomi ndio wamedidimiza mashirika yetu(hawana uzalendo hata kidogo, wamejaa ujinga wakujipatia hela kwa hila na uwizi). Angalia taasisi za serikali watu wamejazana mle, hakuna anaeweza kumkemea mwenzake, kwenye akili zao kumejaa michongo michongo, kutunga safari kwa ajili ya kujipatia perdiem. Kwao kipimo cha mafanikio ni kupata hela za ujanja ujanja, kwenye nyuso zao kumejaa usanii mtupu, ukiwa na bidii ya kazi wataku kejeli na hata kukufanyia hila. Kwenye kundi la hawa watu huruhusiwi kuboresha. Utaambiwa hujafuata utaratibu, subiri kwanza hadi tufanye kikao, na kama hujafanyiwa hila basi utaonewa huruma kwa kufanya kazi kwa bidii, wajisemea aaah huyu mbona anajitesa hivi.
Hii ndio Tanzania yetu.
Sisi watanzania hatuna cha kujivunia kwa hawa wasomi wetu wanaoringa kwa kuvaa majoho, hatuoni impact yoyote kwenye jamii kutokana na usomi wao. Kwa mfano mtu amesota hapo UDSM amepata hadi PhD, huyu mtu atatafuta wahisani(donors) atafanya research ambayo haina faida kwa nchi yake bali kwa hao wahisani(kuganga njaa), ni hawa hawa wasomi ndio wamedidimiza mashirika yetu(hawana uzalendo hata kidogo, wamejaa ujinga wakujipatia hela kwa hila na uwizi). Angalia taasisi za serikali watu wamejazana mle, hakuna anaeweza kumkemea mwenzake, kwenye akili zao kumejaa michongo michongo, kutunga safari kwa ajili ya kujipatia perdiem. Kwao kipimo cha mafanikio ni kupata hela za ujanja ujanja, kwenye nyuso zao kumejaa usanii mtupu, ukiwa na bidii ya kazi wataku kejeli na hata kukufanyia hila. Kwenye kundi la hawa watu huruhusiwi kuboresha. Utaambiwa hujafuata utaratibu, subiri kwanza hadi tufanye kikao, na kama hujafanyiwa hila basi utaonewa huruma kwa kufanya kazi kwa bidii, wajisemea aaah huyu mbona anajitesa hivi.
Hii ndio Tanzania yetu.