Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,828
Nimesoma kwa shida na taabu nyingi, misukosuko na dhoruba ndizo zinazo endelea kunisonga tangu nikiwa mdogo, labda rabsha hizo kwa kizungu ndio huitwa challenges.
Mtaa ninaoishi ni wa hali ya chini, namshukuru Mwenyezi Mungu nilisha wahi kuvaa joho na kikofia, pia kushikana mkono no rais kwenye mahafali (majaoho huvaliwa hata kwenye graduu za chekechea, lakini wahadhiri hawahudhurii)
Sipendi watoto wa leo wapite mapito niliyopitia, kwa hiari nimeamua kuwa MWALIMU WA HIARI MTAANI.
Kama mjuavyo, maduka ya Uswahilini kama sio la Mpemba basi ni la Mchaggah.
Leo nilikuwa nikimuuliza mtoto wa Mchagga muuza duka hesabu za mara a.k.a tebo a.k.a hesabu za kuzidisha.
Baba na mama muuza duka wakanijia juu, kwa nini namuuliza mtoto wao maswali wakati sichangii katika ada wala hela ya daftari?
Nimeporomoshewa matusi hadi nimekoma, sijui ni wapi tunalipeka hili taifa.
Wazazi wamewaka eti naringia degree yangu, wamesema degree yangu ni ya kuunga unga, sijui kusoma wala kuandika.
Wanajinadi hili taifa limeuzwa kwa wenye hela, ukiwa na hela unafanya utakalo.
Waweza kununua cheti kuanzia cha msingi hadi cha chuo , hata kama mwanao hajui kusoma wala kuandika.
Kwenye udhia penyeza rupia.
Baada ya kusikia maneno hayo nikasikia kuzimia.
Hakika Elimu na mwamko wangu wa kuelimisha jamii vimeniponza mtaani.
Mtaa ninaoishi ni wa hali ya chini, namshukuru Mwenyezi Mungu nilisha wahi kuvaa joho na kikofia, pia kushikana mkono no rais kwenye mahafali (majaoho huvaliwa hata kwenye graduu za chekechea, lakini wahadhiri hawahudhurii)
Sipendi watoto wa leo wapite mapito niliyopitia, kwa hiari nimeamua kuwa MWALIMU WA HIARI MTAANI.
Kama mjuavyo, maduka ya Uswahilini kama sio la Mpemba basi ni la Mchaggah.
Leo nilikuwa nikimuuliza mtoto wa Mchagga muuza duka hesabu za mara a.k.a tebo a.k.a hesabu za kuzidisha.
Baba na mama muuza duka wakanijia juu, kwa nini namuuliza mtoto wao maswali wakati sichangii katika ada wala hela ya daftari?
Nimeporomoshewa matusi hadi nimekoma, sijui ni wapi tunalipeka hili taifa.
Wazazi wamewaka eti naringia degree yangu, wamesema degree yangu ni ya kuunga unga, sijui kusoma wala kuandika.
Wanajinadi hili taifa limeuzwa kwa wenye hela, ukiwa na hela unafanya utakalo.
Waweza kununua cheti kuanzia cha msingi hadi cha chuo , hata kama mwanao hajui kusoma wala kuandika.
Kwenye udhia penyeza rupia.
Baada ya kusikia maneno hayo nikasikia kuzimia.
Hakika Elimu na mwamko wangu wa kuelimisha jamii vimeniponza mtaani.