Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,570
- 19,442
Katika wiki hii nitakuwa nyumbani full time kuanzia tarehe 24 Dec 2010 hadi tarehe 4 January 2011 kama mwenyezi mungu atanifikisha huko. Nimeamua kutumia muda huo kutumia thread hii kuandika somo la uraia kuhusu Katiba ya Tanzania na kuchambua udhaifu wake. Ingawa wengi wetu tunaijua Katiba yetu, kuna idadi kubwa ambao hawaijui sawasawa na hivyo kutokuelewa ulazima wa Tanzania kuwa na Katiba mpya.
Ninaomba mod asiunganishe thread hii na nyingine kusudi niweze kuwa na mtililiko mzuri wa mawazo.
Katiba inayotumika Tanzania iliandikwa mwaka 1977 na kufanyiwa marekebisho madogo kulingana na mabadiliko ya kisiasa kutoka chama kimoja hadi vyama vingi ambayo yote yalijumuishwa katika toleo la mwaka 2000. Ingawa kuna toleo la kiingereza la katiba hiyo, toleo kuu ni lile la kiswahili, kwa hiyo kukiwa na masigishano ya lugha kati ya toleo la kiswahili na kiingereza, basi lile la kiswahili linatawala.
katiba hiyo imegawanyika katika sura 10 zenye jumla ya ibara 152. Katiba ya Tanzania imaongelea karibu mambo yote ya muhimu kuwamo kwenye katiba na vile vile imejumuisha na mambo mengine ambayo siyo ya muhimu kuwamo kwenye Katiba.
Kabla ya kuanza kuangalia udhaifu wa ibara mbalimbali za Katiba, nitaanza na ule udhaifu wa jumla katika uandishi wa Katiba Yenyewe
Udhaifu wa Kwanza kabisa wa jumla katika uandishi wa katiba ya tanzania ni ule muundo wake; imeandikwa kwa mtindo wa kuzunguka zunguka kama vile ni kwa ajili ya wanasheria tu badala ya kuandikwa ikiwa imenyooka kwa ajili ya kusomwa na kueleweka na raia wote. Kwa mfano, ibara ya 2(2) inazungumzuia jambo linalohusu Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar bila kuwa imeelezea serikali hizo ni vitu gani. Inabidi mtu arukie ibara ya 151 kujua serikali hizo ni vitu gani.
Katika hizo ibara 152 za Katiba yetu kuna ibara ambazo hazina kitu kutokana na kuwa zilishafutwa lakini zimetunza namba zake; kwa mfano, ibara ya 10, 80, na 82. Kama ibara hizi zilishafutwa, hakuna umuhimu wa kuendelea kuziorodhoseha huku zikiwa tupu.
Ninaomba mod asiunganishe thread hii na nyingine kusudi niweze kuwa na mtililiko mzuri wa mawazo.
Katiba inayotumika Tanzania iliandikwa mwaka 1977 na kufanyiwa marekebisho madogo kulingana na mabadiliko ya kisiasa kutoka chama kimoja hadi vyama vingi ambayo yote yalijumuishwa katika toleo la mwaka 2000. Ingawa kuna toleo la kiingereza la katiba hiyo, toleo kuu ni lile la kiswahili, kwa hiyo kukiwa na masigishano ya lugha kati ya toleo la kiswahili na kiingereza, basi lile la kiswahili linatawala.
katiba hiyo imegawanyika katika sura 10 zenye jumla ya ibara 152. Katiba ya Tanzania imaongelea karibu mambo yote ya muhimu kuwamo kwenye katiba na vile vile imejumuisha na mambo mengine ambayo siyo ya muhimu kuwamo kwenye Katiba.
Kabla ya kuanza kuangalia udhaifu wa ibara mbalimbali za Katiba, nitaanza na ule udhaifu wa jumla katika uandishi wa Katiba Yenyewe
Udhaifu wa Kwanza kabisa wa jumla katika uandishi wa katiba ya tanzania ni ule muundo wake; imeandikwa kwa mtindo wa kuzunguka zunguka kama vile ni kwa ajili ya wanasheria tu badala ya kuandikwa ikiwa imenyooka kwa ajili ya kusomwa na kueleweka na raia wote. Kwa mfano, ibara ya 2(2) inazungumzuia jambo linalohusu Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar bila kuwa imeelezea serikali hizo ni vitu gani. Inabidi mtu arukie ibara ya 151 kujua serikali hizo ni vitu gani.
Katika hizo ibara 152 za Katiba yetu kuna ibara ambazo hazina kitu kutokana na kuwa zilishafutwa lakini zimetunza namba zake; kwa mfano, ibara ya 10, 80, na 82. Kama ibara hizi zilishafutwa, hakuna umuhimu wa kuendelea kuziorodhoseha huku zikiwa tupu.