Elimu ya msingi kwa kiingereza inakuaje?

Shinto

JF-Expert Member
Dec 6, 2010
1,781
96
Wakuu,
Kwanza nianze kwa kutangaza "interests"! Mimi nimesoma shule za Kanumba mwanzo mwisho!.
Sasa jana nilibahatika kuona paper ya jiografia ya dogo moja anayesoma hizi shule zenu za kisasa 'english medium'.
Yeye anajiandaa kumaliza darasa la saba mwaka huu, sasa nikaona swali nikahisi alikosa kwa sababu ya 'mabomba' tu kwenye lile swali. Nikajitahidi kutafsiri, nikamuuliza kwa kiswahili swali lile lile akapatia!!!!!!!.
Kutoka hapo, nikaamini kuwa tutake tusitake kizungu ni kikwazo kwa hawa watoto. Yaani katika somo, 50% inapotezwa kwa sababu ya ugumu wa lugha, hasa ikiwa mtoto anarudi nyumbani anakoongea kiswahili au anakaa boarding za magumashi (wanazoongea kiswahili watoto wakiwa peke yao).

Swali hapa, tuifanye elimu ya iwe kiswahili tuu, au kiingereza tuu? Tukichagua hilo la pili, itabidi tuifanye kiingereza kuwa lugha ya kwanza kwa mawasiliano hata huku uswahilini!

Kwanini wale wanaozungumzia kiwango cha elimu kushuka, hawashupalii hili?

Nawasilisha!
 
Point unayo ila sio kuwa force watoto kuzungumza English kwani wazazi wengi hawafahamu Engish...issue ni kuangalia swala zima la elimu Tanzania....mother tongue and Kiswahili are major languages of our children, for some even Kiswahili is hard....ni challenge ume raise na ni lazima tuangalie namna ya kukabiliana na tatizo hilo
 
Point unayo ila sio kuwa force watoto kuzungumza English kwani wazazi wengi hawafahamu Engish...issue ni kuangalia swala zima la elimu Tanzania....mother tongue and Kiswahili are major languages of our children, for some even Kiswahili is hard....ni challenge ume raise na ni lazima tuangalie namna ya kukabiliana na tatizo hilo

Kweli mkuu,
Kinachonishangaza ni kwanini watu wenye dhamana na wanaharakati wa elimu hawaoni kama hii ni factor mojawapo inayopelekea kiwango cha elimu kushuka!
 
Back
Top Bottom