Elimu imenishinda

tizo1

JF-Expert Member
Mar 9, 2011
856
145
Naomba ushauri jaman!nimemaliza kidato cha sita HKL na nimepata DIV 4 YA 19 .je nifanye nini sasa?naomba mnisaidie.
 
Usiwe na hofu huo siyo mwisho wa maisha..tulia mwombe Mungu, He always has a plan 4u, Jeremiah 29:11...
Kuna stori nyingi sana za watu waliofeli form 6 na sasa wamefanikiwa academically and in life...wala usiwe na hofu mdogo wangu!!!
* one of the options ni kutumia vyeti vyako vya form four uanze certificate uendelee na life..
* au, kama unaona, unajua, na una uhakika kuwa imetokea kwa bahati mbaya, labda hukuwa tayari kimaandalizi, as in u r very sure...then i suggest u resit the examinations..lakini hii ni kama una uhakika wa sababu iliyokufanya upate matokeo hayo!!!
Ulikuwa shule gani mdogo wangu!??
 
Usiwe na hofu huo siyo mwisho wa maisha..tulia mwombe Mungu, He always has a plan 4u, Jeremiah 29:11...
Kuna stori nyingi sana za watu waliofeli form 6 na sasa wamefanikiwa academically and in life...wala usiwe na hofu mdogo wangu!!!
* one of the options ni kutumia vyeti vyako vya form four uanze certificate uendelee na life..
* au, kama unaona, unajua, na una uhakika kuwa imetokea kwa bahati mbaya, labda hukuwa tayari kimaandalizi, as in u r very sure...then i suggest u resit the examinations..lakini hii ni kama una uhakika wa sababu iliyokufanya upate matokeo hayo!!!
Ulikuwa shule gani mdogo wangu!??
nilikuwa kwiro high school
 
Pole Tizo1. Ukweli ni kuwa bado una nafsi kubwa sana ya mafanikio katika maisha. A-level huwa ina suprises zake na mazingira ya usomaji mara nyingi ni magumu. Miongoni mwa mambo ambayo huwa yanatatiza ni kuulizwa maswali na watu wa mtaani kuhusu matokeo yako na pia inauma pale unapoona wenzako wanaenda vyuo vya elimu ya juu na kukuacha. Hili ni jambo la kawaida.

USHAURI:

  1. Usijaribu kuzuia maumivu ya kufeli. Kwa kipindi fulani ni lazima na ni halali pia kupata maumivu. Usifanye kazi kubwa sana kujaribu kuzuia maumivu, yataisha yenyewe. Maumivu huisha kama utakuwa na altenatives. Ukishapata jibu juu ya hatua za kuchukua utashangaa ghafla maumivu yanaanza kuisha.
  2. Soma kwa hatua. Kwa kutumia cheti chako cha Form 4 unaweza kuapply vyuo vinavyotoa certificates then diploma then degree n.k. Ni sawa tulikuwa tunataka kwenda chuo kikuu, lakini matokeo hayaturuhusu. Katika mazingira kama haya tufe? Hapana maisha ni lazima yaendelee, hata kama watu watakucheka, vumilia. Katika kuchagua certificates angalia courses za mambo unayoyaweza au kuyapenda, pia ni vizuri kuangalia soko la ajira la courses hizo Tz (kama unawaza kuajiriwa).
  3. Kama unadhani umefeli kwa bahati mbaya unaweza ku-resit, japo ku-resit na kufaulu ni kitu kigumu sana. Angalia uhalisia wa uwezo wako.
Jipe moyo, maumivu ni lazima yawepo kwa muda fulani na ni lazima yaishe. Ila ni rahisi maumivu kuisha kama utajua nini hatua ya kuchukua baada ya matokeo haya. Tuko pamoja na Mungu akubariki.

NB. Kama utakuwa unahitaji ushauri wa ziada au ushauri private waweza kunitumia private message.
 
nilikuwa kwiro high school

Hakuna haja ya pole na wala usikubali yeyote akupe POLE. Panga stratergy yako upya, naamini ulikuwa una ndote, malengo, you wanted to be(come) somebody. Hebu fanya assessment kama umeharibu sana au kuna uwezekano wa ku-make up.
There's still a life for you.
Nilikuwepo ile Kwiro ya Makunja, sisi ndo tulianzisha combi za arts mahali hapo. Natumaini Mama Ngapo bado atakuwepo!
 
Pole Tizo1. Ukweli ni kuwa bado una nafsi kubwa sana ya mafanikio katika maisha. A-level huwa ina suprises zake na mazingira ya usomaji mara nyingi ni magumu. Miongoni mwa mambo ambayo huwa yanatatiza ni kuulizwa maswali na watu wa mtaani kuhusu matokeo yako na pia inauma pale unapoona wenzako wanaenda vyuo vya elimu ya juu na kukuacha. Hili ni jambo la kawaida.

USHAURI:

  1. Usijaribu kuzuia maumivu ya kufeli. Kwa kipindi fulani ni lazima na ni halali pia kupata maumivu. Usifanye kazi kubwa sana kujaribu kuzuia maumivu, yataisha yenyewe. Maumivu huisha kama utakuwa na altenatives. Ukishapata jibu juu ya hatua za kuchukua utashangaa ghafla maumivu yanaanza kuisha.
  2. Soma kwa hatua. Kwa kutumia cheti chako cha Form 4 unaweza kuapply vyuo vinavyotoa certificates then diploma then degree n.k. Ni sawa tulikuwa tunataka kwenda chuo kikuu, lakini matokeo hayaturuhusu. Katika mazingira kama haya tufe? Hapana maisha ni lazima yaendelee, hata kama watu watakucheka, vumilia. Katika kuchagua certificates angalia courses za mambo unayoyaweza au kuyapenda, pia ni vizuri kuangalia soko la ajira la courses hizo Tz (kama unawaza kuajiriwa).
  3. Kama unadhani umefeli kwa bahati mbaya unaweza ku-resit, japo ku-resit na kufaulu ni kitu kigumu sana. Angalia uhalisia wa uwezo wako.
Jipe moyo, maumivu ni lazima yawepo kwa muda fulani na ni lazima yaishe. Ila ni rahisi maumivu kuisha kama utajua nini hatua ya kuchukua baada ya matokeo haya. Tuko pamoja na Mungu akubariki.

NB. Kama utakuwa unahitaji ushauri wa ziada au ushauri private waweza kunitumia private message.
nashukuru kwa ushauri mzuri,nitaufanyia kazi.pia nta ku pm ili unijuze zaid.nimekata tamaa kabisa.ki ukwel nlikuwa fit sana'
 
Hakuna haja ya pole na wala usikubali yeyote akupe POLE. Panga stratergy yako upya, naamini ulikuwa una ndote, malengo, you wanted to be(come) somebody. Hebu fanya assessment kama umeharibu sana au kuna uwezekano wa ku-make up.
There's still a life for you.
Nilikuwepo ile Kwiro ya Makunja, sisi ndo tulianzisha combi za arts mahali hapo. Natumaini Mama Ngapo bado atakuwepo!
asante kwa ushauri.
 
we mbona hujafeli! kufeli ni kupata division 0.. kuna vyuo vingi unaweza kuapply usome remedial course then unaunga degree mwaka huu huu. fuatilia st. augustine university mdogo wangu, usikate tamaa.
 
we mbona hujafeli! kufeli ni kupata division 0.. kuna vyuo vingi unaweza kuapply usome remedial course then unaunga degree mwaka huu huu. fuatilia st. augustine university mdogo wangu, usikate tamaa.
Asante sana kwa ushaur mzuri.UMENITIA MOYO na kunipa mwanga!nilikuwa na uwezo mzuri sana!hakuna wasi ntajitahd kufanya hivyo!
 
mdogo kwanza naomba kukuambia kuwa ujaanguka bali umeteleza na "kuteleza si kuanguka" si nafasi kibao za kuendelea na elimu ya juu tafuta pre degree me najua hii iko zanzibar sijui ni chuo gani hasa,ambayo unasoma one year ukipass unaendelea na masomo yko, vile vile unaweza ukaanza ngazi ya cheti ,diploma na kufikia advance diploma. nakushauri kw wakati huu usiwe na haraka katika maamuzi yako , kuwa makini na tumia mda wako kwa kuuliza watu na kuomba ushauri, i hope utafanikiwa
 
mimi ushauri wangu usirudie mtihani... utapoteza muda, jipange tafuta mradi ... kama ni biashara usifanye ya kuuza na kununuwa, fikiria biashara ambayo ita provide service "even though inategemea na sehemu uliyopo" ..

kufeli kitu cha kawaida sana kwa elimu yetu ya bongo.

Jipange
 
asante sana TIZO1...asanteni wadau wote mliotoa ushauri wa kujenga.....hapa sasa napata faraja na maana ya kukaa JF....it is a building block, nikiwa mdau mkubwa wa elimu nashawaishika kusema dogo TIZO1 kujgundua tatizo au kushirikisha watu tatizo lako tayari umeshalitatua 50%... yaani umeshafika nusu ya jibu la tatizo lako
Shule zipo nyingi kufikia malengo yako ..japo ile njia uliyokuwa unaiona haikidhi haja!
rejea ibada kwa kasi mpya
 
Huna haja ya kujilaumu kivile, ni kweli unaokosa kufikia malengo yako unaumia, lazima kila kitu kiende mbele, Naunga mkono wote wanaosema kuwa tumia cheti chako cha fom4 (kama unahitaji kuendelkea na elimu ya juu) unaweza kuanza na dip na kama inashindikana kabisa anzia cheti. Vyuo vilivyo chini ya Nacte vinasaidia sana katika hili, vipo vingi mfano ni IFM, CBE, Mwalimu Nyerere na TIA, USTAWI,
Ningekushauri tembelea USTAWI MNMA utapata zaaidi

Halafu (SIRI YAKO) unaweza kucope na stress ulizonazo kwa kuangalia mifano ya watu walioanzia na elimu za UPE lakini leo ni madaktari, mfano mmoja ni Dr Kadeghe Maiko:A S 39:
 
Huna haja ya kujilaumu kivile, ni kweli unaokosa kufikia malengo yako unaumia, lazima kila kitu kiende mbele, Naunga mkono wote wanaosema kuwa tumia cheti chako cha fom4 (kama unahitaji kuendelkea na elimu ya juu) unaweza kuanza na dip na kama inashindikana kabisa anzia cheti. Vyuo vilivyo chini ya Nacte vinasaidia sana katika hili, vipo vingi mfano ni IFM, CBE, Mwalimu Nyerere na TIA, USTAWI,
Ningekushauri tembelea USTAWI MNMA utapata zaaidi

Halafu (SIRI YAKO) unaweza kucope na stress ulizonazo kwa kuangalia mifano ya watu walioanzia na elimu za UPE lakini leo ni madaktari, mfano mmoja ni Dr Kadeghe Maiko:A S 39:
Asante sana nazid kufarijika na wana JF nilipo wengi si wasomi na wanafikiri kufel nh uzembe!kwel hiki ni jukwaa la elimu tayari naanza kupata mwanga na kuona si mimi pekee niliyefeli maisha
 
asante sana TIZO1...asanteni wadau wote mliotoa ushauri wa kujenga.....hapa sasa napata faraja na maana ya kukaa JF....it is a building block, nikiwa mdau mkubwa wa elimu nashawaishika kusema dogo TIZO1 kujgundua tatizo au kushirikisha watu tatizo lako tayari umeshalitatua 50%... yaani umeshafika nusu ya jibu la tatizo lako
Shule zipo nyingi kufikia malengo yako ..japo ile njia uliyokuwa unaiona haikidhi haja!
rejea ibada kwa kasi mpya
asante sana angalau nimepata mwanga fulani hivi!JF ni msaada tosha jamani
 
Kufeli shule sio kufeli maisha mdogo wangu.
Unaposhindwa upande mmoja geukia upande wa pili. Tafuta shule za ufundi ujiendeleze inawezekana hiyo ndio channel ya kutokea mungu aliyokupangia.
 
asante sana TIZO1...asanteni wadau wote mliotoa ushauri wa kujenga.....hapa sasa napata faraja na maana ya kukaa JF....it is a building block, nikiwa mdau mkubwa wa elimu nashawaishika kusema dogo TIZO1 kujgundua tatizo au kushirikisha watu tatizo lako tayari umeshalitatua 50%... yaani umeshafika nusu ya jibu la tatizo lako
Shule zipo nyingi kufikia malengo yako ..japo ile njia uliyokuwa unaiona haikidhi haja!
rejea ibada kwa kasi mpya

Asante sana mkuu kwa maneno yako hapo juu. Kaka TIZO1 usikate tamaa kama wadau hapo juu walivyosema kufeli pepa sio kufeli maisha. Nakuomba jipange na kusonga mbele hata mm nakushauri usirudie pepa kwan unaweza songambele na hizo point zako cheki vyuo hapo tz, nakupiga masomo ya jioni unaunga degree kabisa.

Sasa naona bongo vijana tunabadilika kwan nilikuwa nachukia kumwambia mtu heti umefeli na walio faulu wakawa wanajiona wapo fiti kiakili lakini sio hivyo katika ulimwengu huu.

pamoja tutajenga taifa, hila vijana tubadilishe mawazo yetu. Wana JF pamoja tutapeleka taifa la tz kwenye ukurasa mpya.
 
Back
Top Bottom