EL; RA & AC Wamtunishia Misuli JK: Wagoma Kujibu Barua

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Makamda na Wakuu wa JF;

Nyeti zilizofika katika dawati la Superman zinasema wale TRIANGLE TRIPPLETS aka PEMBETATU PACHA aka RACHEL inasemekana wakekataa kujibu barua walizopewa hivi karibuni zikiwataka wajieleze kwa nini wasifukuzwe uongozi na uanaachama wa Chama Cha Magamba CCM.

Nyeti zinasema kuwa EL amesema mwenye ushahidi dhidi yake na mwenye ushahidi wa nani anapaswa kuondoka CCM kwa ufisadi aje nao na hivyo wote wamekataa katu katu kusema wala kujibu kitu.

Inasemekana kuwa ni kweli RACHEL wamekuwa na vikao vyao vya siri na mpaka sasa wamekutana mara mbili tangu watoke Dodoma kwenye vikao vya CC na NEC.

Nyeti zinasema kuwa mara baada ya Vikao vya CC. Mkuu wa Kaya alimwita EL kule Ikulu ndogo ya Chamwino Dodoma majira ya saa nane usiku na akamuuliza kuwa imekuwaje Makamu Mwenyekigoda wa Chama Cha Magamba Mh. PM akakutaja na wewe waziwazi kuwa ni FISADI na je tutafanikiwa mikakati yetu tuliyopanga huko nyuma? (NB: Hii ni Mikakati ya Boyz II Men ya EL kuwa Next pale Magogoni). Hata hivyo EL alimjibu Mkuu wa Kaya kuwa bado anatafakari kilichotokea ndani ya CC na kumwambia JK ampe muda na atarudi na jibu.

Inasemekana EL alikaa kama nusu saa na kisha akaondoka. Desk la Superman limehabarishwa kuwa EL alikwisha jua mpango wa JK wa kumtosa kwa kumzungunguka pasipo kuharibu urafiki wao. Hata hivyo hadi leo hii JK bado hajapewa jibu.

Pamoja na yote hayo RACHEL wamechukizwa zaidi na maneno ya Dogo Nape na Kada Chiligati na Mukama ambao wanaaendelea kuwapa siku 90 wajitoe au watoswe kwa kuwa eti wao ni MAFISADI.

Naye Mu-Iran RA inamesemakana kama anataka bora Jahazi sasa liingie maji na wote wazame. Yaani kama noma na iwe noma.

Kuna mengi sana yatakuja baada ya mapumziko ya Pasaka from 28th May 2011 ambacho kitakuwa na Mishindo Mkuu.

Update 1: Easter Sunday - 24th April 2011


Rais JK, leo akiongea katika Tamasha la Muziki wa Injili uliohusisha vikundi vya kwaya toka nchi mbalimbali alisema:

"Katika kushughulikia swala la mafisadi, haki itatendeka na hawatamuonea haya mtu yeyote"

Source: ITV News Bulletin of 8.00 PM


Update 2: Monday 25th April 2011:

RAIS Jakaya Kikwete amesema amepata moyo mpya wa kuendeleza kazi ya kujivua gamba na yeye na wenzake watajitahidi kuifanya kazi hiyo kwa haki bila kumwonea mtu. Alisema alitangaza tangu Februari mwaka huu kuwa CCM itajivua gamba na sasa wameanza kuifanya kazi hiyo ingawa watu wengine wameanza kumtupia lawama Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye aliyekuwepo katika tamasha hilo.

Kabla ya kutoa kauli hiyo katika Tamasha hilo la Pasaka, lililofanyika mjini Dar es Salaam, Askofu wa Kanisa la Assemblies of God Tanzania (TAG) Onesmo Ndegi, alisema hatua ya kujivua gamba inayochukuliwa na CCM chini ya Mwenyekiti wake, Rais Kikwete ina mkono wa Mungu. Askofu Ndegi alisema sherehe za Pasaka mwaka huu ni maalumu kwa kuwa ni mwaka ambao Tanzania itaadhimisha miaka 50 tangu Uhuru ambayo katika Ukristo inaitwa Jubilee na maana yake ni kuweka kitu huru ama kukiondoa katika mateso.

Alisema kutokana na hali hiyo, Mungu amempa ujasiri Rais Kikwete wa kujivua gamba, kitendo ambacho CCM ilikianza hivi karibuni kwa kuwaondoa madarakani baadhi ya viongozi wake wa juu. "Ujasiri wa Rais wetu ni ujasiri aliopewa na Mwenyezi Mungu pamoja na dua tunazomwombea, tunaomba kujivua gamba huko kuwe kwa ukweli na kusiishie hapo tu," alisema Askofu Ndegi.

Baada ya kumaliza kusema hayo, Askofu huyo aliomba maaskofu wengine waliokuwepo ukumbini kumwekea mikono Rais sehemu waliko na kumwombea dua ya kumpa ulinzi, ujasiri na hekina katika uongozi wake.

Lakini Rais Kikwete pia alisisitiza umuhimu wa kudumisha amani nchini na kuwataka wananchi kuvumiliana baina ya watu wa dini mbalimbali na kutowasikiliza watu wanaohubiri habari za udini kwa lengo la kutaka kuleta mafarakano nchini. Tamasha hilo ambalo Rais Kikwete alikuwa mgeni rasmi, lililenga kuchangisha fedha za kusaidia yatima, watu wenye ulemavu na mahitaji kwa wanawake wasiojiweza.

Source: HabariLeo


Peace and Love

Respect.

Superman.

QED
 
Kama Lowasa ameshagundua kuwa JK ana mpango wa kumtosa kwa kumzunguka na kama ni kweli JK ana mpango huo,basi ni mwanzo mzuri kwao wote JK na Lowasa na kwa Wadanganyika.Kama ulivyosema mkuu,tutaona na kusikia mengi tusiyoyatarajia katika siasa zetu katika kipindi kifupi kijacho
 
Kama Lowasa ameshagundua kuwa JK ana mpango wa kumtosa kwa kumzunguka na kama ni kweli JK ana mpango huo,basi ni mwanzo mzuri kwao wote JK na Lowasa na kwa Wadanganyika.Kama ulivyosema mkuu,tutaona na kusikia mengi tusiyoyatarajia katika siasa zetu katika kipindi kifupi kijacho

Wakuu wa JF, iko hivi:

Inasemekana kuna bomu litalipuka siku si nyingi toka kwa hawa kina RACHEL. Sasa Mzee wa Kaya anajaribu kwa kila hali kuwa karibu na EL ili kumaliza tofauti. This remains to be seen. Maana habari nyingine zinasema Wakulu Wastaafu (Mzee Ruksa & Mzee wa Uwazi na Ukweli) wamemwambia Mkuu wa kaya awatose (Mzimu wa Mwalimu bado unaishi).

Mistake aliyoifanya JK ni mwaka jana wakati wa kampeni . . . . ilikuwa awatose huko lakini sasa ni ngumu. Sasa leo anawatumia akina Nape; Chiligati na Mukama waseme ili kusudi yeye asionekane mbaya kwa hawa kina RACHEL. Pia kuna nyeti zinasema Mkuu wa Kaya yuko radhi kumtosa AC wakati wowote lakini kwa kuwa amejipachika kwa hawa jamaa wawili inakuwa ngumu.

Mzee Mzima aliambiwa wakati wa Richmond kuwa hii kampuni sio Genuine na akapewa data zote lakini EL akaenda kwa haraka sana kumsakizia Msabaha kwa sababu kuwa anacheewasha mchakato na akaingia Mkenge. JK bila hiana akamuondoa Msabaha kwenye Wizara

Kwenye EPA mpaka sasa Mkkulu amekalia Mafile mezani kwake hajayafanyia kazi na data za wezi wote anazo.

Kesi ya ex-Balozi wa Italy Prof. Mahalu inasemekana ni visa binafsi na uwezekano ni mkubwa kwa prof kushinda ile kesi.

Katika mazingira hayo, definetely hii ni Ngoma ya Kikubwa ambayo mkuu wa Kaya inabidi aicheze vizuri.

All in all kama ana nia ya kweli bado uwezo wa kushinda anao in any way.

Peace and Love.

Respect.
 
Wakuu wa JF, iko hivi:
[
Katika mazingira hayo, definetely hii ni Ngoma ya Kikubwa ambayo mkuu wa Kaya inabidi aicheze vizuri.

All in all kama ana nia ya kweli bado uwezo wa kushinda anao in any way.

Respect. [/COLOR][/SIZE][/FONT]

Tatizo la mkuu anang'ata na kupuliza na hiyo strategy wa watu wa .... wenzio wameshamshtukia. Angekua na msimamo angemaliza hii issue mapema. lakini anataka kujionyesha ni mtu mzuri kwakila mtu wakigeuka wenzie anawang'ata sasa wameshtuka.
 
Tatizo la mkuu anang'ata na kupuliza na hiyo strategy wa watu wa .... wenzio wameshamshtukia. Angekua na msimamo angemaliza hii issue mapema. lakini anataka kujionyesha ni mtu mzuri kwakila mtu wakigeuka wenzie anawang'ata sasa wameshtuka.

MODS Mbona mnanichanganya?

Mimi nina nyeti nyingi za kupost ambazo hazina uhusiano na thread nyingine wameziunganisha na kuipotezea.

Jamani mods anaglieni basi hata content kabla hamjaunganisha na habari za magazetini.

Nashauri thread hii iachwe pekee vingivevyo mmenichanganya maana humu kuna threads kibao mmezichanganya.

Respect.
 
Kwa mtazamo wangu ingekuwa 'magamba' yenyewe ni AC na RA,nadhani kiulaiini JK angewatosa.Lakini hapa gogoro kubwa ni mshkaji wake EL,ambaye wametoka mbali kisiasa na powerful kwenye siasa za CCM na yeye ndiye aliye play part kubwa 2005(and maybe even before that) na kuhakikisha mkulu anakwenda magogoni..Hapa ndipo panamtatiza sana JK.Na EL naye nadhani atakuwa anajuta wakati mwingine kwanini hakuchukua fomu ya Urais 2005!
 
MODS Mbona mnanichanganya?

Mimi nina nyeti nyingi za kupost ambazo hazina uhusiano na thread nyingine wameziunganisha na kuipotezea.

Jamani mods anaglieni basi hata content kabla hamjaunganisha na habari za magazetini.

Nashauri thread hii iachwe pekee vingivevyo mmenichanganya maana humu kuna threads kibao mmezichanganya.

Respect.


Nakubaliana nawe mkuu..Mods please mnaharibu utamu wote sasa!
 
....Hawa jamaa wanajidanganya,mimi nimeona huu mwelekeo muda mrefu sana,hakika tukubali tusikubali CCM ni genge la kimafia,unaweza kushangilia wanapofanya vitu kumbe wanataka kuwapumbaza mkiwa mnajiona...Naomba wanamapinduzi wa kweli tukaze buti chini ya uongozi wa chama chetu cha ukweli CHADEMA.............
 
Kuhusu Maandamano ni kweli kuna watu wanaomuunga mkono EL ambao wal wanataka waandamane na kuonyesha wako nae bega kwa bega. Yeye binafsi EL anadaiwa kusema anajiweka sawa kujibu mapigo.

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom