snowhite
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 17,708
- 23,637
Mungu Baba,
najua mimi si mkamilifu kiasi cha kusogea mbele yako
najua sina utakatifu wa kuisogelea meza yako
lakini baba katika udhaifu wangu na wa wenzangu
twaja mbele yako tukiomba msaada wako
Baba ndoa nyingi zimekuwa ni vidonda .baba wanao tumekata tamaa
Baba wanao hatuna tena uwezo kwa nguvu zetu hizi za kibinadamu
tumefunikwa upofu hatuoni tena la kufanya kunisuru ndoa zetu
Baba hakuna lingine tunaweza fanya kama taasisi hii haiko sawa baba
tunajifariji kuwa tuko ok lakini ukweli ni kwamba mioyo yetu ni mitupu na nafsi zetu hazina urazini
hatuna amani kwenye familia zetu,hatuna furaha
Baba tuliowaamini na kuwakabidhi miili na mioyo yetu ndio wamekuwa visu vya kutuumiza
na mishale ye kututoboa,dhamiri zetu ni mfu si hai tena
ndoa nyingi Baba zimepoteza uelekeo,tunatembea kwenye ubatili,tunatembea kwenye uzandiki na ufedhuli
hakuna kujaliana tena kwenye ndoa Baba,maumivu ya wenzetu yamekuwa si yetu tena
ule umoja katika uwili tulioapa kuuishi sasa hauna maana tena
ndoa nyingi zimekuwa ni kwa ajili ya ridhiko la nje la mwanadamu zaidi ya ridhiko la ndani kabisa
nyama katika nyama zetu hakuna tena
damu katika damu zetu hakuna!\
Baba tupe busara tuzipende ndoa zetu
Baba tupe busara tuamini katika kupendwa na kupenda tena
Baba tupe busara ya kutimiza wajibu wetu tukiwa ni wake au waume
Baba tujalie roho ya msamaha na kuamini katika kusamehewa
Baba tuondolee roho ya kisasi maana ulisema kisasi si kazi yako KISASI NI KWA MUNGU!
Baba vita iliyopo dhidi ya ndoa mwanadamu na macho yake ya nyama hatuwezi kuipigana Baba
VITA HII NI YAKO NA HAKIKA MIKONONI MWAKO NAIKABIDHI
UKAWAJAZE KINAMAMA NA KINABABA WOTE NEEMA YA UPENDO NA KUCHUKULIANA
UKAWAPE BUSARA YA MALEZI WANANDOA WOTE MAANA KATIKA HILI LA NDOA ZILIVYOKOSA THAMANI NA MALEZI YANATUSHINDA BABA!
UWABARIKI WATOTO WETU! NYUMBA ZETU! WAUME ZETU! WAKE ZETU!
najua mimi si mkamilifu kiasi cha kusogea mbele yako
najua sina utakatifu wa kuisogelea meza yako
lakini baba katika udhaifu wangu na wa wenzangu
twaja mbele yako tukiomba msaada wako
Baba ndoa nyingi zimekuwa ni vidonda .baba wanao tumekata tamaa
Baba wanao hatuna tena uwezo kwa nguvu zetu hizi za kibinadamu
tumefunikwa upofu hatuoni tena la kufanya kunisuru ndoa zetu
Baba hakuna lingine tunaweza fanya kama taasisi hii haiko sawa baba
tunajifariji kuwa tuko ok lakini ukweli ni kwamba mioyo yetu ni mitupu na nafsi zetu hazina urazini
hatuna amani kwenye familia zetu,hatuna furaha
Baba tuliowaamini na kuwakabidhi miili na mioyo yetu ndio wamekuwa visu vya kutuumiza
na mishale ye kututoboa,dhamiri zetu ni mfu si hai tena
ndoa nyingi Baba zimepoteza uelekeo,tunatembea kwenye ubatili,tunatembea kwenye uzandiki na ufedhuli
hakuna kujaliana tena kwenye ndoa Baba,maumivu ya wenzetu yamekuwa si yetu tena
ule umoja katika uwili tulioapa kuuishi sasa hauna maana tena
ndoa nyingi zimekuwa ni kwa ajili ya ridhiko la nje la mwanadamu zaidi ya ridhiko la ndani kabisa
nyama katika nyama zetu hakuna tena
damu katika damu zetu hakuna!\
Baba tupe busara tuzipende ndoa zetu
Baba tupe busara tuamini katika kupendwa na kupenda tena
Baba tupe busara ya kutimiza wajibu wetu tukiwa ni wake au waume
Baba tujalie roho ya msamaha na kuamini katika kusamehewa
Baba tuondolee roho ya kisasi maana ulisema kisasi si kazi yako KISASI NI KWA MUNGU!
Baba vita iliyopo dhidi ya ndoa mwanadamu na macho yake ya nyama hatuwezi kuipigana Baba
VITA HII NI YAKO NA HAKIKA MIKONONI MWAKO NAIKABIDHI
UKAWAJAZE KINAMAMA NA KINABABA WOTE NEEMA YA UPENDO NA KUCHUKULIANA
UKAWAPE BUSARA YA MALEZI WANANDOA WOTE MAANA KATIKA HILI LA NDOA ZILIVYOKOSA THAMANI NA MALEZI YANATUSHINDA BABA!
UWABARIKI WATOTO WETU! NYUMBA ZETU! WAUME ZETU! WAKE ZETU!