OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 48,775
- 102,132
Sasa tunaweza kusema wazi kwamba mzee wa ''vijana ni bomu'' hana madhara tena hasa nje ya CCM. Ni kama Simba aliyeng'olewa meno na kucha na kuwekwa katika mabanda ya sabasaba na kila mtu kuweza kumpapasa kadri ya ujasiri wake. Hali imekuwa mbaya zaidi huko Arumeru baada ya CHADEMA kumuonyesha kuwa nguvu ya pesa haiwezi kuwa zaidi ya Nguvu ya Umma, Hongera CHADEMA. CHADEMA ni wanaume wa nguvu, tofauti na Edward ambaye amewekeza zaidi kwenye siasa za KUVIZIANA makanisani na kwenye makundi ndani ya chama. Hapa nakumbuka alipotua toka Ujerumani na kauli yake kwamba ''mapambano yataendelea''. Je EL amekosa ujasiri kiasi cha kushindwa hata kuweka wazi ni aina gani ya mapambano anayofanya,je hii sio kuvisiana?
Kushindwa kukata kiu ya Watanzania juu ya ushiriki wa JK katika Richmond imezidi kumpunguzia heshima kisiasa. Ule mradi wa kununua vijana kumtembelea Monduli iliishia wapi? Jamii ya watu makini (mfano Arumeru) imemkataa, mbaya zaidi hata makanisani alipokimbilia tunasikia jumba bovu linataka kumwangukia.
Binafsi namshauri apiganie uimara wa afya yake na abaki kulea wajukuu. E.LOWASA hana madhara tena nje ya CCM.
Wanamtandao Karibuni tudhibitishe hilo
Kushindwa kukata kiu ya Watanzania juu ya ushiriki wa JK katika Richmond imezidi kumpunguzia heshima kisiasa. Ule mradi wa kununua vijana kumtembelea Monduli iliishia wapi? Jamii ya watu makini (mfano Arumeru) imemkataa, mbaya zaidi hata makanisani alipokimbilia tunasikia jumba bovu linataka kumwangukia.
Binafsi namshauri apiganie uimara wa afya yake na abaki kulea wajukuu. E.LOWASA hana madhara tena nje ya CCM.
Wanamtandao Karibuni tudhibitishe hilo