Edibily Jonas Lunyamila,"Lunya"

Haya yalikuwa ni matangazo ya moja kwa moja kutoka Uwanja wa taifa mjini Dar es salaam kupitia redio Tanzania Dar es Salaam,"Mpira unatoka katika lango la timu ya Dar Yanga Afrikans kuelekea katika lango la timu ya Simba "Taifa Kubwa", Golikipa wa Yanga Steven Nemes anaupiga mpira vizuri kabisa hukuuuuu anauchukua Said Mwamba Kizotaa Kizotaa anampasia Method Mogella Mogella pembeni kabisaaaa anampelekeaaa kwakeeee Salum Kabunda Kabundaa Kabunda kwakeee Constatine Kimanda Kimandaaa anapeleka mpira kwa Ken Mkapa Ken Mkapa Mkapa Mkapa anatoa pasi ndeeeefuuuuu kwake Lunyamila Lunyaamiilaaaaaa Lunyamilaaaa chenga ya kwanza chenga ya piliii Lunyamila bado Lunyamilaaaa Lunyamilaaaa hatari katika lango ya timu ya Simba lalalalalalalal gooo lalaa goooo alalalalal Gooooooooooooooooooooooooo!!!

Umenikumbusha mbali aisee. Enzi hizo jumamosi kabla ya mechi ya Simba na Yanga, betri zinatolewa kwenye redio asubuhi na kuanikwa juani mchana wote na kurudishwa kwenye redio saa tisa tayari kusubiri ngoma.

Baada ya sijui taarifa ya habari na matangazo ya kifo (ambayo yalikuwa yanamaliza charge za betri tuu), unasikia, "Sasa tunajiunga na Uwanja wa Taifa kusikiliza matangazo ya mpira kati ya timu za Yanga na Simba. Watangazaji wetu huko ni Charles Hilary na Omar Jongo.

Mara "Asante sana asante sana kutoka studio, karibuni katika matangazo ya mpambano mkali wa Ligi Daraja la Kwanza kati ya Mambigwa watetezi Young Africans na Simba Sports club. Mimi ni Charles Hilary nikiwa na mwenzangu hapa Omar Jongo tayari kabisa kuwaletea matangazo ya mpambano huu moja kwa moja kutoka Uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam. Hali ya hewa ni nzuri kabisa, mashabiki wamefurika pande zote kweli kweli wakiwa tayari kabisa kushughudia mpambano huu. .... Kabla ya kuwatajia lineup ya timu zote mbili turudi kwanza studio kuwasikiliza wadhamini wetu" Shiiiiiiiit.

Wakirudi uwanjani, tunatajiwa line up za timu, ambazo wote tulikuwa tunazijua anyway. Halafu ngoma inaanza, mara dakika ya tatu tuu Yanga wanafunga, na mfungaji ni yule yule aliyetufunga mwaka jana, Said Sued "Scud". Baada ya hapo wiki nzima ni kama vile vile vile mtu unaumwa maleria kali.

Siku hizi jamaa wanatangaza Ligi Kuu ya Uingereza na bado wana madoido yale yale.

[video=youtube_share;Nr76ngQzv4w]http://youtu.be/Nr76ngQzv4w[/video]
 
one of the greatest player this country has ever produced. naamini kwa upande wa left wing, hakuna kama lunyamila ktk historia ya tanzania. inasikitisha aliishia hapa hapa na kuishia kupata visenti vya akina gulamali. ndo matatizo ya kuzaliwa at a wrong time au wrong place! wanamsifu Giggs, lakini Giggs kwa Lunyamila wala haoni ndani...

Mkuu Manumbu marehemu Gulamali (rip) alimpeleka Eddy kwenye majaribio ujerumani lakini bahati haikuwa yake,alikuwa ni mchezaji mzuri sana aliyeibukia michezo ya sekondari huko shinyanga.Muhimu kutupia macho michezo ya Umiseta na umitashumta.
 
Last edited by a moderator:
siku hizi ni fundi gereji pale mwembechai BIHONYI AUTO GARAGE kajaa tele anakula spana
 
Alisoma shy bush kama sikosei.nakumbuka matokeo yake yalipotoka wapenzi wa simba walifurahia sana maana alitaga yai
Alitaga ksbb alipokuwa Form IV alikuwa ameitwa kwenye team ya Taifa ya Tanzania Bara kwenye mashindano fulani ya Challenge,kwahiyo alikuwa anatoka Shy anakuja kupigania Taifa lake wakati wenzake wanaendelea kusoma na kujiandaa na mitihani,na ndo mashindano yale yaliyoibua kipaji chake...unafikiri kwa mazingira ya namna hiyo kwanini asizungushe hata kama angekuwa ndetichia angetaga tu,hata Masuke.....kwanza mimi nachelea kusema Kijana alikuwa bright sana basi tu soka lilimnyima fursa ya kuthibitisha hilo na ndo maana alifaulu Darasa la VII peke yake katika shule aliyokuwa anasoma huko Shinyanga Vijijini
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka kulikuwa na tangazo fulani Highlights za matukio yanayoonyesha vipaji katika soka kwenye TV (nafikiri ni ITV ile) lilikuwa linamuonyesha Lunya akiruka madaluga ya mabeki wawili wa team pinzani ambao waliishia kuvaana wenyewe huku mpira ukiwa umetulia kwenye mguu wake....dah kilikuwa ni kipande fulani ambacho usingeweza kuamini kama kili'tendwa na Mtanzania....nakumbuka ilikuwa ni kwenye mashindano ya COSAFA Castle.
 
Nimewahi kukaa naye siku 1 jukwaa kuu VIP game ya Yanga alikuwa anaonyesha kusikitika jinsi wachezaji wa Yanga wa siku hizi wanavyoogopa kupiga chenga na kukokota vitu ambavyo enzi zake ilikuwa ni kama Yanga kumfunga Simba msimu huu (yaani kwa lugha ya kimahesabu huwa inasemwa "given")
 
Alitaga ksbb alipokuwa Form IV alikuwa ameitwa kwenye team ya Taifa ya Tanzania Bara kwenye mashindano fulani ya Challenge,kwahiyo alikuwa anatoka Shy anakuja kupigania Taifa lake wakati wenzake wanaendelea kusoma na kujiandaa na mitihani,na ndo mashindano yale yaliyoibua kipaji chake...unafikiri kwa mazingira ya namna hiyo kwanini asizungushe hata kama angekuwa ndetichia angetaga tu,hata Masuke.....kwanza mimi nachelea kusema Kijana alikuwa bright sana basi tu soka lilimnyima fursa ya kuthibitisha hilo na ndo maana alifaulu Darasa la VII peke yake katika shule aliyokuwa anasoma huko Shinyanga Vijijini
Mkuu tabia gani hii ya kuniombea mimi nitage? si angefanya kama mwenzake Akilimali kwenye mtihani wa form four mwaka 1999, siku moja kabla ya mtihani alipanga dawati lake safi lakini cha ajabu kesho yake hakuonekana sijui alikuwa amekula dili na headmaster ila baadaye ilibidi arudie form four na akamaliza 2000 matokeo yake siyakumbuki. Halafu jamaa ni jirani yangu huko Mbezi kwa Yusuf.
 
Inasikitisha sana nasikia Yanga walimuiba kabla hajafanya mitihani ya Form 4 sijui kweli?
 
nilimwona lunyamila pale mtwara wakati yanga ikicheza na bandari mtwara alifunga goli ambalo wachezaji wa bandari walishangilia pamoja na mashabiki waliokuja kutoka wilaya zote kuja kumwona LUNYAMILAAAAAA
 
Lunyamila alikuwa na kipaji cha aina yake. Jamaa namfagilia. Inasikitisha mno hakupata chance ya kwenda kucheza soka ughaibuni kunakoeleweka sio umangani. Nakumbuka aliwahi kupata chance ya kufanya trials na FC Koln kule Bundesliga sasa sijui ilikuwaje
Nakumbuka alienda Ujerumani kufanya trials za kujiunga bundesliga huku nyuma bongo kukawa na mechi ya Simba na Yanga pale ccm kirumba. Wanazi wa Yanga wakamtumia ujumbe arudi haraka naye akakubali. Alifika Airport ijumaa na kuunganisha ndege siku hiyo hiyo kwenda Mwanza. Kesho yake Jumamosi alicheza mpira mkubwa mno Simba akafungwa 2-0, goli moja alifunga yeye. Huo ndio ukawa mwisho wa Lunya kucheza ulaya. Huyu jamaa hata Nonda Shaban aliyechezea yanga na UEFA Champions League alikuwa anaomba usiku na mchana acheze kama Lunya. Ila siku hizi yupo Mbezi ya kimara na bado ni mnazi wa Yanga. The
 
Nakumbuka alienda Ujerumani kufanya trials za kujiunga bundesliga huku nyuma bongo kukawa na mechi ya Simba na Yanga pale ccm kirumba. Wanazi wa Yanga wakamtumia ujumbe arudi haraka naye akakubali. Alifika Airport ijumaa na kuunganisha ndege siku hiyo hiyo kwenda Mwanza. Kesho yake Jumamosi alicheza mpira mkubwa mno Simba akafungwa 2-0, goli moja alifunga yeye. Huo ndio ukawa mwisho wa Lunya kucheza ulaya. Huyu jamaa hata Nonda Shaban aliyechezea yanga na UEFA Champions League alikuwa anaomba usiku na mchana acheze kama Lunya. Ila siku hizi yupo Mbezi ya kimara na bado ni mnazi wa Yanga. The
Umenikumbusha hayo magoli yalifungwa na Bakari Malima (Jembe ulaya) yote kwa kichwa
 
nilimwona lunyamila pale mtwara wakati yanga ikicheza na bandari mtwara alifunga goli ambalo wachezaji wa bandari walishangilia pamoja na mashabiki waliokuja kutoka wilaya zote kuja kumwona LUNYAMILAAAAAA
Nilimuona Dodoma uwanja wa Jamhuri mechi na CDA kipindi hicho aisee alifunga goli 1 ambalo alimpiga mlinzi darizi na golikeeper alikuwa katoka kidogo nae akachop ule mpira. Ilikuwa hatari sana.
 
Back
Top Bottom