Eddo: Hata Pierre Nkuruzinza na Hussein Rajabu hawakukutana barabarani

watenda

Member
Mar 31, 2011
73
13
Jana nimemshuhudia Edward Lowassa akiirejea kauli yake ya miaka miwili iliyopita akidai kwamba yeye na Rais Kikwete hawakukutana barabarani, akimaanisha kwamba urafiki wao huo ambao unadaiwa kudumu kwa miongo takribani mitatu na ushee, hauwezi kumalizwa hivi hivi. Maana yake ni kwamba hata akimfanyia hujuma za namna gani, hata akikosa uadilifu kiasi gani, na hata akiwa na sifa mbaya ya uongozi iliyopitiliza hapaswi kuchukuliwa hatua kwa sababu tu hawakukutana barabarani.

Hili likanikumbusha uswahiba uliokuwa umekolea kati ya Rais wa sasa wa Burundi Pierre Nkuruzinza na mshirika wake Hussein Rajabu ambaye hapa tunapozungumza yuko gerezani akilazimika kwenda haja kubwa na ndogo kwenye ndoo. Hawa walipanga wote kuingia msituni na kuendesha harakati zilizowawezesha kushika uongozi wa nchi, Nkuruzinza akiwa Rais wa nchi na Rajabu akiwa Mwenyekiti wa chama tawala CNDD-FDD. lakini kwa sababu za kutovumilia kile ambacho Rais alikiona ni hujuma dhidi yake, utawala wake na ustawi wa nchi (kwa maoni ya Rais huyo) alichukua hatua za siyo tu kumvua madaraka ya chama Rajabu na kuwavua uongozi wa kiserikali wafuasi watiifu wa Rajabu, alimfikisha mahakama na kumshitaki kwa mashitaka mbalimbali, yakiwemo ya uhaini na hatimaye kuhukimiwa kifungo jela. Swali: Kama hawa nao walikuwa washirika wa muda mrefu na wa karibu, wakiendesha harakati pamoja na bado hatua zikachukuliwa kwa maslahi ya Taifa, nini kinachomfanya Lowassa adhani kwamba urafiki wao huo usio wa kukutana barabarani ndiyo uwe kinga yake dhidi ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa maovu yanayohusishwa naye?

Lowassa ajifunze kuelewa yale ya nchi za wenzetu kwani hata Besigye na Museveni walikuwa washirika wa karibu sana toka msituni mpaka ikulu ya Nakasero. Ona yanayotokea leo! Asijidanganye!
 
Mkuu umempa dozi kali ya mwaka na sisi wengine tuliyasahau mambo haya. Hivi kurejea rejea kauli hiyo ni kumtisha Muungwana au ni nini? Halafu anaunga mkono uasi wa vijana wake wahuni na kuomba eti wasuluhishwe na chama na kutolea mfano wa yaliyotokea wakati ule wa miaka ya 70 wakati hoja za vijana wakati huo zilikuwa za kiitikadi na hakukuwa na uchochezi kama huu wa watu waliopewa fedha ili waasi uongozi wa nchi na kukiuka katiba na maadili ya umoja wao. Jana kathibitisha kwamba kumbe wahune wale wanaoijiita UVCCM wana baraka zake.
 
kumbe ndio maana akawaita waandhishi wa habari kuongea nao ili mkuu wa kaya akimuona asimuadhibu kweli tz undugu na urafikilization utatuponza..
 
Tanzania, mmmmmhhhhh,, hawawez kufanya hvo!"""""

Livingston Lusinde- Mwana wa baba

Nape Nnauye- Mwana wa Baba

January Makamba- Mwana wa Baba

Bakar Malima- Mwana wa Baba

Husein Mwinyi- Mwana wa Baba


twende kwa urafiki......

Huko ni balaaaaa, mawazir, wakuu wa mikoa, wakurugenz..........WASHKAJI ZANGUUUUUUUUUUU
 
Jana nimemshuhudia Edward Lowassa akiirejea kauli yake ya miaka miwili iliyopita akidai kwamba yeye na Rais Kikwete hawakukutana barabarani, akimaanisha kwamba urafiki wao huo ambao unadaiwa kudumu kwa miongo takribani mitatu na ushee, hauwezi kumalizwa hivi hivi. Maana yake ni kwamba hata akimfanyia hujuma za namna gani, hata akikosa uadilifu kiasi gani, na hata akiwa na sifa mbaya ya uongozi iliyopitiliza hapaswi kuchukuliwa hatua kwa sababu tu hawakukutana barabarani.

Hili likanikumbusha uswahiba uliokuwa umekolea kati ya Rais wa sasa wa Burundi Pierre Nkuruzinza na mshirika wake Hussein Rajabu ambaye hapa tunapozungumza yuko gerezani akilazimika kwenda haja kubwa na ndogo kwenye ndoo. Hawa walipanga wote kuingia msituni na kuendesha harakati zilizowawezesha kushika uongozi wa nchi, Nkuruzinza akiwa Rais wa nchi na Rajabu akiwa Mwenyekiti wa chama tawala CNDD-FDD. lakini kwa sababu za kutovumilia kile ambacho Rais alikiona ni hujuma dhidi yake, utawala wake na ustawi wa nchi (kwa maoni ya Rais huyo) alichukua hatua za siyo tu kumvua madaraka ya chama Rajabu na kuwavua uongozi wa kiserikali wafuasi watiifu wa Rajabu, alimfikisha mahakama na kumshitaki kwa mashitaka mbalimbali, yakiwemo ya uhaini na hatimaye kuhukimiwa kifungo jela. Swali: Kama hawa nao walikuwa washirika wa muda mrefu na wa karibu, wakiendesha harakati pamoja na bado hatua zikachukuliwa kwa maslahi ya Taifa, nini kinachomfanya Lowassa adhani kwamba urafiki wao huo usio wa kukutana barabarani ndiyo uwe kinga yake dhidi ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa maovu yanayohusishwa naye?

Lowassa ajifunze kuelewa yale ya nchi za wenzetu kwani hata Besigye na Museveni walikuwa washirika wa karibu sana toka msituni mpaka ikulu ya Nakasero. Ona yanayotokea leo! Asijidanganye!

Hivi mna uhakika kwamba kweli huyu jamaa aliitisha mkutano wa waandishi wa habari akiwa nyumbani kwake au akiwa hospitali. Siamini kama waziri mkuu 'mstaafu' na rais mtarajiwa anaweza kusumbua watu halafu asizungumzie mambo ya msingi na kurudia singo yake iliyochuja ya kutokukutana na rais barabarani akaacha hoja zenye mashiko kama Richmond, binti yake Dowans na kuvuliwa gamba. Akawa bize kutisha waandishi wa habari wakati umma unaelewa na wenyewe wakisijifu kwamba wamenunua vyombo vyote vya habari. Anazungumzia vyombo vipi vya habari vilivyobaki? Si avinunue hivyo navyo amalize mchezo ili neno lake liwe kama andiko takatifu? Na waandishi wale waliokodiwa ndege kutoka Dar wakawa pale kama wapagazi, wasijue la kufanya na kuuliza maswali ya kitoto kama mtu aliyeshikwa ugoni. Aibu gani hii!
 
Huo ndo ujamaa unaoimbwa kila kukicha tanzania, na ukizingatia Sheria za nchi yetu hazina menu ni balaa tupu, Pierre wa Burundi alifanikiwa kumtia nguvuni swahiba wake kutokana na kutoendekeza ujamaa usiyo kuwa na maana yoyote ktk maendeleo ya nchi na wananchi hilo wanalitambua. Sisi huku hilo hatuna tunasubiri matukio tu na wala hatuna mipango thabiti ktk kupambana na waarifu wa nchi..
 
amesema amechoka kuchafuliwa na kupakaziwa. na kuanzia sasa atachukua hatua. NAONA MOVIE YA URAISI INAANZA.
 
Tanzania, mmmmmhhhhh,, hawawez kufanya hvo!"""""

Livingston Lusinde- Mwana wa baba

Nape Nnauye- Mwana wa Baba

January Makamba- Mwana wa Baba

Bakar Malima- Mwana wa Baba

Husein Mwinyi- Mwana wa Baba


twende kwa urafiki......

Huko ni balaaaaa, mawazir, wakuu wa mikoa, wakurugenz..........WASHKAJI ZANGUUUUUUUUUUU

mwana wa baba Vita Kawawa ....... Mwana wa baba Edward sokoine....... Mwana wa baba Riz1 kikwete.......
 
Mie narudia kusema lowassa alikuwa anapima upepo hakuwa na lolote la maana la kusema hawezi kunyea kambi, anaihitaji ccm hiihii kutimiza lengo lake kuwa Rais.Kuhusu kutokutana na kikwete barabarani nafikiri anajaribu kutuambia hata ile nafasi ya Uwaziri mkuu hakustahili alipewa kwa sababu wametoka mbali.Kweli inatisha!
 
Tanzania, mmmmmhhhhh,, hawawez kufanya hvo!"""""

Livingston Lusinde- Mwana wa baba

Nape Nnauye- Mwana wa Baba

January Makamba- Mwana wa Baba

Bakar Malima- Mwana wa Baba

Husein Mwinyi- Mwana wa Baba


twende kwa urafiki......

Huko ni balaaaaa, mawazir, wakuu wa mikoa, wakurugenz..........WASHKAJI ZANGUUUUUUUUUUU

Bakari Malima mchezaji wa zamani wa Yanga?
 
hawakukutana barabarani....lazima walikutana lang'ata au DDC kariakoo enzi hizo.,maana prezidaa kwa kuparty noma..
 
Hivi mna uhakika kwamba kweli huyu jamaa aliitisha mkutano wa waandishi wa habari akiwa nyumbani kwake au akiwa hospitali. Siamini kama waziri mkuu 'mstaafu' na rais mtarajiwa anaweza kusumbua watu halafu asizungumzie mambo ya msingi na kurudia singo yake iliyochuja ya kutokukutana na rais barabarani akaacha hoja zenye mashiko kama Richmond, binti yake Dowans na kuvuliwa gamba. Akawa bize kutisha waandishi wa habari wakati umma unaelewa na wenyewe wakisijifu kwamba wamenunua vyombo vyote vya habari. Anazungumzia vyombo vipi vya habari vilivyobaki? Si avinunue hivyo navyo amalize mchezo ili neno lake liwe kama andiko takatifu? Na waandishi wale waliokodiwa ndege kutoka Dar wakawa pale kama wapagazi, wasijue la kufanya na kuuliza maswali ya kitoto kama mtu aliyeshikwa ugoni. Aibu gani hii!

Hivi anamaanisha kwamba kutukana viongozi wa kitaifa kama Rais na familia yake na wale wote walio na misimamo tofauti na yeye ni jambo linalohitaji kukaliwa kikao na kulijadili? Mbona hakuendesha suluhu kati ya Millya na Ole Sendeka walipoparurana kwenye mkutano alioupanga yeye kule Monduli? Yeye si ndiyo kiongozi wa wamasai hao mahasimu? Kauli hii imebainisha wazi kwamba yanayotokea Arusha yana mkono na baraka zake! Anajifanya kutoa reconciliatory messages ili aonekane ni peace maker kwa vurugu anazoziasisi, kuzifadhili na kuziratibu. Hiyo "Alibi" yake ya kwamba alikuwa nje ya nchi haina mashiko. Alipanga kabla ya kwenda na huko alikokuwa alikuwa akitoa maelekezo!
 
Mimi nadhani ni Kikwete ndo anayemtuma "wambie hatukukutana barabarani"..

Una maana Kikwete Rais? Basi ndugu yangu kapimwe kichwa. Yaani rais abariki kutukanwa na kushambuliwa kwa familia yake, taasisi ya urais na hadhi ya chama halafu amtume muasisi wa hujuma hizo aongee hilo. Nadhani wengi wetu hatumjui Kikwete the President!
 
hawakukutana barabarani....lazima walikutana lang'ata au DDC kariakoo enzi hizo.,maana prezidaa kwa kuparty noma..

Wengi tulishaanza kumsahau na kusahau mabaya na madhila yake kwa uchumi wataifa hili. Sasa kama mtu aliyelogwa vile anatutonesha vidonda hivi. Wacha tu watu wamtandike maana kayataka mwenyewe.
 
lowassa alikuwa anataka kujivua gamba akatishwa na ikulu ikabidi apige porojo zingine
 
Nakumbuka mbaali sana! Enzi za mzee wa Mchinga na bendi yake ya Mchinga Sound na wimbo wake wa gunia la misumari. Jamaa anajificha kwenye kivuli cha mpapai wakati wa mvua yenye upepo mkali. Sasa akayafanya yote haya, likiwemo lile la kutaka kumpindua mwenyekiti ili achukue yeye au mshirika wake. Sasa anageuza kwende nje ya nchi kama "kivuli chake cha mpapai" lakini hakitafua dafu maana mvua hii ni cyclonic.
 
hata marehemu Mzee Kasela Bantu hakukutana barabarani na Mwl, na ndio aliye mu-introduce mwl kwa wazee wa TAA, lakini mwisho wasiku Mzee Kasela Bantu alitiwa kizuizini asitoke Tabora
 
Back
Top Bottom