Jana nimemshuhudia Edward Lowassa akiirejea kauli yake ya miaka miwili iliyopita akidai kwamba yeye na Rais Kikwete hawakukutana barabarani, akimaanisha kwamba urafiki wao huo ambao unadaiwa kudumu kwa miongo takribani mitatu na ushee, hauwezi kumalizwa hivi hivi. Maana yake ni kwamba hata akimfanyia hujuma za namna gani, hata akikosa uadilifu kiasi gani, na hata akiwa na sifa mbaya ya uongozi iliyopitiliza hapaswi kuchukuliwa hatua kwa sababu tu hawakukutana barabarani.
Hili likanikumbusha uswahiba uliokuwa umekolea kati ya Rais wa sasa wa Burundi Pierre Nkuruzinza na mshirika wake Hussein Rajabu ambaye hapa tunapozungumza yuko gerezani akilazimika kwenda haja kubwa na ndogo kwenye ndoo. Hawa walipanga wote kuingia msituni na kuendesha harakati zilizowawezesha kushika uongozi wa nchi, Nkuruzinza akiwa Rais wa nchi na Rajabu akiwa Mwenyekiti wa chama tawala CNDD-FDD. lakini kwa sababu za kutovumilia kile ambacho Rais alikiona ni hujuma dhidi yake, utawala wake na ustawi wa nchi (kwa maoni ya Rais huyo) alichukua hatua za siyo tu kumvua madaraka ya chama Rajabu na kuwavua uongozi wa kiserikali wafuasi watiifu wa Rajabu, alimfikisha mahakama na kumshitaki kwa mashitaka mbalimbali, yakiwemo ya uhaini na hatimaye kuhukimiwa kifungo jela. Swali: Kama hawa nao walikuwa washirika wa muda mrefu na wa karibu, wakiendesha harakati pamoja na bado hatua zikachukuliwa kwa maslahi ya Taifa, nini kinachomfanya Lowassa adhani kwamba urafiki wao huo usio wa kukutana barabarani ndiyo uwe kinga yake dhidi ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa maovu yanayohusishwa naye?
Lowassa ajifunze kuelewa yale ya nchi za wenzetu kwani hata Besigye na Museveni walikuwa washirika wa karibu sana toka msituni mpaka ikulu ya Nakasero. Ona yanayotokea leo! Asijidanganye!
Hili likanikumbusha uswahiba uliokuwa umekolea kati ya Rais wa sasa wa Burundi Pierre Nkuruzinza na mshirika wake Hussein Rajabu ambaye hapa tunapozungumza yuko gerezani akilazimika kwenda haja kubwa na ndogo kwenye ndoo. Hawa walipanga wote kuingia msituni na kuendesha harakati zilizowawezesha kushika uongozi wa nchi, Nkuruzinza akiwa Rais wa nchi na Rajabu akiwa Mwenyekiti wa chama tawala CNDD-FDD. lakini kwa sababu za kutovumilia kile ambacho Rais alikiona ni hujuma dhidi yake, utawala wake na ustawi wa nchi (kwa maoni ya Rais huyo) alichukua hatua za siyo tu kumvua madaraka ya chama Rajabu na kuwavua uongozi wa kiserikali wafuasi watiifu wa Rajabu, alimfikisha mahakama na kumshitaki kwa mashitaka mbalimbali, yakiwemo ya uhaini na hatimaye kuhukimiwa kifungo jela. Swali: Kama hawa nao walikuwa washirika wa muda mrefu na wa karibu, wakiendesha harakati pamoja na bado hatua zikachukuliwa kwa maslahi ya Taifa, nini kinachomfanya Lowassa adhani kwamba urafiki wao huo usio wa kukutana barabarani ndiyo uwe kinga yake dhidi ya hatua zinazopaswa kuchukuliwa kwa maovu yanayohusishwa naye?
Lowassa ajifunze kuelewa yale ya nchi za wenzetu kwani hata Besigye na Museveni walikuwa washirika wa karibu sana toka msituni mpaka ikulu ya Nakasero. Ona yanayotokea leo! Asijidanganye!