EAC wajadili mchakato sarafu moja

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
EAC wajadili mchakato sarafu moja Monday, 17 January 2011 20:13

Mussa Juma, Arusha

NCHI za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC), jana zilianza mchakato wa kuanza matumizi ya sarafu moja kwa nchi hizo , ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya jumuiya hiyo.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, Balozi Juma Mwapachu, akizungumza katika kikao hicho, alisema wajumbe tisa katika nchi tano za jumuiya hiyo wamechaguliwa kushughulikia suala hilo.

Alisema umoja wa fedha katika nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki utasaidia sana kukuza uchumi na kuimarisha mahusiano katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara.

" Leo tumeanza na kikao cha kwanza cha kuanzisha mchakato wa kuwa na umoja wa fedha, hadi kufikia mwezi Machi nadhani tutakuwa katika hatua nzuri,"alisema Mwapachu.

Alisema hadhani kama kutakuwa na ugumu wa kufikia kuwa na umoja wa fedha kwani tayari itifaki mbalimbali za jumuiya hiyo zimesainiwa na kuwa na mafanikio.

"Tulikuwa na itifaki ya umoja ya forodha , tukaja soko la pamoja sidhani kama hili la umoja wa fedha litakwama"alisema Mwapachu.

Katika majadiliano hayo ya umoja wa fedha, kimsingi jana wawakilishi wa nchi zote wanachama wa jumuiya hiyo, walikubaliana kuanza majadiliano ya kufikia hatua ya kuwa na sarafu moja.

Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki hadi sasa ni Tanzania, Uganda, Kenya, Rwanda na Burundi ambao ndio wanashikilia nafasi ya Uenyekiti wa jumuiya hiyo.

 
" Leo tumeanza na kikao cha kwanza cha kuanzisha mchakato wa kuwa na umoja wa fedha, hadi kufikia mwezi Machi nadhani tutakuwa katika hatua nzuri,"alisema Mwapachu.

Hivi kinachoanza ni benki kuu moja au sarafu moja? Are we not placing a cart before horses..................
 
wakiweka bank kuu moja tunataka ikae Arusha, na si Nairobi kama kipindi kile, kwasababu wakenya walituonea sana ile bank ya kipindi kile. tuwe macho sana kwa sasaivi.
 
wakiweka bank kuu moja tunataka ikae Arusha, na si Nairobi kama kipindi kile, kwasababu wakenya walituonea sana ile bank ya kipindi kile. tuwe macho sana kwa sasaivi.
Labda Mafisadi wawe wameshatwaliwa na Bwana ndio pesa zitakuwa Salama
 
Hii kitu ni bad idea especially in light ya matatizo tunayoyaona katika Euro zone. Kwa kile ambacho wakuu wanataka, ile East African Currency Board (EACB) ndiyo inayoweza kurudi kuzireplace member states Central Banks. Tatizo kubwa la Monetary Union au muungano wowote ule ni uachiaji wa nguvu za kutunga sera na kuzisimamia mamlaka nyingine. Hii monetary union inamaanisha BoT watasalimisha uwezo wao wa kutunga na kusimamia monetary policy kwa EACB or whatever the new currency board/regional central bank is going to be called.

Binafsi ningependa kuona Tanzania ikiweka conditionalities za kuingia katika Monetary Union hii kama zile alizoweka Gordon Brown wakati wa mchakato wa Uingereza kuingia katika Eurozone. Na test hizo zilikuwa ni;

Economic Harmonisation.

The UK economy must be harmonised with the Euro zone. If the UK economy was growing much faster than EU then UK interest rates would need to be higher. For example, at the moment if the UK joined interest rates would fall and this may cause inflation. Therefore it is essential that the UK has a similar economic cycle to Europe. Even if there is temporary harmonisation there is no guarantee it will continue on a permanent basis.

Is there sufficient Flexibility?

If the UK went into recession could it be able to cope? It would have no influence over Monetary policy but also Fiscal policy is limited by the growth and stability pact. This limits the amount of government borrowing and therefore limits the scope for expansionary fiscal policy.

Effect on Investment.

Would joining the euro create better conditions for firms making long-term decisions to invest in Britain? UK inward Investment has not suffered since the UK decided not to join

Effect on Financial services.

What impact would entry into the euro have on the UK's financial services industry? London as a financial centre has boomed in recent years.

Effect on Growth and Jobs

Would joining the euro promote higher growth, stability and a lasting increase in jobs? There is no clear evidence that it would. UK economy has done better outside the Euro than in the Euro.

Kwa hizo za juu unaweza kusubstitute the UK for Tanzania na Euro for the proposed East African Shilling.
 
Back
Top Bottom