EAC kujenga mtandao wa reli

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,122
Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, zimeazimia kujenga mtandao wa reli utakaoziunganisha kwa lengo la kuimarisha usafirishaji wa kikanda ili kukuza uchumi na maendeleo ya jamii.Katibu Mkuu wa Wizara ya Afrika Mashariki, Stergomena Tax, aliyasema hayo jana katika mkutano uliokutanisha wizara yake na Wizara ya Miundombinu kuelezea kuhusu kongamano la kanda ya EAC litakalofanyika siku mbili mfululizo kuanzia leo jijini Dar es Salaam.
Kongamano hilo linatarajia kufunguliwa na Rais Jakaya Kikwete na litahusisha nchi zote wanachama, wadau wa maendeleo, wawekezaji binafsi pamoja na wadau wa usafiri wa reli ili kujadili kwa pamoja namna ya kuboresha, kuendeleza reli na gharama itakayotumika.
Tax alisema mkutano huo utajadili mpango kamambe wa reli wa nchi za EAC na namna utakavyotekelezwa.
Alisema hatua hiyo imetokana na maagizo ya wakuu wa nchi za EAC ambao walikaa mwaka 2004 na kukubaliana kuandaa mpango kamambe wa ujenzi wa miundombinu.
"Wakuu hawa walitambua kwamba bila kuandaa mpango huu nchi zote katika ukanda huu zitabakia kutokuwa na ushindani kutokana na gharama kubwa za usafirishaji na uchukuzi kuliko sehemu nyingine duniani," alisema.
Tax alisema katika mkutano huo wa mwaka 2004 wakuu wao waliguswa na tatizo la kudidimia kwa huduma za uchukuzi wa reli na mchango wake katika usafirishaji wa mizigo na kuharibika kwa miundombinu ya barabara katika ukanda huo kutokana na usafirishaji wa mizigo mingi.
Aidha, alisema kutokana na maagizo ya wakuu hao, Sektetarieti ya EAC ilimteua mshauri mwelekezi ambaye ni CPCS Transcom ya Canada, kufanya kazi ya kutayarisha mpango kamambe wa reli ya Afrika Mashariki (EARMP) ambaye aliikamilisha Januari, mwaka jana.
Alisema mshauri huyo aliukabidhi mpango huo kwenye kikao cha mawaziri wa sekta ya uchukuzi, mawasiliano na hali ya hewa ambao nao walipendekeza kufanya mabadiliko na kuongeza njia nyingine mpya za reli ambazo zilisahaulika kwenye mpango huo.
Tax alisema kutokana na tatizo la miundombinu ambayo ndio itakayoweza kufungua fursa nyingi za kufanya biashara wameamua kukutana leo ili kuona namna ya kuziboresha.
Naye Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Miundombinu, Omar Chambo, alisema ndani ya mpango huo, Serikali ya Tanzania imekusudia kutekeleza miradi miwili muhimu ya kimataifa.
Chambo alisema wamekusudia kujenga reli ambayo itajumuisha nchi tatu ya Tanzania, Rwanda na Burundi ambayo itakuwa na umbali wa kilomita 1651.
"Reli hii itaanzia Dar es Salaam-Isaka Kigali/Keza-Gitega -Musongati ambapo kati ya umbali huo kilometa 970 ni za kuboresha reli ya kati ya kutoka Dar es Salaam hadi Isaka, kilomita 494 ni ujenzi wa reli mpya ya kati kutoka Isaka hadi Kigali, Rwanda na kilomita 197 ni ujenzi wa reli mpya ya kati kutoka Keza hadi Musongati Burundi," alisema.
Chambo alisema hivi sasa upembuzi yakinifu umeshakamilika na kazi inayofuata ni kufanya usanifu wa kina na kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa reli hiyo.
Kadhalika, alisema wanatarajia kujenga reli mpya ya Arusha hadi Musoma itakayojumuisha nchi za Tanzania na Uganda yenye umbali wa kilomita 573.
Alisema kutokana na umuhimu wa miundombinu katika kukuza uchumi na kuleta maendeleo ya jamii wizara yake imeweka miradi hiyo kwenye programu ya miaka 10 ya uwekezaji.
Alisema pamoja na utekelezaji wa ujenzi wa reli, serikali inaendelea kutekeleza miradi ya barabara kwa kujenga barabara kutoka Arusha, Namanga hadi mto Athi kwa urefu wa kilomita 240.
"Barabara nyingine ni Arusha, Holili hadi Voi kwa kilomita 260, barabara ya Malindi, Lungalunga, Tanga hadi Bagamoyo kwa kilomita 400 na uanzishwaji wa Vituo vya Pamoja vya Mipakani (OSBP)," alisema.
Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo, Balozi Juma Mwapachu, alisema kutokana na kuwepo kwa hali mbaya ya miundombinu, Rais wa Benki ya Dunia alipowatembelea Marais wawili wa EAC, aliomba kuharakishwa kwa kongamano hilo ili waweze kutazama tatizo la mfumo wa reli moja au kuongeza zaidi.



CHANZO: NIPASHE
 
Mkuu, this is a big joke.
each country should sort its own messy first before thinking of connecting rail-way.
sasa tukishaunganisha njia za reli ndo itakuwa nini kama reli zenyewe hazipo na hazifanyi kazi?

wanasiasa wananiudhi sana, na nafikiri IQ yao huwa inamatatizo. Privetization imemaliza nchi hii jamani!!!! utafufuaje reli wakati kuna waarabu wana semi-trailer zinabeba mizigo kwenda Zambia, malawi, Congo< Ruanda, Burundi na kwingineko......achilia mbalai mikoa yote ya Taz? Ukifufua reli maana yake hawa Waarabu na waswahili kiduchu wafanye nini? malori yao wayapeleke kubeba Taka manispaa ya Temeke??

Kunahitajika nguvu ya ziada, ahaya yanayofanyika sio kwa defolt, yamepangwa na wahuni, na viongozi wetu wameyakubali. Nyerere alishawahi kusema kuwa mtu akikushauri kitu cha kijinga na wewe ukakubali, basi atakuona wewe ni mjinga zaidi.
 
Mkuu, this is a big joke.
each country should sort its own messy first before thinking of connecting rail-way.
sasa tukishaunganisha njia za reli ndo itakuwa nini kama reli zenyewe hazipo na hazifanyi kazi?

wanasiasa wananiudhi sana, na nafikiri IQ yao huwa inamatatizo. Privetization imemaliza nchi hii jamani!!!! utafufuaje reli wakati kuna waarabu wana semi-trailer zinabeba mizigo kwenda Zambia, malawi, Congo< Ruanda, Burundi na kwingineko......achilia mbalai mikoa yote ya Taz? Ukifufua reli maana yake hawa Waarabu na waswahili kiduchu wafanye nini? malori yao wayapeleke kubeba Taka manispaa ya Temeke??

Kunahitajika nguvu ya ziada, ahaya yanayofanyika sio kwa defolt, yamepangwa na wahuni, na viongozi wetu wameyakubali. Nyerere alishawahi kusema kuwa mtu akikushauri kitu cha kijinga na wewe ukakubali, basi atakuona wewe ni mjinga zaidi.

Hata mimi sielewi hapa.

TRL tunasikia kila siku watumishi wanagoma mara treni imeanguka, matatizo lukuki. Sasa sielewi kama kweli kuna utatuzi wa dhati au basi tu ndo vile wanatafuta turufu fulani kwa kutoa ahadi hewa.
 
Hata mimi sielewi hapa.

TRL tunasikia kila siku watumishi wanagoma mara treni imeanguka, matatizo lukuki. Sasa sielewi kama kweli kuna utatuzi wa dhati au basi tu ndo vile wanatafuta turufu fulani kwa kutoa ahadi hewa.
Abdulhalim!
You are absolutely right huo ni ujiko wa wanasiasa uchwara kama Jakaya Mrisho Kikwete na akina MSEVENI. Kikwete and his bandwagon have never been serious as long as CCM haijawahi kufanya anything meaningful na hao partners wake whether ni wa short term or long term hakuna chochote zote ni ahadi hewa tu. Enzi za Mkapa, M-7 alitaka kujenga reli kutoka Tanga kupitia Arusha kuelekea Uganda alipokuwa at logger heads na akina Moi . Can Mkapa or M-7 tell us waht happened about that project na wakati huo Jakaya was the foreign minister he talked a lot of nonsense about the EA Community revival and today he is comedying about railway intergration hii ni aibu. For more than ten years its only blah blah---While Rites the Indian fools wanted and actually uprooted some sections of the Moshi-Taveta- Voi railway line and these fools are dreaming. Nadhani nimechoka and have no words to express my anger!!!!
 
Mkuu, this is a big joke.
each country should sort its own messy first before thinking of connecting rail-way.
sasa tukishaunganisha njia za reli ndo itakuwa nini kama reli zenyewe hazipo na hazifanyi kazi?

wanasiasa wananiudhi sana, na nafikiri IQ yao huwa inamatatizo. Privetization imemaliza nchi hii jamani!!!! utafufuaje reli wakati kuna waarabu wana semi-trailer zinabeba mizigo kwenda Zambia, malawi, Congo< Ruanda, Burundi na kwingineko......achilia mbalai mikoa yote ya Taz? Ukifufua reli maana yake hawa Waarabu na waswahili kiduchu wafanye nini? malori yao wayapeleke kubeba Taka manispaa ya Temeke??
Kunahitajika nguvu ya ziada, ahaya yanayofanyika sio kwa defolt, yamepangwa na wahuni, na viongozi wetu wameyakubali. Nyerere alishawahi kusema kuwa mtu akikushauri kitu cha kijinga na wewe ukakubali, basi atakuona wewe ni mjinga zaidi.

Samahani mdau hivi Temeke siku hizi ndo kumekuwa DAMPO au umetolea mfano??
..Ni kweli kabisa maneno hayo yanadhihirisha maono ya Baba wa Taifa ...kwa kuweka sawa alitumia neno Zuzu tena zuzu la mwisho( badala ya mjinga)...Rais wetu anapokuwa jukwaani mara nyingine anawezakuzungumza vitu ambavyo ni vyakufirika zaidi kuliko kutendwa??..Nakumbuka hawa rites walipokuwa na kuleta vichwa vya matreni ni yeye alikwenda kufanya ufunguzi wake akasema tuwape muda...sasa wamenyea kambi naona cha kuzungumza mkuu wa kaya hana...tutegemea nyimbo nzuri za maneno toka kwa viongozi wetu kuelekea kwenye uchaguzi
 
Abdulhalim!
You are absolutely right huo ni ujiko wa wanasiasa uchwara kama Jakaya Mrisho Kikwete na akina MSEVENI. Kikwete and his bandwagon have never been serious as long as CCM haijawahi kufanya anything meaningful na hao partners wake whether ni wa short term or long term hakuna chochote zote ni ahadi hewa tu. Enzi za Mkapa, M-7 alitaka kujenga reli kutoka Tanga kupitia Arusha kuelekea Uganda alipokuwa at logger heads na akina Moi . Can Mkapa or M-7 tell us waht happened about that project na wakati huo Jakaya was the foreign minister he talked a lot of nonsense about the EA Community revival and today he is comedying about railway intergration hii ni aibu. For more than ten years its only blah blah---While Rites the Indian fools wanted and actually uprooted some sections of the Moshi-Taveta- Voi railway line and these fools are dreaming. Nadhani nimechoka and have no words to express my anger!!!!
Mkuu, I dont understand these guys......kweli. unaongea kujenga reli wakati umeshindwa kuendesha shirika la reli, na wahuni hawa wahindi wamekuja kula.
Mnakumbuka kuwa 2005 CCM ilipewa magari yanaitwa Mahanra kutoka India? na mnakumbuka Raisi or Waziri mkuu wa India alikuja kwenye inaguration ya Kikwete? sasa ni Pay back time. Rites ni kampuni kubwa na ina uzoefu wa kuendesha treni India, lakini kwa nini ahawawezi hapa? Hwa wamekuja kwa makusudi mazima ya kuchukua walichoipa CCM mwaka 2005.

And we the sons and daughters of Tanganika, tunawapa hawa wahuni madaraka....We need to do something.
 
Back
Top Bottom