Wanajamvi wenzangu, nimeona tangazo la kuitwa watu kwenye usaili katika sekretarieti ya ajira ya utumishi wa umma usaili utakaofanyika kuanzia tarehe 20 September 2012 hadi 5 October 2012. Kwa wale wote mliiomba mnaweza kupitia pitia katika tovuti yao ila naona wameita baadhi ya fani na sina uhakika kama ni zile nafasi 2285 za May au ni nyingine? Pia nimeona wameitwa kwenye usaili watu 730 walioomba nafasi ya ukatibu tarafa, hivi wanahitajika watu wangapi hadi waitwe idadi yote hiyo? ..........................Kaaaazi kweli kweli!!!!