Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,404
- 31,384
- Thread starter
- #21
Nikushukuru kwa maoni yako. Ni kweli kuwa gharama za ushiriki wa Gadafi katika vita ya Kagera umetugharimu.Watu wa Magharibi wana sera isiyotangazwa inaitwa FACTS ON THE GROUND. Watakudunda au kukupora rasilimali ili mnegotiate kwa maslahi yao mfano mafuta ya Libya na kuwepo na taifa la Israel nchini Palestina.
"Mapanya" wa Libya wamedhibiti sehemu kubwa ya nchi lakini tusubiri kama wataweza kuiongoza Libya kama nchi huru ya Walibya na yenye maslahi kwa walibya.
Katika mstakabali wo wote endelevu ebu jiulize maswali machache.
1 Lengo (la muda mfupi, wa kati na mrefu) ni nini?
2. Mkakati wake unatekelezeka?
3. Kuna rasilimali za kutekeleza mkakati huo?
4. Mfumo wa tathmini upo katika kila hatua?
5. Madhara na changamoto zinatatulika?nani?
6. Manufaa (ya muda mfupi, wa kati na mrefu) yanatambulika na yanamnufaisha nani?
Naamini kwa tukio la NTC huko Libya ni sawa na kuingia kwenye awamu mpya ya ukoloni mambo leo. Kwa kwetu hilo pia ni lakujifunza lakini nani ajifunze nini ndiyo issue.
Watawala hawakubali ya NTC Libya kwa sababu walinufaika na Gadafi, halafu athari za mabadiriko kwao ni suicide (angalia ya Igunga)
Sisi kama taifa hatukuwa na chaguo na wala hatukuwa na tatizo na Libya. Tutakumbuka kuwa kwa mara ya kwanza Idd Amin aliishambulia Tanzania mwaka 1973 kwa ndege kule Mwanza na busara za Mzee Haile Selasi (RIP) na Mwalimu Nyerere(RIP) ziliepusha balaa hilo. Amin akadhani Tanzania ni wadhaifu hadi alipoamua kuchukua kipande cha Ardhi.
Mbinu aliyotumia Idd Amin ni kutangaza kuwa kulikuwa na njama za kuuhujumu Uislam jambo ambalo Wazanzibar wengi wanadhani ni kweli katika kujenga hoja za chuki dhidi ya muungano. Ni hapo ndipo alimuomba msaada na Gadaffi kukubali hilo kwa misingi ya utetezi wa kidini.
Hizi zikawa ni dalili za mwanzo za ubabe wake aliouendeleza hadi kufikia kipigo cha Rais Reagan.
Gadafi akachukua mwelekeo mpya pale alipokosana na wenzake katika Arab League, hili lilitokea kwa sababu ya msimamo wake juu ya Palestina akiamini kuwa umoja huo umekuwa mamluki na kuwatelekeza Wapalestina. Inaweza kuwa alikuwa na hoja ya msingi na maana zaidi tukiangalia Arab league inavyofanya kazi kama mhuri wa nchi za Magahribi.
Libya ikahamishia nguvu zake AU na alisaidia sana katika makundi ya uasi na ukombozi. Ndiyo maana ANC wamechukizwa sana na kitendo cha NATO. Hata pale ilipokuwa katika vikwazo vya uchumi Mandela alithubutu kwenda kwa Gaddafi kumshukuru kwa misaada akiwaambia nchi za magharibi kuwa wakati wa dhiki Libya ilikuwa nao na hawakubali kuchaguliwa Rafiki.
Wakati AU ikipita katika kipindi kigumu sana kiuchumi na kisiasa Gadaffi alitumia rasilimali zake kuendesha umoja huo. Ikafikia mahali akataka awe mwenyekiti licha ya historia yake yenye utata. AU hawakuwa na chaguo ila kukubaliana na mfadhili wao.
Gadaffi akataka umoja wa Africa U.S.A akitaraji kuwa rais ndoto ambayo haikutimia na ilijengwa katika ubabe tu.
Licha ya kwamba alifanya mambo mchanganyiko mazuri na mabaya, huko nyumbani hali haikuwa shwari.
Kile alichokipigania kuondoa ufalme ndicho alichokirejesha ingawa si rasmi ni kwa mgongo wa demokrasia ambayo haikuwepo bali serikali ya familia.
Libya ikawa haina taasisi za kisiasa (alternative political institutions) kama ilivyokuwa kwa Misri n.k.
Mfumo wa demokrasia ukabaki kwenye majukwaa na karatasi ukweli ukiwa ni mfumo wa kifalme.
Ni kutokana na kukosekana mbadala wa kisiasa, yalipotokea maasi Libya ikabaki kuwa kama taifa lililopata uhuru leo.
Lengo la kwanza la 'mapanya' lilikuwa kumuondoa Gaddhafi kwani hiyo ndio ilikuwa kazi kubwa kuliko nyingine.
Maasi hayakuanza kwa watu wa kaliba ya juu bali wananchi wa kawaida bila kuwa na mkakati wa muda mfupi, wa kati au mrefu lengo likiwa kumuondoa kwanza.
Tutakumbuka walivyokuwa wanapigana bila mpangilio wakisaidiwa na ari hadi NATO ilipowasaidia. Inaweza kuwa kulikuwa na mkakati wa NATO, ukweli wa mageuzi ya Arab spring hatuwezi kuupuza hata kidogo. Hata wa Israel wanajua impact ya Arab spring kwa mustakabali wao ndiyo maana Mahamoud Abas wa Palestina amekuwa na 'guts' hadi kupelekaea Israel kunywea katika baadhi ya misimamo.
Ni ukweli ya kuwa kuna changamoto nyingi sana zilizopo mbele ya Libya. Tunachokiona sasa ni post war honeymoon.
Moja ya changamoto ni kujenga taasisi za kisiasa zitakazoleta utengamano jambo ambalo si rahisi kama inavyodhaniwa.
Ukweli unabaki kuwa yatakuwepo mapambano ya ndani 'power struggle' kati ya waliojitoa mhanga na kundi lililofaidika na Gadhafi.
Malengo ya muda mfupi moja lilikuwa kumuondoa Ghadafi, ya muda wa kati ni kujenga taasisi za kisiasa na muda mrefu ni kuwa na taifa moja huru.
Haya hayataweza kupatikana katika sahani ya fedha ' silver plate' yatakuja na gharama kubwa na hilo lazima wajiandae nalo.
Je wana rasilimali za kufanya hivyo? jibu ni ndiyo kuanzia rasilimali watu hadi fedha, ingawa watalazimika kulipia gharama za vita hasa tukizingatia kuwa Libya ina mafuta safi dunia na kwa wingi kwahiyo macho ya wakubwa hayataondoka hapo leo au kesho.
Sijui investment ya elimu aliyoifanya Gaddhafi itawezaje kusaidia katika mikakati kwani ni dhahiri kuwa wasomi hasa wa nchi za kiafrika hawaaminiki hata kidogo. Nchi kama yetu inamalizwa na wasomi sio wafugaji au wakulima. Je wasomi wa Libya ni 'half baked' kama wetu, linabaki kuwa swali gumu.
Mfumo wa kutahmini changamoto na maendeleo utategemea uimara wa serikali nayo ni changamoto kubwa sana.
Changamoto zinatatulika ingawa itachukua muda mrefu kutokana na kutokuwa na mbadala wa kisiasa ulioachwa na Gadhafi kama tunavyoona Misiri pia. Libya ina uwezo kinachotakiwa ni utashi wa kisiasa.
Manufaa hayataweza kutambulika katika kipindi kifupi, muhimu ni pale nchi itakapokuwa imejenga mfumo thabiti wa kujitawala kwa vizazi vijavyo.
Tunao mfano wa Rwanda iliyokuwa majivu 'reduced to ash' na sasa tunaiona inachanja mbuga. Haya hayakutokea katika muongo mmoja bali miwili na bado ina safari ndefu.
Tatizo ninaloliona ni siasa za nchi za kiarabu zisizo tabirika na zinazotawaliwa na hisia kali.
Hatuwezi kukataa uwepo wa ukoloni mambo leo kwa ajili ya rasilimali, nakuhakikishia kuwa nchi za kiarabu zina 'compicated political sphere' na hivyo hakuna gurantee.
Tunaona jini lililokuwa kwenye chupa Misri linavyoumiza vichwa vya nchi za magharibi. Usijeshangaa ukisikia Islamic brotherhood wanaongoza nchi kama Hamas walivyowashangaza katika uchaguzi huru na wa haki pale Palestina na si dhani Libya inaweza kuwa tofauti sana, tatizo ni kuwa hatujui mbadala ni upi kule Libya.
Bado naamini Libya ina somo zuri sana ukilinganisha na yaliyotokea Arab spring. Tunaona maana halisi ya uhuru na si kuwa na kila kitu, tunajifunza kuwa nguvu ya utawala haipo jeshini bali ndani ya umma, tunajifunza ni kwanini tunatakiwa tuwe na taasisi za kisiasa mbadala, tunaona jinsi rasilimali zinavyokodolewa macho, na kikubwa zaidi ni kuwa utu wa mtu si chakula na malazi tu ni pamoja na ushiriki wake katika kuamua mustakabali wa taifa lake.