Mkuu wangu shukran sana na naomba tuvumiliane...Mimi huandika na makosa mengi sana kwa sababu moja kuu. Pengine niwaulize wana JF kina Maxence maana kila napoandika hoja kuna tracing huingia na mara zote znisipokharakisha ku post siwezi tena huwa inaingiwa kiasi kwamba lazima nizime PC kuislafisha na kisha kuanza upya. Hivyo, ni rahisi kuandika haraka na ku post kisha nafanya marekebisho ikisha kuwa hewani. Hapo siingiliwi kabisaaaa!
Tatizo jingine siwezi kuandika pembeni ktk word kisha ndio nirudi hapa na kunukuu nilichoandika ktk word. Nimejaribu hivyo sana na kujiona kama mwandishi wa magazeti ama mtu anayeshindwa kujadili wakati anasoma maelezo ya mtu mwingine. Hata hivyo nitajitahidi kuweka fikra zangu na mnapoona makosa jaribuni kunipa muda..