Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,393
- 31,344
Ndugu wanajamvi,
Awali ya yote niwatake radhi nitakao wakwaza kutokana na kauli zangu.
Sina lengo baya zaidi ya lile la kuboresha.
Ukitembelea majukwa mengi hapa JF, japo basi unaweza kutoka na kitu. Niseme wazi jukwa la elimu ambalo nilidhani lingeng'ara kwahakika limedoda.
Jukwa limegeuzwa sehemu ya kusemana na kutafuta CV za watu,kuomba past papers, aidha limekuwa la kupeana taarifa za mikopo badala ya maarifa ya kieleimu.
Hayo hayana ubaya lakini yasiwe ndio sehemu kuu ya jukwaa la elimu.
Jukwaa lazima libebe maana halisi ya elimu na si kwasababu tu!
Katika dunia ya sasa elimu siyo diploma,degree za uzamili au uzamivu. Elimu ni namna gani utaweza kukabiliana na mazingira magumu ya ushindani. Kwa sasa tumeanza na soko la pamoja la EAC lakini pia sisi tukiwa kama sehemu ya dunia tunachanganyika na watu wa mataifa mengine. Kuna fursa nyingi tu zinazoweza kubadilisha maisha yetu.
Mathalani, nimesoma mara nyingi watu wakiuliza kozi gani bomba au inalipa. Ukweli wa mambo ni kuwa kila kilichopo duniani ukiweza kukitumia vizuri na kwa maarifa kinalipa. Lakini pia lazima uelewe kuwa milango haipo wazi kana kwamba utaweza kupata kila kitu kama unavyotaraji.
Kozi kama za ualimu watu wengi wanaziona kama hafifu lakini hawajui kuwa ndizo kozi zenye milango mingi sana na zinazoingiliana na kozi nyingine kwa namna moja au nyingine. Nitumie msemo wa mitaani kozi ya ualimu ni kama 'funguo malaya' inayoweza kufungua kila mlango. Tatizo watu hawaangalii mambo kwa mtazamo mpana na hapo kuna kupotea kwa hali ya juu.
Ni lazima ujiulize pia endapo kozi 'bomba' unayoitaka katika maisha yako itaweza kukupa fursa!!.
Dunia imebadilika, kuna wasomi wengi wenye sifa wanazurura, sasa mwenzangu uliyehitimu juzi tu kama unadhani umefika ukweli ni kuwa hujafika.
Soko la ajira la sasa haliangalii Degree yako au GPA, linaangalia wewe kama mwajiriwa utaweka nini mezani kulisaidia shirika ua taasisi. Una ujuzi gani zaidi ya degree yako ambayo kila mtu anayo na wengine wanazo kutoka katika vyuo vyenye heshima.
Ikifika hapo kuna mambo yanajitokeza:
1. Una kitu gani kinachokutofautisha na washindani wako wengine? Nafasi moja ya kazi inaweza kuwa na candidates 300, sasa kwanini wewe uajiriwe na si Mr au Miss X ambaye licha ya ukubwa wa degree yake lakini pia anauzoefu kukuzidi. Wenye lugha zao wanasema 'how do you stand out of the crowd'.
2. Unawezaje kujiuza kwasababu nyote mliopeleka CV mnabidhaa ile ile, sasa kwanini waajairi wadhani bidhaa zako ni bora zaidi ya zile 299 zilizojitangaza kuwania nafasi hiyo.
Hapa kunaingia vitu vingine kama ifuatavyo:
a)Ni kwa vipi CV yako imeweza kupenya na kuwa short listed katika zile 10, kutoka zile 299 kwa ajili ya Interview.
Kumbuka usipokuwa short listed basi huna interview na huna kazi hata kama una degree zako na GPA safi.
Kwahiyo unatengenezaje CV (Resume) yako ili ukubalike katika kuingia katika 10 bora ni muhimu sana.
b) Katika 10 bora watakaoitwa katika interview utawezaje kuwashawishi jopo la watahini ili uwe ndani ya 3 bora?
Hapa ndipo mbinu za interview zinapokuja.
Hapa nimejaribu kutoa tu muhtasari wa namna gani dunia inakuwa ya ushindani hata kama una nondo zote.
Ninachotaka kusema hapa ni kuwa, kuwa na Bachelor, master au PhD bado hakujakuhakikishia makali katika ushindani wa dunia ya leo. Ni jinsi gani unajiuza na unaweza kuuza hizo degree zako ni muhimu sana.
Tena teknolojia imesonga mbele hizo CV zinachaguliwa kwa computer, sasa hapo suala la kujuana 'technical know who' halipo. Matokeo ya yote utaishia kukimbilia ukabila na udini wakati ukweli ni kuwa hujui kujiuza au kuuza bidhaa zako.
Hebu tuangalie mambo yaliyosemwa hapo juu, kozi, kuandika CV, kufanya Interview n.k
Wenye jukwaa kama mtaridhia basi tutaendelea kudadavua kwa kiasi tunachoweza ili kupeana maarifa.
Noamba kutoa hoja.
Awali ya yote niwatake radhi nitakao wakwaza kutokana na kauli zangu.
Sina lengo baya zaidi ya lile la kuboresha.
Ukitembelea majukwa mengi hapa JF, japo basi unaweza kutoka na kitu. Niseme wazi jukwa la elimu ambalo nilidhani lingeng'ara kwahakika limedoda.
Jukwa limegeuzwa sehemu ya kusemana na kutafuta CV za watu,kuomba past papers, aidha limekuwa la kupeana taarifa za mikopo badala ya maarifa ya kieleimu.
Hayo hayana ubaya lakini yasiwe ndio sehemu kuu ya jukwaa la elimu.
Jukwaa lazima libebe maana halisi ya elimu na si kwasababu tu!
Katika dunia ya sasa elimu siyo diploma,degree za uzamili au uzamivu. Elimu ni namna gani utaweza kukabiliana na mazingira magumu ya ushindani. Kwa sasa tumeanza na soko la pamoja la EAC lakini pia sisi tukiwa kama sehemu ya dunia tunachanganyika na watu wa mataifa mengine. Kuna fursa nyingi tu zinazoweza kubadilisha maisha yetu.
Mathalani, nimesoma mara nyingi watu wakiuliza kozi gani bomba au inalipa. Ukweli wa mambo ni kuwa kila kilichopo duniani ukiweza kukitumia vizuri na kwa maarifa kinalipa. Lakini pia lazima uelewe kuwa milango haipo wazi kana kwamba utaweza kupata kila kitu kama unavyotaraji.
Kozi kama za ualimu watu wengi wanaziona kama hafifu lakini hawajui kuwa ndizo kozi zenye milango mingi sana na zinazoingiliana na kozi nyingine kwa namna moja au nyingine. Nitumie msemo wa mitaani kozi ya ualimu ni kama 'funguo malaya' inayoweza kufungua kila mlango. Tatizo watu hawaangalii mambo kwa mtazamo mpana na hapo kuna kupotea kwa hali ya juu.
Ni lazima ujiulize pia endapo kozi 'bomba' unayoitaka katika maisha yako itaweza kukupa fursa!!.
Dunia imebadilika, kuna wasomi wengi wenye sifa wanazurura, sasa mwenzangu uliyehitimu juzi tu kama unadhani umefika ukweli ni kuwa hujafika.
Soko la ajira la sasa haliangalii Degree yako au GPA, linaangalia wewe kama mwajiriwa utaweka nini mezani kulisaidia shirika ua taasisi. Una ujuzi gani zaidi ya degree yako ambayo kila mtu anayo na wengine wanazo kutoka katika vyuo vyenye heshima.
Ikifika hapo kuna mambo yanajitokeza:
1. Una kitu gani kinachokutofautisha na washindani wako wengine? Nafasi moja ya kazi inaweza kuwa na candidates 300, sasa kwanini wewe uajiriwe na si Mr au Miss X ambaye licha ya ukubwa wa degree yake lakini pia anauzoefu kukuzidi. Wenye lugha zao wanasema 'how do you stand out of the crowd'.
2. Unawezaje kujiuza kwasababu nyote mliopeleka CV mnabidhaa ile ile, sasa kwanini waajairi wadhani bidhaa zako ni bora zaidi ya zile 299 zilizojitangaza kuwania nafasi hiyo.
Hapa kunaingia vitu vingine kama ifuatavyo:
a)Ni kwa vipi CV yako imeweza kupenya na kuwa short listed katika zile 10, kutoka zile 299 kwa ajili ya Interview.
Kumbuka usipokuwa short listed basi huna interview na huna kazi hata kama una degree zako na GPA safi.
Kwahiyo unatengenezaje CV (Resume) yako ili ukubalike katika kuingia katika 10 bora ni muhimu sana.
b) Katika 10 bora watakaoitwa katika interview utawezaje kuwashawishi jopo la watahini ili uwe ndani ya 3 bora?
Hapa ndipo mbinu za interview zinapokuja.
Hapa nimejaribu kutoa tu muhtasari wa namna gani dunia inakuwa ya ushindani hata kama una nondo zote.
Ninachotaka kusema hapa ni kuwa, kuwa na Bachelor, master au PhD bado hakujakuhakikishia makali katika ushindani wa dunia ya leo. Ni jinsi gani unajiuza na unaweza kuuza hizo degree zako ni muhimu sana.
Tena teknolojia imesonga mbele hizo CV zinachaguliwa kwa computer, sasa hapo suala la kujuana 'technical know who' halipo. Matokeo ya yote utaishia kukimbilia ukabila na udini wakati ukweli ni kuwa hujui kujiuza au kuuza bidhaa zako.
Hebu tuangalie mambo yaliyosemwa hapo juu, kozi, kuandika CV, kufanya Interview n.k
Wenye jukwaa kama mtaridhia basi tutaendelea kudadavua kwa kiasi tunachoweza ili kupeana maarifa.
Noamba kutoa hoja.