Dunia isiyo sawa

ngoshwe

JF-Expert Member
Mar 31, 2009
4,131
931
attachment.php


Tukiwa katika hali nzuri kimaisha, tunapokula milo zaidi ya mitatu kwa siku na kusaza, ltunapo lala kwenye mahekalu ya zaidi ya lile la Mfalme Suleiman, tunapougua kidogo lakini tunajitibu kwa gharama kubwa, watoto wetu wanaposoma kule ambapo ada inazidi ile ya chuo kikuu, wake au waume zetu wanapoenda kwenye saloon ambazo huduma ya kuremba nywele inazidi ya kodi ya nyumba ya mwezi kwa baadhi ya wanadamu wenzetu, tushukuru Mungu na katika hilo tutumie fursa na Baraka ambazo Mungu ametujalia na tuwakumbuke na wale walio kama hawa!!!
 

Attachments

  • KID in HARDSHIP.jpg
    KID in HARDSHIP.jpg
    50.5 KB · Views: 365
Na je umeshamwona mgombea flani tajiri sana akijipitisha kwa wapiga kura wake walio masikini kwa 95%. Ulimuona anavyojifanya kuyafahamu matatizo ya wapiga kura wake hao?na jinsi alivyo hodari kuyaainisha,yes mi nimeona mgombea ubunge. Aki jaribu kutoa mchanganuo wa jinsi atakavyo jitahidi kutatua tatizo sugu la maji kwa kuwachimbia visima vitatu na jinsi atakavyoomba misaada ili kupata vijisenti kidogo vya kukarabati banda moja la kijiji ili liweze kutumika kama zahanati ikiwa ni kipindi cha mwisho cha uwakilishi. Na wakati wote huo mgombea huyu alikuwa kasimama juu ya Lexus yake huku mtoto wake akiwa kaketi juu ya bonet la HUMMER. Baada ya blaablaa tukampigia makofi tukamwimbia mapambio akaenda zake sisi tukaendelea kuumiza kichwa namna ya kupata maji japo ya kukorogea uji tunywe tulale.the world is absolutely fair, we are extremely unfair.
 
Africa bana....usawa gani mnaozungumzia. Mimi naona uchafu kwenye hiyo picha, ukiwa unanjaa au maskini sio lazima inzi wakutambaeee.
 
Back
Top Bottom