Dunia ina Umri gani? Mabillioni, Mamillioni, Malaki au Maelfu?

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Jul 22, 2011
3,752
5,497
hoe-oud-de-aarde.jpg

???????

Swali hili ni Muhimu sana hasa dunia ya leo maana limeigawa katika vipande viwili ambavyo havina ukaribu wala ufanano hata chembe.

1:Wanaoamini Dunia iliumbwa(Creationists) - Dunia ina umri wa miaka takribani 6000 (maelfu).Pia kunadhana ndogondogo zinazoendana na hii.

2:Wanaoamini Dunia iliibuka (Evolutionists) - Dunia iliibuka Takribani miaka Bilioni 4.6 na maisha kuanza miaka Billioni 3.5 iliyopita.Pia kuna dhana takribani saba za uibukaji.

Haya ndio Matokeo ya Hii mitazamo miwili.
1: Kama dunia ni changa (Miaka kama 6000) Basi Dhana ya uibukaji EVOLUTION inakufa hapohapo. Somo kwamba tulitokana na Sokwe linafia hapo hapo.​

2: Kama Dunia imezeeka na inaumri wa miaka Billioni 4.6 basi, Dunia haikuumbwa na chochote kuhusu uumbaji ni stori zisizo sawa. Na ikumbukwe bila tukio hili ktuokea kwa mabillioni ya miaka tena kidogo kidogo hii dhana inakufa rasmi.
Vipimo Vya miaka.
1: EVOLUTION; Hapa wanatumia Carbon dating au Radiometric Dating (Ni njia ambazo ili zifanye kazi inabidi ujumuishe na MAKISIO/ASSUMPTIONS), Yawezekana kuna mengi zaidi pia.

2:CREATION; Hapa inatumika Umri wa watu hasa waliozaliwa baada ya adam,Historia,Utafiti na nyaraka za kale na kwenda hadi kufika leo tulipo.Yawezekana kuna mengi zaidi pia

Karibuni kwa changamoto fikirishi,
always am a Winner Kiranga gasgas Nyani Ngabu CHARMILTON tejateja Apollo Iceman 3D UHURU JR Kikwajuni One Behaviourist Stefano Mtangoo Hb wa Ilala Kahtan Ahmed Vivax Warrior faiz MALCOM LUMUMBA na wengine wengi...

Dondosha hapa chochote unachoamini au kujua kuhusu haya mawili. Ninaamini hakuna ambaye yuko pande zote mbili kwani hazichangamani.

Ukitoa na reference, illustrations, Quotes, links, chochote kile Kumtetea Adam au Homosapiens na makazi yake tutashukuru
 
Hadi sasa bado haijajulikana wepi ndio wapo sahihi,na inawezekana hadi vizazi vitafutika duniani na jibu lisijulikane.
 
Mimi moja kwa moja napingana na CREATIONISM kwa maana haina mantiki.Nasema haina mantiki kwa sababu inatuachia maswali yasiyo na majibu na kutulazimisha tuiamini badala ya kuielewa.Mimi nina maswali yafuatayo kuhusu CREATIONISM.

1.Kama watu wote walitokea sehemu moja(mf.Mashariki ya kati), ni technologia ipi iliyotumika kusambaza watu kutoka mashariki ya kati kwenda maeneo mbalimbalina ya Dunia kama Chile, Madagascar n.k?
walivukaje bahari? Kama walisafiri, kwa nini wasingekuwa wanawasiliana kwa safari za mara kwa mara? Kwa nini kina V.Da Gama, C.Columbus wawe wagunduzi wa maeneo mengine? ina maana waliamini Dunia ni maeneo walimoishi pekee?

2.Kama tumetokana na Baba na Mama mmoja, kwa nini watu tunatofautiana sana? nini sababu na mechanism iliyosababisha wawepo watu weupe na weusi? Miaka 6000 inatosha kuruhusu mabadiliko makubwa tunanoyashuhudia ya tofauti miongoni mwa jamii za watu wa hii Dunia?

3.Kwa nini kuna mabaki ya kale yenye umri zaidi ya miaka milioni? kwa nini hayo mabaki hayapatikani nje ya Africa? Kwa nini fossils zinaonesha 'Life complexity' inaongezeka kutoka matabaka ya chini kuja matabaka ya juu ya miamba?

4.Kwa kuwa Watu waliumbwa kutokana na udongo, ni material yepi yaliyotumika kuumba viumbe wengine kama wanyama na mimea? Mbona watu wanafanana sana na hawa viumbe wengine?

5.Ukowapi ushahidi/mabaki ya bustani ya Eden, masalia/makaburi ya Adam na Eva?
Yako wapi masalia ya safina ya Nuhu? Mbona Palaeontology haioneshi kama mafuriko ya Dunia nzima yamewahi kutokea na kuua watu?

6.Kwa nini vitabu vya dini havizungumzii uwepo wa sayari nyingine?, Kama hizo Sayari ziliumbwa na Mungu, ni za kazi gani?

7.Kama Mungu ndiye muumbaji wa kila kitu, kwa nini aumbe viumbe hatarishi kwa watu wake kama vile; Virus, bacteria na Fungus wenye kusababisha magonjwa na vifo kwa watu? Mungu mwenye upendo wote anaweza kuumba vyanzo vya matatizo kwa watu wake?

8.Kwa nini miili ya viumbe vya Mungu iwe na vestigial organs?

9.Kwa nini Mungu aumbe Dunia yenye majanga asilia kama matetemeko ya nchi, mafuriko, vimbunga na milipuko ya volcano? Intelligent designer anaweza kuumba dunia yenye majanga kama hii ya kwetu?

10.Kwa nini Mungu alisikitika na kuhuzunika baada ya kumuumba Binadamu(Mwa.6:5-8)? Mungu gani mjuzi wa yote afanye jambo la kumsikitisha na kumhuzunisha siku za mbeleni?
 
Kwa mujibu wa data zilizopatikana kwa satellite ya wmap pamoja na ile COBE ambazi zilikuwa zinatafiti background radiation zilionyesha universe ina miaka 14 bil, nakubariana na scientific kuliko kuliko hiyo ya miaka 6000, dini ya kale kabisa kwa data zilizopo ni wa Hinduism na maandiko yao yanaspan zaidi ya miaka ya hiyo miaka 6000 haingii akilini dunia kuwa na miaka 6000.
 
Estimation za bible ni chaka... hawana records... cha ajabu wameshindwa hata kumuuliza yesu hilo swali ambae ndio mungu wao... hivi haya maswali tunayouliza leo kwanin hakuulizwa yesu ayatolee majibu?? Alafu kuna watu watuambia kila siku kwamba wameongea na Mungu.. why amumuulizi maswali haya awape majibu???
 
Huu ni mtihani mwingine. Ila cha msingi ni lazima tujue kuwa;
1. Shetani yupo
2. Shetani anapingana na Mungu
3. Shetani ana nguvu na akili nyingi sana.

Kutokana na hayo, ni rahisi kwa shetani kulazimisha wanasayansi waongee wanachoongea, au kubadilisha ukweli kuwa uongo na uongo kuwa ukweli. Maswali yapo mengi mnoooo tena mno, lakini hayana majibu. Kukosa majibu hakumaanishi kuwa Mungu hayupo au uumbaji siyo sahihi.

Mimi ninaamini uumbaji kwa kuwa ni neno la Mungu lilioandika.
 
Napingana na Bible, maana utafiti wake hauna mantiki na umejikita zaidi kwenye kuamini(imani)

Imani iko 50/50, inaweza ikawa kweli au isiwe hivyo basi bible inaongopa.

Big Bang imetokea kati ya miaka billion 12 mpaka 14
Iliyopita. To put this in perspective, the Solar System is thought to be 4.5 billion years old and humans
have existed as a genus for only a few million years. Astronomers estimate the age of the universe
in two ways:
1) by looking for the oldest stars; and
2) by measuring the rate of expansion of the
universe and extrapolating back to the Big Bang; just as crime detectives can trace the origin of a
bullet from the holes in a wall.
 
Biblia iko sahihi kabisa kuhusu maelezo yake. Watu ndio wapo kimakosa katika tafsiri zao. Biblia haijawahi sema kuwa dunia ina miaka kama elfu sita kuja saba kwa sasa ila miaka hiyo ni ya kuanzia Adamu.
Lakini kabla ya Adamu kuumbwa kulikuwa na miaka mingi huko nyuma ya kuumbwa kwa ulimwengu ikiwepo na dunia ndani. Yawezekana ni mamilioni au mabilioni ya miaka, maana maandiko yanasema kwamba "hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi" ,nukta; sasa baada ya kuziumba mbingu na nchi haijulikani alikaa mdagani kabla ya Roho wa Mungu kutulia sasa katika uso wa maji aliyoyaumba hapo kwanza na kuanza kuikarabati kwa ajili ya kuuweka uhai juu yake. Hapo ndipo sasa anatenga maji na nchi kavu na kisha kuweka viumbe hai.
Pia ijulikane kuwa mtu wa mwili wa nyama, yaani Adamu ndie kiumbe wa mwisho kuumbwa. Kwa wale wa nadharia ya uumbaji wa Mungu kuwa katika siku saba kwa mfano uliopo wa siku saba za juma za kawaida ya binadamu ndio kabsaa hawawezi kamwe kuupata uumbaji jinsi ulivyokuwa kwa kina.
 
Biblia iko sahihi kabisa kuhusu maelezo yake. Watu ndio wapo kimakosa katika tafsiri zao. Biblia haijawahi sema kuwa dunia ina miaka kama elfu sita kuja saba kwa sasa ila miaka hiyo ni ya kuanzia Adamu.
Lakini kabla ya Adamu kuumbwa kulikuwa na miaka mingi huko nyuma ya kuumbwa kwa ulimwengu ikiwepo na dunia ndani. Yawezekana ni mamilioni au mabilioni ya miaka, maana maando yanasema kwamba "hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi" ,nukta; sasa baada ya kuziumba mbingu na nchi haijulikani alikaa mdagani kabla ya Roho wa Mungu kutulia sasa katika uso wa maji aliyoyaumba hapo kwanza na kuanza kuikarabati kwa ajili ya kuuweka uhai juu yake. Hapo ndipo sasa anatenga maji na nchi kavu na kisha kuweka viumbe hai.
Pia ijulikane kuwa mtu wa mwili wa nyama, yaani Adamu ndie kiumbe wa mwisho kuumbwa. Kwa wale wa nadharia ya uumbaji wa Mungu kuwa katika siku saba kwa mfano uliopo wa siku saba za kawaida ya binadamu ndio kabsaa hawawezi kamwe kuupata uumbaji jinsi ulivyokuwa kwa kina.
Kitabu cha Mwanzo, nadhani ndicho kitabu kibovu kabisa kwenye Bible.

Hakina logic, ni contradiction mwanzo mwisho.

Kitabu cha mwanzo kinasema kwamba watu waliumbwa baada ya kuumbwa kwa mimea na wanyama,wanyama waliumbwa[Mwa.1:11-24], kisha watu mke na mume wakaumbwa kwa pamoja [Mwa.1:26-31]
Yaani kwenye hizoo nukuu, Mungu aliumba wanyama na mimea halafu watu wakawa wa mwisho kuumbwa.Kwenye hizo nukuu, Bibilia inasema mwanaume na mwanamke waliumbwa kwa wakati mmoja.

Sehemu nyingine ya kitabu cha Mwanzo inaeleza kwamba mtu aliumbwa kabla ya kuumbwa kwa wanyama.
Kitabu kinasema Mungu almuumba Adam kwanza[Mwa.2:7], halafu mimea ikaoteshwa baada ya kuumbwa kwa Adamu[Mwa.2:8-9].....Halafu wanyama wakaumbwa baada ya kuumbwa kwa Adamu[Mwa.2:18-19]

Halafu Eva akaumbwa mwishoni baada ya kuumbwa kwa Adam, mimea na wanyama[Mwa.2:21-23]

Hivi kweli kitabu chenye mikanganyiko kama hii unaweza kukitumia kama njia ya kujifunza chanzo cha uhai?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom