Engager
JF-Expert Member
- Jan 12, 2011
- 1,273
- 2,648
Imepungua kwa Albino sasa imehamia kwa wanaume!!
"Uchawi mpya umeibuka nchini Zimbabwe ambapo mbegu za uzazi za wanaume zimekuwa dili kiasi cha kundi la wanawake kuwabaka wanaume na kisha kuiba mbegu zao za kiume. Habari za wanaume kubakwa zimetangazwa ktk miji ya Harare, Gweru na Mashonaland. Wanawake watatu wametiwa mbaroni katika mji wa Gweru kutokana na matukio ya kuwabaka wanaume waliyoyafanya hivi karibuni. Wanawake hao walikamatwa ktk gari lao ambalo wamekuwa wakilitumia kama chambo cha kuwavuta wanaume kwa kisingizio cha kuwapa lifti. Ndani ya gari kulikutwa kondom 33 ambazo zilikuwa na mbegu za kiume za wanaume tofautitofauti. Wanaume wanapo kubali kupewa lifti, hutekwa kwa bunduki na kupelekwa sehemu za mbali ambako hulazimishwa kufanya mapenzi na wanawake hao kwa kutumia kondom au wakati mwingine bila hata kinga huku wakiwa wameelekezewa bunduki. Baada ya hapo wanawake hao hukusanya mbegu za kiume na kisha kuwatupa wanaume hao pembeni ya barabara. Wanawake hao wamekuwa wakizikusanya mbegu hizo za kiume na kuzitumia ktk masuala ya kishirikina".
Haya sasa! Sipati picha haya mambo yakiingia bongo nadhan hakutakuwa na haja ya mtutu...lol
"Uchawi mpya umeibuka nchini Zimbabwe ambapo mbegu za uzazi za wanaume zimekuwa dili kiasi cha kundi la wanawake kuwabaka wanaume na kisha kuiba mbegu zao za kiume. Habari za wanaume kubakwa zimetangazwa ktk miji ya Harare, Gweru na Mashonaland. Wanawake watatu wametiwa mbaroni katika mji wa Gweru kutokana na matukio ya kuwabaka wanaume waliyoyafanya hivi karibuni. Wanawake hao walikamatwa ktk gari lao ambalo wamekuwa wakilitumia kama chambo cha kuwavuta wanaume kwa kisingizio cha kuwapa lifti. Ndani ya gari kulikutwa kondom 33 ambazo zilikuwa na mbegu za kiume za wanaume tofautitofauti. Wanaume wanapo kubali kupewa lifti, hutekwa kwa bunduki na kupelekwa sehemu za mbali ambako hulazimishwa kufanya mapenzi na wanawake hao kwa kutumia kondom au wakati mwingine bila hata kinga huku wakiwa wameelekezewa bunduki. Baada ya hapo wanawake hao hukusanya mbegu za kiume na kisha kuwatupa wanaume hao pembeni ya barabara. Wanawake hao wamekuwa wakizikusanya mbegu hizo za kiume na kuzitumia ktk masuala ya kishirikina".
Haya sasa! Sipati picha haya mambo yakiingia bongo nadhan hakutakuwa na haja ya mtutu...lol