Du kumbe na jirani yangu ni changuduoa anajiuza

Pole please find a way to talk through ili awe huru tena kwako, Noma hiyo kaka.


Jamani ukistaajabu ya Musa utaona sijui ya nani, mwenzio nimepata aibu ya mwaka nikiwa na mama mkwe wangu. Kwa kifupi ni kwamba nilikua nimetembelewa na mama yangu mkwe kutoka huko Katavi mkoa mpya na kwa bahati mbaya ndo mara yake ya kwanza kuja Dar. Kutokana na mihangaiko ya kazi za mchana na ratiba kuwa tight siku za weekend na siku za weekdays sikufanikiwa hata siku moja kumtoa dina, juzi usiku ikabidi twende zetu dina mimi mke wangu na mama mkwe maeneo ya posta maana yeye alikua anaondoka siku inayofuata yaani jana kurudi Katavi. Sasa tukawa tumechelewa kutoka mpaka kwenye saa nne na nusu usiku, wakati wa kurudi njiani maeneo ya Africa Sana – Sinza tukapata pancha nikawaambia mke wangu na mama mkwe wakae kwenye gari tu ili nitafute kijana maeneo ya standi ya daladala Africa sana au hata pale kwenye kituo cha mafuta anisaidie kubadilisha tairi hata kwa kumlipa maana sikutaka kuchafua suti yangu.

Ile kushuka ndani ya gari kutembea tu hatua kama tano nikavamiwa na machangu kama wawili wote wakafikiri nataka huduma kumbe mimi natafuta kijana wa kunisadia kubadilisha tairi. Lakini kilichonistua ni kumwona dada ambae ni jirani yangu na pia tunafanya nae ofisi za karibu maeneo ya mjini nae akiwa miongoni mwa wale wasichana wawili waliokuwa wanafikiri nataka huduma.Alivoniona alijiskia vibaya alitamani ardhi ipasuke. Sasa mimi sielewi hivi wasichana wanajiuza for only finding satisfactions, au shida za maisha au ni hulka tu ya wasichana? Nasema hivo kwa sababu huyo dada ana kazi nzuri tu ingawa sijui mshahara wake lakini kazi yake inaweza kumfanya aishi mjini bila wasi wasi. Nimekutana nae leo wakati naelekea lunch yaani hana amani hata kidogo lakini mimi nayachukulia kama mapito.
 
wanawake hujiuza kwa kuwa wanajua wapo wa kuwanunua...mtu huwezi fanya biashara kafir, lazima kuna faida hapo.
 
very true
ma cd ni weengi kuliko unavyoamini


Ha ha ha ha. Ninao ushuhuda mwingine unaohurumia hawa tunaowaita machangu.

Kuna mtu fulani katika idara moja muhimu sana katika serikali ya tz nadhani alihisi hapendeki machoni pa wale tunaodai warembo. Huyu kijana alikuwa kakamilika tu katika yale maeneo akawa anapata shida sana jinsi ya kufanya na lile itaji linapochemka.

Kilichotokea kijana huyu mwenye kipaji sana katika mambo ya vitabuni, alianza kutembelea maeneo ya vilabu vya pombe za kienyeji kwenye eneo moja linaitwa Iyunga katika jiji la Mbeya. Ni miaka ya 1970 hapo--somewhere mwishonimwishoni hivi.

Akiwa kule kakumbana na muuza pombe mmoja inasemekana alikuwa anagawagawa ivi. Boom! siku ya kwanza kurudi naye kambini kesho katoa uzuru kazini. Siku ya tatu kaenda staff room na taarifa kwa wenzie, jamani ee, mwenzenu mke nimepata.

Huyu bwana kabila yake Mchaga. Muuza pombe Mnyakyusa. Wanaijua hii familia wanasema ni familia imara sana yenye watoto wenye akili, hekima na busara sana.

So you see: kama ulivyosema awali boss, hawa binadamu wengine wanajiingiza katika ile shuhuli kwa frustration tu. Otherwise some of them are very good people. Of course ni lazima ubahatike kukumbana na huyo good people kwenye kundi. Ingawa nayo hiyo ina namna nyingine ya kuiangalia: kwani ni kundi gani la binadamu halina good people na bad people.... Lipi?
 
namshangaa.

Hajui kuna siku atamfaa wakati wa jua afu kwa mkopo au offer ya promosheni tu.

Haahaahaahaa:) Hii ya offer ya promosheni imenikuna sana! Unaoata ya promo kisha kesho unakopa kupitia karata ya ujirani mwema!
 
mkuu mwenzio nnapoishi kuna ka nyumba kadogo uani, kuna cd wa uswazi kapangishiwa na mbabu mme wa mtu, kwanza kuongea hajui si unajua wanawake wa uswahilini full makelele, akiingia na wenzie getini kama sokoni. Huyo mbabu na yeye shida tupu mpunga wenyewe mbuzi akitoka saa nne usiku kurudi kwa mkewe, huyo cd ndo anajitayarisha kutoka ikifika saa sita usiku anadaka bajaj kitu san ciro anakwenda tafuta mingo. Kurudi saa tisa kumi. Akiamka sasa anawapigia simu ma cd wenzie utasikia jana sijapata chochote yaani kila nikijitahidi kaudaka wanataka kwa buku au mia tano, watu hawana pesa siku hizi. Namuonea sana huruma yule babu sijui anatafuta maradhi ukubwani
 
Mbona ya kawaida hayo yasikupe mawazo sana, sisi mbona tumepanga nao nyumba moja mama na mwanae Wote biashara yao ndio hiyo, walifanya siri ila baadaye siri ikafichuka baada ya kugombania bwana mmoja hatimaye wakachambana usiku kucha na huyo mama anaishi na mme wake mwanaume anafanya kazi bandari.
 
Mbona ya kawaida hayo yasikupe mawazo sana, sisi mbona tumepanga nao nyumba moja mama na mwanae Wote biashara yao ndio hiyo, walifanya siri ila baadaye siri ikafichuka baada ya kugombania bwana mmoja hatimaye wakachambana usiku kucha na huyo mama anaishi na mme wake mwanaume anafanya kazi bandari.

Mama changu na binti changu..lol
Hapo lazima kieleweke tu..na hzo za kushare mabwana mbona watashare sana!
 
accoording to my analysis: watuwengi hawapendi kutegemea mshahara mmoja, hii inapelekea watu kuwa wabunifu na kuwa na entrepreneur mind set... my take huyo jirani yako hapo kajiajiri.
 
Somo la leo-mpe offa alafu chukua time zako
atakuwa huru na wewe utaweka akiba shemeji akienda Katavi wewe utakwenda Kavita
 
Ah! wewe aibu ipo wapi hapo? Hilo chimbo jipya mzee, kulijua tu ni hazina hiyo itakusaidia baadae.
 
mi ningependa kujua nani alikaa mbele kati ya mama na mke hata mimi nina ugeni soon

hivi seat ya mbele ina umuhimu wake? ndio maana niliwahi kukuta madiwani walikuwa na safari ya kikazi wakawa wanagombania kiaina seat ya mbele.
 
The oldest business in the world here comes again..
I always find difficult to blame prostitutes while there are men all around looking for and hook them up..
Stop chasing them and automatically this business will impulsively be limped off..
But as long as you appreciate their work don't be surprised to see even King's daughters hustling!!!

Very True.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom