WanaJF
Ni ukweli ulio wazi kwamba watawala wanapata hofu kuu kwa sasa kila wakisikia neno CHADEMA.Hakika wanaweweseka.Kiwango cha umma kuunga mkono chama pinzani katika historia ya Taifa hili kwa sasa tunashuhudia CHADEMA ikivuka mipaka ya kupendwa! Fantastic!
Wachambuzi wa mambo tunajiuliza kuna nini? Hata hivyo bila shaka yoyote CHADEMA kwa sasa kimejipambanua kama wakili na mtetezi mkuu wa wananchi wa Taifa hili.Watanzania wa leo si wajinga wanaona.Ukitazama bunge huhitaji kuwa msomi kujua ni chama kipi kinatetea wanyonge wa Taifa hili.Ni CHADEMA.
Nimefanya utafiti wangu binafsi katika mikoa mitano.Shinyanyanga,Rukwa,Lindi,Mwanza na Singida.Kila mkoa tumehoji watu 50 na jula ya mikoa 5 tumehoji watu 250.Pamoja na mambo mengine kulikuwa na swali tuliwauliza watu.."NI CHAMA KIPI UNACHOKIONA NI MTETEZI WA KWELI WA MATATIZO YA WANANCHI NA UNACHOONA KINAFAA KUONGOZA TAIFA TUKAPATA MAFANIKIO?" Majibu ya swali hili yaliniacha mdomo wazi kama ifuatavyo: Shinyanga waliosema CHADEMA ni 41,Rukwa CHADEMA ni 36,Lindi CHADEMA ni 31,Mwanza CHADEMA ni 46 na Singida CHADEMA ni 38.Vyama vingine vyote ikiwemo CCM waligawana kura zilizobaki katika watu 50 waliohojiwa katika kila mkoa.Watu watashangaa nilikuwa nafanya utafiti wa nini-Hakika nilikuwa nafanya Research kwa ajili ya Masters degree yangu ninayokamilisha ya mambo ya siasa.Huo ndiyo mtizamo halisi wa umma.
Kwa upande mwingine nguvu ya CHADEMA inazidi kupaa kutokana na watawala kuihofia mno kupita kiasi.Vitendo wanavyofanya kulitumia jeshi la polisi kuzuia harakati za kisiasa huku wakiwaua kwa risasi wafuasi wa CHADEMA ni sawa na kuchochea moto wa kuzidi kupendwa na kuonewa huruma na jamii.
Tunafahamu majemadari wawili wa chama hicho Dr Wilbroad Slaa na Freeman Mbowe wanapita katika kipindi kigumu sana kwa sasa.Wanajua watanzania wanawatizama kama tumaini pekee la kuipeleka nchi katika neema.Pia wanafahamu wanatakiwa kuchukua nchi kwa amani na salama bila umwagaji damu.Viongozi hawa wakitizama vitisho na mauji ya polisi dhidi yao huku wakiona kundi la watanzania milioni 40 likiwa nyuma wanaona mambo mawili makubwa.Kwanza wanapata moyo na Ari lakini hata hivyo kwa vile wao ni wanadamu kama wengine akili ya kukata tamaa pia inawajia.Hii ni kwa sababu kamba hukatikia pembamba.Hata hivyo sisi wananchi tunawatia moyo mashujaa hawa kwamba wasikate tamaa,waongeze juhudi kwa sababu kumeshapambazuka sasa na siku si nyingi watalihutubia Taifa wakitokea magogoni baada ya uchaguzi!.
WanaJF nawakilisha.
Ni ukweli ulio wazi kwamba watawala wanapata hofu kuu kwa sasa kila wakisikia neno CHADEMA.Hakika wanaweweseka.Kiwango cha umma kuunga mkono chama pinzani katika historia ya Taifa hili kwa sasa tunashuhudia CHADEMA ikivuka mipaka ya kupendwa! Fantastic!
Wachambuzi wa mambo tunajiuliza kuna nini? Hata hivyo bila shaka yoyote CHADEMA kwa sasa kimejipambanua kama wakili na mtetezi mkuu wa wananchi wa Taifa hili.Watanzania wa leo si wajinga wanaona.Ukitazama bunge huhitaji kuwa msomi kujua ni chama kipi kinatetea wanyonge wa Taifa hili.Ni CHADEMA.
Nimefanya utafiti wangu binafsi katika mikoa mitano.Shinyanyanga,Rukwa,Lindi,Mwanza na Singida.Kila mkoa tumehoji watu 50 na jula ya mikoa 5 tumehoji watu 250.Pamoja na mambo mengine kulikuwa na swali tuliwauliza watu.."NI CHAMA KIPI UNACHOKIONA NI MTETEZI WA KWELI WA MATATIZO YA WANANCHI NA UNACHOONA KINAFAA KUONGOZA TAIFA TUKAPATA MAFANIKIO?" Majibu ya swali hili yaliniacha mdomo wazi kama ifuatavyo: Shinyanga waliosema CHADEMA ni 41,Rukwa CHADEMA ni 36,Lindi CHADEMA ni 31,Mwanza CHADEMA ni 46 na Singida CHADEMA ni 38.Vyama vingine vyote ikiwemo CCM waligawana kura zilizobaki katika watu 50 waliohojiwa katika kila mkoa.Watu watashangaa nilikuwa nafanya utafiti wa nini-Hakika nilikuwa nafanya Research kwa ajili ya Masters degree yangu ninayokamilisha ya mambo ya siasa.Huo ndiyo mtizamo halisi wa umma.
Kwa upande mwingine nguvu ya CHADEMA inazidi kupaa kutokana na watawala kuihofia mno kupita kiasi.Vitendo wanavyofanya kulitumia jeshi la polisi kuzuia harakati za kisiasa huku wakiwaua kwa risasi wafuasi wa CHADEMA ni sawa na kuchochea moto wa kuzidi kupendwa na kuonewa huruma na jamii.
Tunafahamu majemadari wawili wa chama hicho Dr Wilbroad Slaa na Freeman Mbowe wanapita katika kipindi kigumu sana kwa sasa.Wanajua watanzania wanawatizama kama tumaini pekee la kuipeleka nchi katika neema.Pia wanafahamu wanatakiwa kuchukua nchi kwa amani na salama bila umwagaji damu.Viongozi hawa wakitizama vitisho na mauji ya polisi dhidi yao huku wakiona kundi la watanzania milioni 40 likiwa nyuma wanaona mambo mawili makubwa.Kwanza wanapata moyo na Ari lakini hata hivyo kwa vile wao ni wanadamu kama wengine akili ya kukata tamaa pia inawajia.Hii ni kwa sababu kamba hukatikia pembamba.Hata hivyo sisi wananchi tunawatia moyo mashujaa hawa kwamba wasikate tamaa,waongeze juhudi kwa sababu kumeshapambazuka sasa na siku si nyingi watalihutubia Taifa wakitokea magogoni baada ya uchaguzi!.
WanaJF nawakilisha.