Dr. Willbroud Slaa on his TWITTER account today!

Status
Not open for further replies.
Ficha upumbavu wako, usifiche hekima yako.

Leteni mapesa arusha tule CCM tukalale Chadema.

Tehe tehe tehe tehe! Kwi kwi kwi kwi kwi. Hapa arusha mjini CCM hamna chenu Rejao, hata kama chadema watasimamisha jiwe litapita kwa kishindo! Tunawasubiri kwa hamu kubwa! Natamani uchaguzi ungekuwa kesho!

Pole sana Sweetlady,
Mcheki jamaa alivyochoka gafla!!
lema.jpg
 
A way forward ni kuwa kitu kimoja CDM kuna shutma zinaizonga pengine ni propaganda tu za wenye kuchukia maendeleo ya CDM lakini hakuna hata siku moja CDM imekanusha au kutolea maamuzi ambayo yatawafanya watu wapuuze shutma hizo.
1. Kuwa CDM ni chama cha kikanda na hata wabunge wake wengi ni wa kutoka kanda fulani.
2. CDM ina mkono wa kanisa (hapa nakumbuka shutma dhidi ya CUF wao walikuwa wanazikanusha ila kwa bahatio mbaya au sijapata kusikia popote CDM wakikanusha hili)

Mabadiliko yatapatikana watanzania wakiwa wamoja bila kujali kanda zao/koo zao wala dini zao je CDM wapo tayari kuonyesha njia?
Mkuu sikiliza hapa; Freeman Mbowe akiongea na Watanzania waishio nchini Marekani Februari 4, 2012 pt 4 - YouTube
 
Upo Karatu, meru au Moshi? huko ndiko zipo highly demanded! Kwingine hamna mtu anataka kukisikia hicho chama
Wewe wasema! Mbeya, Kigoma,Dar,Tarime,Iringa na Mwanza nako ni kaskazini sio ?!
 
Lema alipata kura 2010 kwa sababu watu walikuwa hawamfamu. Kwa kipindi hiki cha mwaka na nusu watu wamemfahmu Lema ni mtu wa aina gani. Wameona matatizo aliyowaletea, vurugu za kila siku na kurudi nyuma kwa maendeleo ya Jimbo la Arusha mjini. Kwa sasa hawawezi kurudia tena kosa walilolifanya 2010. Watu wengi sana wamefurahia uamuzi wa maahakama...at last wameondoka na matatizo!!

Mkuu kaka yako BARUBARU yuko wapi au kabadili ID?
 
Kwenye Twitter kuna jamaa anaitwa Yericko Nyerere (member JF) ametweet ''CCM mnaruka sarakasi huku mmejifunga taulo, mtaweza?''
 
"Maendeleo hayaletwi kwa kubahatisha, bali huletwa na mabadiliko, wewe na mimi(sisi) ndo tunaotakiwa kuleta mabadiliko"(nimeitafisiri kwa kiswahili, mtaniwia radhi kama nitakuwa nimepotosha). !

Mkuu unajua tena mambo ya lost in translation.., naona bora ungeiacha kama ilivyo ili kutokupoteza maana au ungeweka kama ilivyo na kuitafsiri pia
 
Hapana. Tupe Link, sina imani na hii, maana hata mimi kwenye page yake imekwenda
It does not matter, nani ameandika haya. ukweli ni kwamba ni ya hekima! tukae mkao wa kazi kuwaaibisha mafisadi tena!
 
DR. SLAA KATIKA TWTTER: Maneno yaliyoelezwa kuhuhusu kuchoshwa na maisha ya sasa kama elimu duni, kupanda kwa garama ya maisha kwa 150%, wanyonge kunyanyaswa pasipo huruma, umasikini uliokithiri kuzidi kulemea mamilioni kwa mamilioni ya Wa-Tanzania. nchi kutawaliwa na mabwenyenye wenye uroho wa mali na madaraka. machungu anayopata tanzania wa kawida, huwezi ukaeleza ukamaliza. Tanzania litaendelea kujigaragaza ndani ya giza kuu bila kujua hatima yake endepo CCM ikiendelea kuwemo madarakani. mapambazuko yatakuepo pale tu upinzani utakapochukuwa hatamu ya uongozi. MEE WETU CCM AMEZEEKA ANAHITAJI KUSTAAFU.
 
Machungu ya mtanzania kutokana na utawala ulopo hauwezi ukaelezeka (beyond tongue can tell) k.m kupanda kwa gharama ya maisha kwa kiwango kinachozidi 150%,umaskini uliokithiri kuendelea kumlemea mtanzania, utawala wa mabwenyenye wenye uchu wa mali na madaraka kuendelea kushamiri, kila kunapokucha watawala walaghai kuwapamba wananchi kwa maneno matamu ya kufunika maovu yao (maisha mema kwa kila mtanzaia). Tutasema nini kuhusu tabaka la elimu!!! Shule za matajiri na watawala tofauti na za walala hoi sawa na wakati wa ubaguzi wa rangi enzi za mkoloni. Ajira ni janga kwa mtoto wa mkulima kwao wenye madaraka ajira tele. Ukithubutu kusema mabomu nje nje. Pole sana tanzania. Mzee ccm. Tunakuomba ukastaafu au la utastaafishwa kwa manufaa ya umma
 
Kenya wenzetu wameweza, sie bado tumelala wabongo bana!!

Kenya wameweza. Kuiondoa kanu lakini hakijabadili maisha yamtu alie masikini .maskini bado maskini na tajiri bado tajiri usifiki ukiiweka chadema ndio itaondoa umaskini wako kama hutajishuhulisha kutegemea chama kikuletee maendeleo yako umeumia
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom