Dr. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

Lucy Lameck alifariki baada ya kuugua muda mrefu. Alilazwa muda mrefu tu pale hospitali ya KCMC, lakini kwa hakika sifahamu ni nini kilichokuwa kikimsumbua.


Kithuku,

Huyu Lucy Lameck tena ni nani mie naona nimepita kapa hapo!
 
Lucy Lameck alifariki baada ya kuugua muda mrefu. Alilazwa muda mrefu tu pale hospitali ya KCMC, lakini kwa hakika sifahamu ni nini kilichokuwa kikimsumbua.

Maana kuna "taarifa" kwamba alikuwa na "uhusiano" na Rais wetu wa kwanza .... ??!! ... sijui kama naweza ku-connect dots hapa.
 
Kishoka,Kithuku,Kuhani,

..sidhani kama hao Wachaga na Wapare walikuwa na ujanja wa kumpinga Mwalimu.

..kama wengekuwa wajanja kiasi hicho, basi Mwalimu angevunja vyama vya ushirika vya maeneo mengine kama NYANZA, na kuacha vile vya Kilimanjaro -- KNCU na VUASU.

..kuna wafanya biashara wengi tu wakubwa walikuwepo tangu miaka ya Nyerere. wako waliokuwa na mashamba makubwa, wengine walikuwa na magari ya mizigo, mabasi, etc etc.

..siyo kwamba nashangazwa na wananchi wa Kusini tu. nashangazwa na wa-Tanzania wote walivyoshindwa kumdhibiti Mwalimu Nyerere pale siasa zake zilipowaumiza wananchi.

NB:

..hao wanasiasa uliowataja actually walitumiwa na Mwalimu na umuhimu wao ulipoisha akawabwaga.

..sikumbuki kama ni Eliufoo au Nsilo Swai aliyetumika katika kuvunja Umangi maeneo ya Uchagani.

..Chediel Mgonja, pamoja na kuacha kazi yake Ubalozini UN, na kurudi nyumbani akiwa na miaka 30, alikuja kutupwa vibaya na Mwalimu miaka ya 80.

..Mgonja, former minister of foreign affairs, education,sports and culture, alikuja kuishiwa mpaka akawa anaomba lifti kwenye magari ya mkaa na mafuta. Mwalimu alishindwa nini kumsaidia mjamaa mwenzake.

..KAMBARAGE ALIKUWA MJANJA, HAKUNA ZAIDI YAKE TANZANIA[/red].
 
Maana kuna "taarifa" kwamba alikuwa na "uhusiano" na Rais wetu wa kwanza .... ??!! ... sijui kama naweza ku-connect dots hapa.

Taarifa za "redio mbao" mbona zilimpakazia Nyerere na wengi tu, wapo waliodai ati alikuwa anamchukua Bibi Titi (ujana wake alikuwa na umbo lile la kimanyema hasa, tukunyema mpaka chini! Japo sijui kabila lake), ukiuliza ushahidi unaoneshwa picha ya Nyerere akicheza naye muziki kwenye party ya kusherehekea uhuru 1961! Wengine wakamsema na Secretary wake mzungu Joan Wickens, lakini yote hayo hayakuwahi kuthibitishwa beyond rumours! Na yalikuwa yanasemwa sambamba na yale mautani aliyokuwa anasemwa nayo mzee Kawawa, na ile "miujiza" ya kifimbo cha Nyerere, ambayo yote sidhani kama kuna lenye ukweli.
 
Taarifa za "redio mbao" mbona zilimpakazia Nyerere na wengi tu, wapo waliodai ati alikuwa anamchukua Bibi Titi (ujana wake alikuwa na umbo lile la kimanyema hasa, tukunyema mpaka chini! Japo sijui kabila lake), ukiuliza ushahidi unaoneshwa picha ya Nyerere akicheza naye muziki kwenye party ya kusherehekea uhuru 1961! Wengine wakamsema na Secretary wake mzungu Joan Wickens, lakini yote hayo hayakuwahi kuthibitishwa beyond rumours! Na yalikuwa yanasemwa sambamba na yale mautani aliyokuwa anasemwa nayo mzee Kawawa, na ile "miujiza" ya kifimbo cha Nyerere, ambayo yote sidhani kama kuna lenye ukweli.

Hii ya tukunyema kazi kweli kweli sina mbavu tena hapa, LOL
 
Field Marshall ES,

Mkuu Field Marshall ES Heshima, na wengineo pia heshima mbele. Huu mjadala nami umenifanya nimjue huyu Dr. Kleruu, na zaidi Mwamwindi ambaye nilikuwa sijui haya. Sasa nataka Mkuu FM ES hapo unapozungumzia Mwalimu Nyerere anajutia kifo kimoja alichoidhinisha, huenda hapa tunacheza na lugha, katika vifo 10 (kama nadhani Kuhani alipoonesha majibu bungeni, vilivyotekelezwa awamu ya kwanza), huenda ni hicho cha Mwamwindi tu ndio anaona hakuwa fare. Lakini vile tisa alivyoviafiki huenda anaona kulikuwa hakuna tatizo. Ni hayo tu wakuu.
 
Mkuu Field Marshall ES Heshima, na wengineo pia heshima mbele. Huu mjadala nami umenifanya nimjue huyu Dr. Kleruu, na zaidi Mwamwindi ambaye nilikuwa sijui haya. Sasa nataka Mkuu FM ES hapo unapozungumzia Mwalimu Nyerere anajutia kifo kimoja alichoidhinisha, huenda hapa tunacheza na lugha, katika vifo 10 (kama nadhani Kuhani alipoonesha majibu bungeni, vilivyotekelezwa awamu ya kwanza), huenda ni hicho cha Mwamwindi tu ndio anaona hakuwa fare. Lakini vile tisa alivyoviafiki huenda anaona kulikuwa hakuna tatizo. Ni hayo tu wakuu.

Mfumwa,

Nashukuru umekuja na macho yaliyo na nguvu na kuliona hilo kuwa Nyerere alijutia hukumu moja ya kifo aliyoidhinisha kwa kuwa dhamira yake ilimsuta. Hao tisa wengine wala hakujigusa na nakumbuka vizuri kuna Mhindi ambaye alinyongwa kwa kumuua mkewe kwa makusudi ili apate bima ya maisha! Huyu Mdosi, inasemekana Nyerere wala hakusubiri muda kutafakari maana huyo mke alikuwa ama wa pili au watatu kufa kwenye "ajali"!
 
Mfumwa,

Nashukuru umekuja na macho yaliyo na nguvu na kuliona hilo kuwa Nyerere alijutia hukumu moja ya kifo aliyoidhinisha kwa kuwa dhamira yake ilimsuta. Hao tisa wengine wala hakujigusa na nakumbuka vizuri kuna Mhindi ambaye alinyongwa kwa kumuua mkewe kwa makusudi ili apate bima ya maisha! Huyu Mdosi, inasemekana Nyerere wala hakusubiri muda kutafakari maana huyo mke alikuwa ama wa pili au watatu kufa kwenye "ajali"!

Hiyo kesi nakumbuka hata wakili mmoja aitwaye Mwakasungula alikuwa anaitumia kama mfano mmojawapo kwenye kitabu chake "Kesi za Jinai", ambacho kilikuwa kinatumika pia kufundishia mahakimu mahakama za mwanzo kule Mzumbe zamani.
 
Lucy Lameck alifariki baada ya kuugua muda mrefu. Alilazwa muda mrefu tu pale hospitali ya KCMC, lakini kwa hakika sifahamu ni nini kilichokuwa kikimsumbua.

Nijuavyo ni kwamba Lucy Lameck alifariki kutokana na matatizo ya ini.
Nadhani alikuwa anapiga (pombe) kupita kiasi. Nilikutana naye Paris nyumbani kwa balozi Tatu Nuru (rip) yeye alikuwa anapiga brandy kavu kavu.
 
Mwalimu Nyerere anajutia kifo kimoja alichoidhinisha, huenda hapa tunacheza na lugha, katika vifo 10 (kama nadhani Kuhani alipoonesha majibu bungeni, vilivyotekelezwa awamu ya kwanza), huenda ni hicho cha Mwamwindi tu ndio anaona hakuwa fare. Lakini vile tisa alivyoviafiki huenda anaona kulikuwa hakuna tatizo. Ni hayo tu wakuu.

Mkuu Mfumwa Heshima yako bro, dawa ya kutocheza na lugha ni kuleta copy za executive orders alizosaini Mwalimu kwa ajili ya vifo vya wananchi 10, nina uhakika kwa 100%, kua nimeisoma hiyo habari somewhere, Mwalimu akihojiana na Ulimwengu wakati wa uchaguzi wa rais 1995, as a nation nimewahi kuona mengi sana ya ajabu kuhusu taifa langu kwamba sina tatizo kuamini kuwa kuna uwezekano mkubwa kuwa ziliwekwa saini za wengine kwenye hao wengine tisa,

Na ninarudia tena kua sina mapenzi sna na Mwalimu na policies zake, lakini siwezi kumsingizia anything, hasa la uuaji Mwal;imu hakuwa muuaji kwa sababu angekuwa basi angeua wengi sana, infact hata Kambona alikamatwa Airport ya Nairobi, Mwalimu aliwaambia wamuache aende anakotaka, Babu alitakiwa kuuliwa kule visiwani, lakini Mwalimu akamuokoa, Salim alitakwia kuuliwa kuel visiwani lakini Mwalimu akamuokoa, sasa kwa wale mnaomchukia sana Mwalimu, ni haki yenu na ikibidi tupeni sababu badala ya kujaribu kujificha ficha nyuma ya ishus zisizokuwa na kichwa wala miguuu,

Ushaidi uliotolewa bungeni umesema kuwa walinyongwa watu 10 under awamu ya kwanza, kama tatizo ni kum-gotcha Mwalimu, ambaye I have absolutely no love for mnahitaji more than huo ushahidi wa bungeni, wakati umefika sasa tumuache Mwalimu apumzike, mkuu Mfumwa ahsante kwa darasa lako na ninashukuru kwamba huwa linatokea pale tu inapotokea ishu na mtu mmoja, that is wasup lakini ahsante sana.

Lakini pia sina tatizo kukubali hoja yako kuwa alisaini vifo vya wananchi 10, kama itakuletea amani bro!
 
Field Marshall ES,

FMES is right...ni kweli kulikuwa na hizo hukumu,lakini mpaka Mwalimu anatoka madarakani hayo ma file yalikuwa bado yako kwenye desk lake bila ya signature yake.Aliye sign alikuwa Mwinyi,fuatilieni jamani
 
Mwalimu alikuwa anatimiza jukumu la KIKATIBA la RAIS wa NCHI. Maoni ya baadhi wenzetu hapa ni kama vile yeye ndiye alikuwa amehukumu na kisha ametia sahihi watu wanyongwe. Kama kuna alioacha kutia sahihi wakati wengine amefanya hivyo, pengine hilo ndilo la kuangalia. Mwalimu aliiheshimu sana KATIBA.

Kuhusu vijiji vya ujamaa kwa kweli huu ulikuwa ni UKOMBOZI mkubwa kwa tulio wengi. Tuliweza kupelekwa shule baada kutolewa huko porini tulikokuwa tunaishi, kwa mara ya kwanza tulitibiwa kwenye zahanati; UTANZANIA wetu ulijengeka maradufu; na hadi leo tunaishi kwenye vijiji hivi.
 
.
Kuhusu vijiji vya ujamaa kwa kweli huu ulikuwa ni UKOMBOZI mkubwa kwa tulio wengi. Tuliweza kupelekwa shule baada kutolewa huko porini tulikokuwa tunaishi, kwa mara ya kwanza tulitibiwa kwenye zahanati; UTANZANIA wetu ulijengeka maradufu; na hadi leo tunaishi kwenye vijiji hivi.

Mheshimiwa WildCard

Hivyo vijiji vya ujamaa vilivyokusaidia kusoma vilivyoko hadi leo viko wapi,mkoa gani wilaya gani na vinaitwaje? Na vilikusaidia kusoma hadi darasa la ngapi?
 
Mheshimiwa WildCard

Hivyo vijiji vya ujamaa vilivyokusaidia kusoma vilivyoko hadi leo viko wapi,mkoa gani wilaya gani na vinaitwaje? Na vilikusaidia kusoma hadi darasa la ngapi?

Mh! Niulize na jina langu kabisaa...
 
FMES is right...ni kweli kulikuwa na hizo hukumu,lakini mpaka Mwalimu anatoka madarakani hayo ma file yalikuwa bado yako kwenye desk lake bila ya signature yake.Aliye sign alikuwa Mwinyi,fuatilieni jamani

Zanaki,

Unasema tufuatilie, lakini sijui na wewe mwenyewe umefuatilia kilichoandikwa humu ? Waziri kasema "watu 10 walinyongwa wakati wa awamu ya kwanza." Hakusema kulikuwa kuna hukumu 10. Ina maana siku Nyerere anakabidhi funguo walikuwa tayari wameshanyongwa mtu 10. Haiwezekani Mwinyi akaja kutia saini kwa yeyote wa hawa watu 10 kwa sababu yeye alipokuja, 1986, hawa kumi walikuwa wameshauliwa "wakati wa awamu ya kwanza." Ok ? Wewe unaongelea wale waliokuwa kwenye death row siku Nyerere anatoka Ikulu halafu labda wakanyongwa baadae katika kipindi cha awamu ya pili na saini ya Mwinyi, lakini hao wamo katika idadi ile ya 72 ya walionyongwa wakati wa awamu ya pili. Na katika hao 72 nachelea kusema kuna aliyehukumiwa wakati wa Nyerere akanyongwa wakati wa Mwinyi, kwa sababu sidhani Rais mteule anaweza kusukumiziwa mafaili ya death warrant akayakuta mezani baada ya mstaafu kukaa nayo akayawekea wekea usiku weee mpaka yamkute mwingine na yeye akubali kusaini. I don't think so. Mwinyi atakuwa alisaini mafaili ya death warrant aliyoletewa yeye na Mahakama, siyo Nyerere aliyo ya side step. Lakini hizi zote ni speculation, hatuna details za transition protocol za death warrants. Cha uhakika ni kwamba Waziri wa Sheria kasema watu 10 walinyongwa - sio walihukumiwa - walinyongwa wakati wa Awamu ya kwanza.

Oh yeah, Nyerere alikuwa amesafiri mara tisa kati ya kumi, ni Kawawa tu huyu!

Kwani nae amefariki?

Ahaa, kwa hiyo kumbe ishu ni kutolaumu waliofariki. Ok sawa. Nilitaka kujua tu kigezo kipya cha kumtetea Mwalimu. Ok. Mara ya mwisho ilikuwa ni "Mwalimu sio Malaika."
 
mwamwindi alikuwa rc wa iringa na kama alikuwa mwanamapinduzi hasa sielewi isipokuwa siku hiyo ya x-mas rc huyo nafikiri mauti yalikuwa yanamnyemelea aliondoka peke yake bila dereva kwenda isimani sehemu maarufu kwa kilimo cha mahindi sahemu inaitwa mkungugu akiwa ktk gari yake ya mkuu wa mkoa 504 enzi hizo peke yake bila dereva wala mlinzi,
akenda moja kwa moja shambani kwa huyo bwana na akamkuta huyo bwana analima kwa trekta yake rc huyo alikuwa ni mtu jeuri na mwenye kiburi,

alipofika shambani ktk kujibizana kwao ialimprovoke mwamwindi, na mwamwindi akamwomba wwaende wakaongee nyumbani kwake yeye akaendesha trekta lake na rc akiwa ktk 504 yake kuika nyumbani ambapo c mbali na shambani(NYUMBA YA SHAMBANI)akamwambia rc ningoje nakuja alipoingi ndani akatoka na bunduki akamtwanga risasi ya begani rc akamwomba msamaha pamoja na kupiga magoti kumsihi huyo bwn lkn jamaa hakurudi nyuma akampiga nyingine na kummalizia,akapandisha maiti ktk buti ya 504 na kuipeleka kituo kikuu ch polisi iringa kama km 40 hivi toka shambani,

aipofika pale akawaambia polisi nimeleta/kachukueni mbwa wenu kwenye gari yeye akaondoka.nafikiri ni kitu polisi hawakuamini maana hat kumkamata walimfuata nyumbani kwake eneo la mshindo karibu na kanisa katoliki si mbali na samora stadium, hii ikiwa ni nyumba yake anayoitumia akiwa mapumzikoni mjini
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom