WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,457
- 956
gm,
1...malengo ya kuanzisha vijiji vya ujamaa ilikuwa ni pamoja na kuwaweka wananchi karibu na, pamoja na kurahisisha kuwapatia, huduma za kijamii, kama barabara,maji,shule,..
..sasa kwa kigezo hicho tu, tayari kulikuwa na maeneo,haswa ya kule uchagani,ambako kwa kweli misingi ya infrastuctures mbalimbali ilishakuwepo.
..pia haikuwa busara kuwahamisha wakulima wa zao la kudumu kama kahawa.
..sikumbuki kahawa iliingia lini Kilimanjaro, lakini naamini ilikuwa miaka zaidi ya 50 kabla ya operesheni vijiji.
..maeneo ya Upareni settlements zao ziko kijamaa-jamaa. zaidi, wana tatizo kubwa sana la ardhi, na hakuna mapori ambayo ungeweza kupima vijiji vipya vya ujamaa.
.2..nadhani utakubaliana na mimi kwamba Kilimanjaro was a unique case, na kulikuwa hakuna ulazima wa zoezi wa operesheni vijiji.
..halafu things went so wrong ktk mikoa mingine, ilibidi zoezi zima lisitishwe.
NB:
kwa upande mwingine napingana na wale wanaodai kwamba alichofanya Mwawindi ilikuwa ni ushujaa.
..ppl had not exhausted every peaceful option ktk kupinga operesheni vijiji.
..hata UHURU wetu hatukupata kwa mapambano ya silaha.
Je yale malengo ya kuanzishwa vijiji yalifanikiwa?
Iliwahi kufanyika tathmini yoyoye kuona kama kulikuwa na ufanisi ama lah?..
Je itakuwa sahihi kusema kuwa operesheni Vijiji ilipelekea sehemu nyingine za Tanzania kurudi nyuma kimaendeleo badala ya kupiga hatua?