Dkt. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

Masanja,

..unajua kuna watu wanafikiri kutoa visingizio vya ajabu-ajabu kama hivyo hapo juu wanamtetea, kumlinda, na kumuenzi, Baba wa Taifa.

..ku-suggest kwamba Mwalimu Nyerere alikasimisha mamlaka yake ya kusaini death-warrants kwa watu wengine ni kumtukana matusi makubwa kabisa.




Mwikimbi,

..Peter Kisumo, akiwa mkuu wa mkoa, ndiye aliyemshawishi Mwalimu kutokupeleka operesheni vijiji Kilimanjaro.

..kuna sababu nyingi tu zikiwemo za kihistoria, kisiasa, kijiografia, na hata kiuchumi, kwamba zoezi hilo lingeleta madhara makubwa, na lilikuwa halitekelezeki, katika maeneo mengi ya Kilimanjaro.

..Kithuku ameleta maelezo ya kina kuhusu maeneo ambayo vijiji vya ujamaa vilianzishwa Kilimanjaro. lakini utaona kwamba zoezi hilo lilitekelezwa ktk maeneo ambayo kiasili yamekuwa hayakaliwi na makabila makubwa ya Kilimanjaro--Wachaga na Wapare.

Jokakuu,

Maelezo yako ni mazuri na yanaleta mwanga kidogo kuhusu nini kiliendelea wakati ule, kwa mtizamo wangu ninaona kama hii siasa ya ujamaa na vijiji ilikuwa tayari haifai hata kabla haijaanza, kwa sababu huwezi ukalazimisha watu wa sehemu au mikoa fulani kuhama wakati sehemu zingine hawafanyi hivyo. Kwa mtizamo wangu Nyerere angechukua mda yeye na washauri wake kuangalia jambo hilo katika angle nyingi tofauti kabla hawajaamua kuwatoa watu baruti katika maeneo yao kwa jina la kujenga taifa!!
 
Cheki rekodi zako mzee,huyu mama ni kweli aliua watoto wake wakati Mwalimu akiwa rais lakini aliyemwachia huru alikuwa ni Mwinyi...na alisema kuwa huyu mama kishapata adhabu ya kutosha.

Shukrani kwa Sahihisho Zanaki!!!,Ni kweli kwamba aliyemuachia Huru Mama Agnes Liundi ni Mzee Mwinyi baada ya Jumuiya ya Wanawake kumuombea Msamaha kwa Mzee Mwinyi.Nashukuru tena kwa ufuatiliaji wako...maana vinginevyo tutapindisha habari.
 
Shukrani kwa Sahihisho Zanaki!!!,Ni kweli kwamba aliyemuachia Huru Mama Agnes Liundi ni Mzee Mwinyi baada ya Jumuiya ya Wanawake kumuombea Msamaha kwa Mzee Mwinyi.Nashukuru tena kwa ufuatiliaji wako...maana vinginevyo tutapindisha habari.

Mwawado,

Ndiyo JF hiyo kuna kusahihishana na kukosoana na kupeana habari ambazo wengine hatuzijui kabisa! Thanks both of you Zanaki and Mwawado!
 
Mwamindi anachukuliwa kama shujaa wa Kihehe huko Iringa.Dr Kleruu alichukiliwa kama kiongozi mwanamapinduzi shujaa.Kwa hali iliyopo sasa hivi nani shujaa wa kweli?Naona ni Mwamindi ambaye hakutaka kunyanyasika na ubabe wa sera potofu za vijiji vya ujamaa.Enzi zile zilikuwa ni enzi za udikteta ulikolea na ziliwanyima watu uhuru na haki zao za kimsingi katika nchi.Nyerere...atakumbukwa kwa ukaidi na ubabe wake!!!
 
kleruu alikuwa pia na binti tulikaa naye mitaa ya daimond jubilee,upanga nakumbuka tulikuwa tunamwita mama twambi,unfortunately binti wa huyu mama,TWAMBI,perished in the fire iliyotokea katika boarding school kilimanjaro some years ago
...Shauritanga????
 
gm said:
Maelezo yako ni mazuri na yanaleta mwanga kidogo kuhusu nini kiliendelea wakati ule, kwa mtizamo wangu ninaona kama hii siasa ya ujamaa na vijiji ilikuwa tayari haifai hata kabla haijaanza, kwa sababu huwezi ukalazimisha watu wa sehemu au mikoa fulani kuhama wakati sehemu zingine hawafanyi hivyo. Kwa mtizamo wangu Nyerere angechukua mda yeye na washauri wake kuangalia jambo hilo katika angle nyingi tofauti kabla hawajaamua kuwatoa watu baruti katika maeneo yao kwa jina la kujenga taifa!!

gm,

..malengo ya kuanzisha vijiji vya ujamaa ilikuwa ni pamoja na kuwaweka wananchi karibu na, pamoja na kurahisisha kuwapatia, huduma za kijamii, kama barabara,maji,shule,..

..sasa kwa kigezo hicho tu, tayari kulikuwa na maeneo,haswa ya kule uchagani,ambako kwa kweli misingi ya infrastuctures mbalimbali ilishakuwepo.

..pia haikuwa busara kuwahamisha wakulima wa zao la kudumu kama kahawa.

..sikumbuki kahawa iliingia lini Kilimanjaro, lakini naamini ilikuwa miaka zaidi ya 50 kabla ya operesheni vijiji.

..maeneo ya Upareni settlements zao ziko kijamaa-jamaa. zaidi, wana tatizo kubwa sana la ardhi, na hakuna mapori ambayo ungeweza kupima vijiji vipya vya ujamaa.

..nadhani utakubaliana na mimi kwamba Kilimanjaro was a unique case, na kulikuwa hakuna ulazima wa zoezi wa operesheni vijiji.

..halafu things went so wrong ktk mikoa mingine, ilibidi zoezi zima lisitishwe.


NB:

..kwa upande mwingine napingana na wale wanaodai kwamba alichofanya Mwawindi ilikuwa ni ushujaa.

..ppl had not exhausted every peaceful option ktk kupinga operesheni vijiji.

..hata UHURU wetu hatukupata kwa mapambano ya silaha.
 
Mwamindi anachukuliwa kama shujaa wa Kihehe huko Iringa.Dr Kleruu alichukiliwa kama kiongozi mwanamapinduzi shujaa.Kwa hali iliyopo sasa hivi nani shujaa wa kweli?Naona ni Mwamindi ambaye hakutaka kunyanyasika na ubabe wa sera potofu za vijiji vya ujamaa.Enzi zile zilikuwa ni enzi za udikteta ulikolea na ziliwanyima watu uhuru na haki zao za kimsingi katika nchi.Nyerere...atakumbukwa kwa ukaidi na ubabe wake!!!

Alnadaby,

Point yako nzuri, ila nani shujaa zaidi inakuwa debatable kidogo, kwa kiasi fulani wote wawili wanaonekana kuwa mashujaa katika vioo tofauti vya jumuiya yetu, issue inakuja kuwa Mwamwindi alikuwa shujaa kwa kuuwa au kwa kupinga siasa ya ujamaa? au Dr. Kleruu alikuwa mwanamapinduzi kwa kuwakomalia watu kuhama hata kuwaprovoke kama alivyofanya kwa Mwamwindi, Je alitumia madaraka yake vizuri?. At the end of the day nafikiri kitu tunaweza kupata hapa ni mafunzo ambayo yanaweza kutuweka katika hali ya kuiangalia historia yetu na kujifunza kutokana na yaliyotokana. Bottom line ni kuwa nani shujaa na nani mwanamapinduzi inakuwa debatable with compelling evidences or circumstances either or against!
 
Cheki rekodi zako mzee,huyu mama ni kweli aliua watoto wake wakati Mwalimu akiwa rais lakini aliyemwachia huru alikuwa ni Mwinyi...na alisema kuwa huyu mama kishapata adhabu ya kutosha.

Kwa faida ya wasiomjua, huyo mama aliua WATOTO WATATU ambao walizikwa makaburi ya pale Wapiwapi (Maduka mawili) Chang'ombe. Mtoto aliyeponea hospitali Mhimbili ni TAJI LIUNDI (kunradhi kutaja jina lake lakini hii ni historia). Sasa nirudi kwenye mada yetu.

Dr. Kleruu kwa kweli alikuwa kero sana kwa watu wengi sio tu kwa Mwamwindi. Kuna ushahidi tosha kwamba alikuwa anamsumbua huyo mkulima maarufu mara kwa mara ili akiachie mashamba yake kijiji cha ujamaa ingawa aliyaendeleza kitaalamu na kulisha Iringa na nchi mzima. Lililojiri katika mtima wa Kleruu ni wivu na kumkomoa Mwamwindi sababu ya utajiri wake na ndio akatumia ubabe wa cheo na madaraka yake. Hii inanikumbusha John Anderson Nzunda aliyekuwa RC wa Mtwara miaka ya '60 aliyewachapa viboko wananchi akisaidiwa na DC Kabongo kule Newala kwa kutohudhuria mkutano wa hadhara.

Hivi hizi takwimu za walionyongwa wakati wa Awamu mbali mbali zinaashiria nini? Tukumbuke Nyerere pia aliua watu kwa kuwaweka detention (Mwinyi hakudetain hata 'mpinzani mmoja' ingawa alitukanwa na kuchorwa matusi ya ndani ya nguo na wanafunzi wa UDSM), Nyerere aliua Waganda na Watanzania walikufa katika vita dhidi ya Idi Amini, na aliidhinisha uvamizi usiotangazwa huko Biafra, Msumbiji, Shelisheli, Ngazija, n.k. Hawa wapiga debe wa kumtukuza tuuu na "kumfutia madhambi Mwalimu" lengo lao nini? Au ndio aweze kupata huo "utakatifu" kutoka vatican?? Ni vema sasa tuweke bayana madhila tuliyoyapata Watanzania katika utawala wake na ikiwezekana tuendeshe MOOT COURT na ipitishwe judgement posthumously!!
 
Bila kuona haya nadhani katika hii issue Mwamwindi ndiye shujaa. Hakukubali ushenzi na uonevu usiokuwa na maana, hivyo alikuwa tayari kufa kuliko kuona uchafu huo.

Tanzania ya sasa inahitaji watu kama Mwamwindi ambao watasimama na kupigania haki zao na nchi yao. Tungekuwa na akina Mwamwindi wengi hapa Tanzania basi hata pesa za EPA zingerudi.

...Dr Kleruu alichukiliwa kama kiongozi mwanamapinduzi shujaa.Kwa hali iliyopo sasa hivi nani shujaa wa kweli?Naona ni Mwamindi ambaye hakutaka kunyanyasika na ubabe wa sera potofu za vijiji vya ujamaa.Enzi zile zilikuwa ni enzi za udikteta ulikolea na ziliwanyima watu uhuru na haki zao za kimsingi katika nchi.Nyerere...atakumbukwa kwa ukaidi na ubabe wake!!!

Unajua Mbaraka Mwinshehe kwenye wimbo wake wa kumuenzi "Shujaa Mwanamapinduzi," alisema kwamba "kifo chake dokta kimetusikitisha sisi wakulima wote." Inawezekana kabisa hiyo ndio ilikuwa hisia iliyotawala wakati ule. Lakini Alnadaby na Kidatu mlichosema hapo ni kitu muhimu ambacho ni mara chache kinafanywa Tanzania: revisionist history. Mnaangalia upya vitu ambavyo kwa muda mrefu tumekuwa tukiviangalia kupitia lenzi chujio ya Chama na Serikali tu. Na miaka 50, 100 ijayo watakuja kizazi kingine na revisionist historians wao, watasema, wait a minute now, hawa wanamapinduzi hawa na waasisi wa nchi na ma hero yaweza kuwa sio ma hero hata kidogo. Tutakuja kugundua kwamba tumeimbishwa mapambio ya kuabudu sera na mashujaa wakati ilikuwa ni hoodwinking na propagandazing ya chama ambayo, bahati mbaya, mpaka leo inaaminiwa na mamilioni ya Watanzania.

Mwinshehe atasemaje kifo cha Dr. Kleruu kilisikitisha wakulima wote wakati serikali ilikuwa inabidi itumie dola kulazimisha watu wahame makwao kwenda ku clear vichaka kutengeneza vijiji vipya? Isitoshe ni wakulima ndio walimuua huyu Dr. Kleruu!
 
Kuhani,

Kuhani,

Nakubaliana na wewe na ndio hasa kitu kilichonifanya nianzishe hii thread, nimekuwa nikiusikia wimbo huo wa marehemu Mbaraka Mwinshehe kumhusu Dr Kleruu na sikuwa na hata fununu huyu Dr. Kleruu alikuwa nani na alifanya nini. Kwa kipindi cha siku mbili nimejifunza mengi sana kumhusu huyu bwana na hata wakati mwingine naona kama huu wimbo haukuwa na maana kabisa hata kuwepo!
 
gm,alnabady,kjnne46,

..pamoja na taabu zote hizo mbona hakukuwa na maandamano au harakati zozote zile kupinga operesheni vijiji?
 
gm,alnabady,kjnne46,

..pamoja na taabu zote hizo mbona hakukuwa na maandamano au harakati zozote zile kupinga operesheni vijiji?

JokaKuu,

Kama aliyepingandiye huyu aliyenyongwa unafikiri kuna yeyote angetokea kupinga?

Kwa kweli sina uhakika vizuri na historia ya kipindi hicho ila ninachojua miaka ya nyuma ulikuwa ukipinga siasa za Nyerere unaishia kizuizini na kama sikosei usalama wetu wa taifa hadi leo unaoperate kwa siasa za kutisha watu na wala sio za kiuchunguzi au intelligence ambayo inaweza kuleta maendeleo ya nchi.
 
JokaKuu,

Kama aliyepingandiye huyu aliyenyongwa unafikiri kuna yeyote angetokea kupinga?

Kwa kweli sina uhakika vizuri na historia ya kipindi hicho ila ninachojua miaka ya nyuma ulikuwa ukipinga siasa za Nyerere unaishia kizuizini na kama sikosei usalama wetu wa taifa hadi leo unaoperate kwa siasa za kutisha watu na wala sio za kiuchunguzi au intelligence ambayo inaweza kuleta maendeleo ya nchi.

Umejibu sawa kabisa, JokaKuu. Enzi hizo kulikuwa hakuna uhuru wa kuandamana na ukionekana unasema au unakwenda kinyume na yale ya Nyerere na watawala wake wa mabavu basi UNASWEKWA KIZUIZINI, utatengwa au hata kuhamishiwa mji, wilaya, mkoa mwingine na huna kukata rufaa ama mtu wa kumlalamikia. Hali ilifikia pabaya hadi Mwalimu aliitwa "Mussa" kwa sababu akitoa "amri tu" bila mjadala. Tafadhali naomba moada hii ya Nyerere iletwe peke yake tutoe mifano na ushahidi wa "the other side of Mwalimu".
 
Umejibu sawa kabisa, JokaKuu. Enzi hizo kulikuwa hakuna uhuru wa kuandamana na ukionekana unasema au unakwenda kinyume na yale ya Nyerere na watawala wake wa mabavu basi UNASWEKWA KIZUIZINI, utatengwa au hata kuhamishiwa mji, wilaya, mkoa mwingine na huna kukata rufaa ama mtu wa kumlalamikia. Hali ilifikia pabaya hadi Mwalimu aliitwa "Mussa" kwa sababu akitoa "amri tu" bila mjadala. Tafadhali naomba moada hii ya Nyerere iletwe peke yake tutoe mifano na ushahidi wa "the other side of Mwalimu".

Kjnne46,

Thanks!

Wakati Mbaraka Mwinshehe anaimba wimbo wa Dr. Kleruu shujaa wetu na mwana mapinduzi, unafikiri kulikuwa na waimbaji wangapi kipindi kile, mbona hata mmoja asimuimbe Mwamwindi? Freedom of expression imeanza kuingia Tanzania miaka ya karibuni na bado kuna vitu unaweza kujiexpress na vingine huwezi!
 
Mkuu Masanja, ahsante kwa elimu yako nzito sana, lakini kuna maandishi yako wazi Mwalimu akihojiwa na Ulimwengu, ambapo alisema kuwa siku zote za mwisho wa maisha yake amekwua akitembea na
Biblia kila mahali, na ksuali kwa nguvu zake zote ili Mungu amsamehe kutokana na kifo kimoja tu alichokiidhinisha cha Mwamwindi,

Siko hapa as an-apologetic man wa kiongozi yoyote, lakini kama mwenyewe alisema kwua amesaini kifo cha raia mmoja, siwezi kwenda kinyume, kwangu ina maana moja kwamba kuna wanaoukaimu urais alipokuwa hayupo, ambao walisaini either on his behalf au else, lakini kwa maneno yake mwenyewe ni kwamba aliasaini kifo cha Mwamwindi tu!

Ahsante Mkuu.
 

.. kuna maandishi yako wazi Mwalimu akihojiwa na Ulimwengu, ambapo alisema kuwa siku zote za mwisho wa maisha yake amekwua akitembea na
Biblia kila mahali, na ksuali kwa nguvu zake zote ili Mungu amsamehe kutokana na kifo kimoja tu alichokiidhinisha cha Mwamwindi,

... kama mwenyewe alisema kwua amesaini kifo cha raia mmoja, siwezi kwenda kinyume, kwangu ina maana moja kwamba kuna wanaoukaimu urais alipokuwa hayupo, ambao walisaini either on his behalf au else, lakini kwa maneno yake mwenyewe ni kwamba aliasaini kifo cha Mwamwindi tu!

Yaweke hapa basi kama yako wazi hayo maandishi.

Watu kumi wamenyongwa halafu tisa wote wawe sio kwa saini ya Rais mwenyewe ? Yani huyo makamu yeye kila siku Rais akisafiri saini za kunyonga zinamkuta yeye tu, na yeye anaona poa ? Re-think that, man.
 
Mkuu sina mpango kabisa wa kuigeuza hii kuwa big deal, nimesoma wka macho yangu haya maneno ya Mwalimu, nikiyaona nitayaweka nisipoyaona wala siwezi kukosa usingizi, kwa sababu siwezi kukurupuka na this thing bila ya sababu,

I am not na never a Mwalimu, apologist kama unataka ku-score a point na hii ishu uanweza kuamini kuwa umeshinda, ila one thing siwezi kuamini tofauti na maneno ya Mwalimu, kwa sababu ninaamini kwua Mwalimu alikuwa na matatizo mengi sana, lakini kusema uongo on serious ishus kama hii halikuwa lake,

Ingawa pia na wewe unaweza kuleta hizo executive orders alizosaini kwenye vifo 10, otherwise sioni anything serious, kwa sababu the botomline Mwalimu hakwua muuaji, pamoja na matatizo yake mengi sana.

Okay later!

Ahsante Mkuu.
 
Masanja,

..unajua kuna watu wanafikiri kutoa visingizio vya ajabu-ajabu kama hivyo hapo juu wanamtetea, kumlinda, na kumuenzi, Baba wa Taifa.

..ku-suggest kwamba Mwalimu Nyerere alikasimisha mamlaka yake ya kusaini death-warrants kwa watu wengine ni kumtukana matusi makubwa kabisa.




Mwikimbi,

..Peter Kisumo, akiwa mkuu wa mkoa, ndiye aliyemshawishi Mwalimu kutokupeleka operesheni vijiji Kilimanjaro.

..kuna sababu nyingi tu zikiwemo za kihistoria, kisiasa, kijiografia, na hata kiuchumi, kwamba zoezi hilo lingeleta madhara makubwa, na lilikuwa halitekelezeki, katika maeneo mengi ya Kilimanjaro.

..Kithuku ameleta maelezo ya kina kuhusu maeneo ambayo vijiji vya ujamaa vilianzishwa Kilimanjaro. lakini utaona kwamba zoezi hilo lilitekelezwa ktk maeneo ambayo kiasili yamekuwa hayakaliwi na makabila makubwa ya Kilimanjaro--Wachaga na Wapare.

Kwa kumbukumbu yangu wakati wa mchakato vijiji vya ujamaa Peter Abdallah Kisumo alikuwa waziri wa serikali za mitaa na maendeleo vijijini (ndivyo ilivyoitwa wakati huo). Wakati huo alikuwa kijana na alikuwa anavaa zile suti za "Chou en Lai" aina fulani kama zile anazopenda Mzee Malecela. Angalao ninayo sababu fulani ya kukumbuka hilo, lakini mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wa wakati huo simkumbuki.
 
Back
Top Bottom